USHUHUDA: Kuku wa kienyeji (Pure) - Biashara kichaa isiyo na tija

N


Nyongeza ndogo kwenye eneo la uzalishaji.Kuku huatamia mayai kwa siku 21.Fuatilia tarehe ya kwanza ya kuku wako wanapoanza kuatamia,jifunze mbinu za kuwafanya kuku wako waanze kuatamia na kutotoa kwa wakati mmoja.Mfano una kuku 10,unawalazimisha kuku 5 waanze kuatamia kwa pamoja (rejea masomo ya nyuma juu ya ufugaji wa kuku wa asili/kienyeji).

Siku ya 21 alfajiri wanyang'anye kuku waliokuwa wanaatamia vifaranga vyao kabla havijatoa milio,wape mayai mengine.Hawatatoka hapo hadi siku nyingine 21 zifike na watotoe vifaranga vingine.Wanyanyang'anye vifaranga na kuwaachilia wapumzike.Ukiwatunza kwa chakula cha uhakika na kinga za magonjwa majuma mawili/matatu wataanza kutaga tena.Idadi ya vifaranga na mayai atakayokupatia kila kuku haitakuwa ya mazoea.

Kanuni rahisi ni (1) Jua kitu cha kufanya (2) Jua namna ya kufanya (3) Kifanye.
Mambo haya hatupaswi kuyaweka hadharani kiasi hiki.Tanzania wengi wetu hatua ya kwanza na ya pili tupo vizuri sana ,tatizo lipo kwenye hatua ya tatu.Kenya kwenye hatua ya kwanza na pili wapo dhaifu kuliko sisi ila hatua ya tatu wametuacha mbali ndiyo maana baadhi yetu hatutaki kuweka kila kitu hadharani.

Tunalenga kufundishana wenyewe wanafaidi wapita njia kwa tuliyofundishana kisha wanaanza kutucheka nasi tunashangilia.
Bravo, watanzania tuamke na tufanye, utafiti mkubwa umefanywa juu ya huyu kuku hapa Tanzania, ni aibu kufanya mazoea
 
Tukiendekeza ukisasa tutaharibu uumbaji wa Mungu halisi. Waone watoto siku hizi walivyonenepeana kwa sababu ya haya mayai ya kisasa! Daima huwa nafurahia kuwaona wanangu wakiwa na maumbo mazuri bila kufutuka miili. Kuleni hayo mayai ya kisasa majibu mtayajua.
 
Ninaposema breed selection maana yake ni wewe kwenda kitaa kuchagua kuku wa kienyeji wakubwa,mf, kuchi, hii inachukua miaka mingapi?, hawa ukiwasupplement they are always big and heavier comparatively. My take: mleta mada ni copy cat na hajafanya consultation yoyote kwa wataalam, huu ni ugonjwa sugu kwa wajasiliamali wengi.

Addendum: hata kupeleka yai bovu sokoni kwa zama hizi ni aibu kwani kuna candling touch inayokuwezesha kujua kama yai ni bovu ama la, kauli ya mleta mada kuwa yai LA kienyeji (lililorutubishwa) huharibika haraka viz aviz lisilorutubishwa ni ulongo mtupu, the fact is yai lolote ukilitunza kwenye shelf temperature kama ya pwani huharibika haraka.
Kuhusu size ya kuku: kumbuka kuwa hata hawa kuku wa kisasa wanabodysize tofauti so is egg size na egg laying, kwa broiler for instance Ross ni wadogo kuliko arboacres, big dealers huchagua lines wa kufuga na siyo kujifugia tu


Hii kasumba ya watafiti wetu kufanya reaserch za kinadharia na kuzifungia kwenye makabati ndio kama hizi, Profesa wa Poultry anafungua bar badala ya kuwa na banda la kuku kufanya kwa vitendo. Mkuu nakubaliana na hoja zako, ziko sahihi katika level ya kitafiti, ila kibiashara mambo hayako hivyo. Umetoa mfano wa kuchi etc, kwa wafugaji wa kuchi wanaweza kusema neno hapa, kuchi ni kati ya kuku asilia wanaofanya vyema sana sokoni hasa kwa ukubwa wa maumbo yao, ila ni breed ngumu Zaidi katika kuzaliana. Majogoo ya kuchi hudominate matetea mengi Zaidi na kuwapiga majogoo mengine yasikaribie matetea, ila mating kwa kuchi ni tatizo. hata matetea wa kuchi hutaga mayai machache Zaidi kuliko aina nyingine za kuku asilia na hii ndio maana population ya kuchi huwa ni ndogo na haiongezeki kwa kasi.

Pia ifahamike, si jambo rahisi kufanya breed selection kama mtaalamu anavyodai hapa. Kuna baadhi ya breeds mfano kuroiller ya india, Imewagharimu miaka Zaidi ya 50 kwa KEGG FARM, wengineni mpaka miaka mia kupata pure breed ya kuku wanaohimili mazingira magumu, kuwa na maumbo makubwa na kiwango cha juu cha utagaji. na kwa vile kampuni hutumia gharama kubwa sana katika hili, formula la kufanya breed selection hubakia siri ya kampuni, wao huuza parents tu kwa dealers na dealers wao wanauza commercial breeds. Selection inahitaji utaalamu wa juu sana kuweza kubaini dominant na recessive genes ili kupata aina ya kuku unayohitaji. Uzuri wenzetu waliofanikiwa wameshatusaidia kwenye hili la breed selection na izo breeds zipo mtaani ikiwamo wale wanaoitwa wamalawi pamoja na kwamba crosses wengi ni third to tenth generation huwa hawafanyi vyema sana.

Kweli kupeleka mayai mabovu sokoni ni aibu, ila kwa kiasi kikubwa mayai huaribikia yakiwa sokoni tayari na si kwa mkulima.Na sababu hii imefanya supermarket nyingi kutonunua mayai ya kienyeji bali wanakupa supplier a shelf ndani ya supermarket ili uweze kulihudumia. wao hukupa sehemu ya kuweka bidhaa zako, wao wanauza kwa niaba unakuja kuchukua mapato mzigo ukitoka, ila pia jukumu la supplier ni pamoja na kwenda mara kwa mara kubadili mayai yaliyopita muda wake na kuyaweka mapya kwa gharama zako mwenyewe. yale yaliyoharibila/kupita muda ni hasara yako supplier.

'' kauli ya mleta mada kuwa yai LA kienyeji (lililorutubishwa) huharibika haraka viz aviz lisilorutubishwa ni ulongo mtupu, the fact is yai lolote ukilitunza kwenye shelf temperature kama ya pwani huharibika haraka.''

Kunituhumu kusema uongo kwa mambo usiyoyajua ni si sahihi, kwa wale wanaofanya hatching wanaweza kuwa wanajua hili, yai lisilo na mbegu, hata likikaa kwenye incubator kwa siku 21, kwa joto kubwa Zaidi ya lile pwani la nyuzi joto 37.8 bado hubaki vile vile bila kubadilika wakati yale yenye mbegu huwa vifaranga. Na mara nyingi haya masalia ya mayai yasiyo na mbegu toka kwenye incubators / hatcheries baada ya siku ya 18 au 21 ndiyo yanayotumika sana kutengenezea baadhi bidhaa ikiwemo half cakes, chapatti, cakes etc.

Tafiti mnazofanya ni kati ya mambo bora sana kwaajili ya kuendeleza tasnia hii ya ufugaji hapa nchini, ila ni vyema mnavyofanya tafiti hizi angalieni tija ya tafiti zenu katika kufanya mapinduzi ya kibiashara ya ufugaji. kama findings za tafiti haziwezi kuwa na commercial impact basi naweza sema zina tija ndogo sana kibiashara.
 
Ginner
Nimekuelewa Mkuu vizur sana
Ila napenda kukusahihisha kidogo kwenye utagaji mayai kwa kuku wa kienyeji
Kwa uzoefu wangu wa miaka mitano kwenye ufugaji wa kuku wa kienyeji, kuku mmoja jike kwa mwaka anaweza kutaga mayai 150.
Ninachokifanya mimi kuku akianza kutaga huwa nampunguzia mayai hadi idadi ninayoitaka ikamilike ndo nampatia mayai yote tayari kwa kuatamia.
Then akitotoa ninamwacha wiki moja akilea vifaranga baada ya hapo namtoa kwenye chumba cha kulelea vifaranga [namwacha huru] akitoka nje hukaa wiki moja kisha huanza kutaga tena.
Ina maana ukizungusha hivyo kwa mwaka kuku mmoja anaweza kukupa vifaranga 150~ 200
Sema Changamoto Iko Kwenye Soko

Nawasilisha...
 
Kumekuwa na upotoshaji kwa baadhi wa watu wanaojiita wataalamu wa ujasiriamali, hasa wanaofanya shughuli za ufugaji kwa maandiko ya whatsapp bila kuwa na hata kuku mmoja bandani.

Nimesukumwa kuandika bandiko hili hapa kutokana na jumbe mbali mbali za uufugaji wa kimtandao unaoshawishi vijana kuwa watatajirika mapema kwa shughuli za ufugaji kwa kuanza na kuku wa kienyeji kumi na moja na kuweza kupata Zaidi ya kuku miatatu ndani ya kipindi cha mwaka mmoja wa uzalishaji. Hoja yao inaweza kuwa sahihi, ila ningependa kusisitiza mafanikio katika ufugaji hayapo katika idadi ya kuku unayomiki, bali ni namna ulivyoweza kumanage biashara ya ufugaji.

Hoja yangu leo hapa ni kwamba, Biashara ya kuku wa kienyeji hailipi na nikupoteza muda wako. Na nitatetea hoja yangu kwa mifano hai na uzoefu wangu katika ufugaji.

Biashara ya Mayai. (idadi isiyo na tija kibiashara)

Kwa asili ya kuku wa kienyeji,huwa wanatabia ya utagaji wa mayai 7-10 na mara nyingi ni siku kwa siku 10 mfululizo, utamiaji -siku 21, na uleaji wa vifaranga - siku 50-60. Hii inampelekea kwa kuku mmoja kuweza kutaga wastani wa mayai 35-50 kwa mwaka kwani anapoteza muda mwingi kwa shughuli za utamiaji na malezi ya vifaranga badala ya kutaga. Idadi hii ya mayai haina tija kibiashara kwani kuku mmoja anaweza kukuzalishia tray 1 mpka mbili kasoro pekee kwa mwaka ambayo kwa bei ya soko si Zaidi ya shilingi za kitanzania 20,000 tu kwa mwaka.

Changamoto kwenye soko la mayai ya kienyeji. (Uhifadhi wa mayai)

Mayai ya kienyeji ni kati ya bidhaa ngumu Zaidi kuhifadhika. Ikumbukwe kuwa tofauti na mayai ya kisasa, mayai ya kienyeji huwa yamerutubishwa na majogoo. Hivyo kuharibika ndani ya muda ya week moja au pungufu kama hayatatuzwa katika mazingira salama kwaajili ya utunzaji. Kipindi cha joto kali, mayai haya huanza kujitenenezea kifaranga au mishipa ya damu ambayo baada ya muda mfupi hugeuka viza na kutofaa kwa matumizi tena.

Kwa uzoefu wangu binafsi, nilianza kusambaza mayai ya kienyeji kwenye supermarkets miaka mitatu iliyopita. Nilipata changamoto kubwa sana ya kubadilisha mayai mara kwa mara kwani mteja akichukua yai viza ni kumpoteza kabisa. Hii ni changamoto ya kwanza ambayo mpaka sasa bado inasumbua wafugaji wengi.

Bei juu kwa mayai ya kienyeji

Gharama za mayai husika, bei ya mayai ya kienyeji iko juu ukilinganisha na gharama za mayai ya kuku wa kisasa. Soko kubwa la mayai ni pamoja na vibanda vya chips, migahawa na hoteli. hawa wanauhitaji mkubwa sana wa mayai na soko liko juu muda wote wa mwaka.

Soko la mayai ya kienyeji lipo Zaidi kwenye households(soko la familia) hasa kwa vigezo vya kuzingatia afya zaidi. Soko hili la familia sio kubwa, ni soko dogo na mara nyingi hutumia tray moja kwa kipindi cha wiki mbili au Zaidi. Kwa mzalishaji mkubwa wa mayai ya kienyeji ni lazma awe na soko la familia pana Zaidi kuweza kupata faida ndogo, nasema faida ndogo maana ili kuzalisha mayai tray kumi (mayai 300) kwa siku, utahitaji Zaidi ya matetea 700 mpaka 1000 ya kienyeji pure. idadi ambayo ni kubwa kuliko idadi ya mayai yanayopatikana.

Biashara ya Nyama

Na declare interest, mimi pia ni msambazaji wa nyama ya kuku wa kienyeji, hivyo naongea kwa uzoefu, na niko tayari kukosolewa. Pamoja na kufugwa katika misingi ya kijani (organic rearing), iyo pekee haitoshi kumpa thamani inayostahili huyu kuku sokoni.

Thamani ya kuku sokoni ni uzito alio nao, organic component ni jambo la ziada lililo muhimu pia. tunavyo jadili bei ya soko ya kuku huyu ni lazma tumliganishe na gharama za bidhaa pinzani zilizoko sokoni. Haitawezekana kumuuza kuku mwenye kilo moja au pungufu kwa bei ambayo tunashawishiana humu ya 15,000-20,000 wakati bidhaa pinzani (nyama nyeupe) kama samaki sato toka mwanza wanauzwakwa 7,500 kwa kilo, au kitimoto, nyama ya ngombe ambazo nazo kilo ni 7,500-8,000.

Hivyo basi, hoja yangu hapa ni uzito wa kuku husika. Ukiachana na jamii chache za kuku wa kienyeji (kuchi etc) wenye uzito mzuri, majority ya kuku pure wa asili/kienyeji kwa majogoo huwa na pungufu ya kilo moja na nusu. Kumbuka uzito wa kuku hawa sio kwasababu ya malisho duni, laah hasha, bali ni kutokana na vinasaba (genes) vyao kuwafanya kuwa na maumbo madogo madogo. kwa kuku wa aina hii, sitegemei mfugaji kama atafanikiwa kuwapeleka sokoni na kuweza kupata bei nzuri toka kwa mlaji wa mwisho.

Nini kifanyike?

Ili ufugaji uwe wenye tija kibiashara ufanyike, ni lazma wafugaji tuamke na kuachana na ufugaji wa kuku hawa asilia kwani hawana tija. Nikisema hivi simaanishi watu waache kufuga, hapana, ila wafuge aina /breeds za kuku zenye tija kibiashara. Kuku pekee unaoweza kuwafuga kwa mbinu za kienyeji na bado wakakuletea mfugaji faida nzuri kibiashara, ni kuku aina ya chotara (cross breeds). Hii ni aina ya kuku wenye sifa zote za ukienyeji kwa misingi ya mbinu zao za kuwafuga pamoja na namna walivyo nauwezo wa kuhimili mazingira hasa ya vijijini.

Kuna aina mbalimbali ya kuku hawa ikiwamo Black/ white australorps, kroiller, Rhodes island red, red hamshire, Sussex etc. Hawa ni kuku ambao wanaserve purpose zote za mayai na za nyama. Mfano kuku aina ya black/white australorps wao wanauwezo wa kutaga mpaka mayai 250 kwa mwaka, tofauti na wa kienyeji, mayai ya kuku hawa huwa makubwa na yenye kasha jeupe na kiini cha njano kama utawafuga kwenye mazingira na mbinu asilia (za kienyeji).

Ukilinganisha uwezo wa utagaji wa kuku hawa utagundua utagaji wao ni Zaidi ya asilimia 500% ukilinganisha na ule wa kienyeji pure. Idadi hii ya mayai toka kwa kuku mmoja kwa mwaka, anaweza kumwezesha mfugaji kuzalisha mayai kwa wingi na kushusha Zaidi bei ya mazao yake (mayai) kuwa chini kuweza kuliteka soko kwa urahisi Zaidi. Kumbuka, bei ya juu ya mayai ya kienyeji ni kwaajili ya kulipia gharama kubwa za utunzaji wa kuku huyu ilihali utagaji wake ni hafifu.

Pili, kuku hawa wana nyama nyingi Zaidi kuliko hawa wa kienyeji kwa majogoo hufikia mpaka uzito wa kilo 3-3.5. huku matetea hufikia kilo 2-2.5 na huwa na nyama nzuri, iliyokomaa vyema na yenye ladha. kwa uzito huu kwa majogoo, kuku hawa uuzwa kwa bei ya 20,000 - 25,000 wakiwa hai. bei ambayoni kwa mujibu wa bei ya soko kwa makadirio ya shilingi 8,000 kwa kilo kwa nyama nyeupe.

Mapungufu

Pamoja na ubora wa kuku hawa katika ufugaji wa kibiashara, kuku hawa pia wanachangamoto mbali mbali ikiwemo kutokuwa na uwezo wa kutamia. Pamoja na hii kuwa changamoto pia ni fursa kwani kwa yeye kutotamia kunamwongezea nafasi ya yeye kuendelea kutaga mara nyingi Zaidi bila kupumzika. Hivyo changamoto hii ni faida kwa mfugaji anaelenga kufuga kwa tija. Kwa vile mayai haya huwa yamerutubishwa na majogoo, nirahisi kwa mfugaji kuongeza idadi ya kuku kwa kupitia kutotolesha kwa mshine za kuangulia vifaranga au kumpa kuku mwingine ayatamie kwa niaba.


Neno la kufungia:


“ I think I touched a raw nerve when I said farming is NOT cool! I believe farming takes a lot of HARD work and dedication. Lets not lie to the youth that they'll become instant millionaires when they get into farming. It becomes "cool" once you master the trade......” caleb

Ufugaji unalipa ukiweza kuibudu biashara ya ufugaji,


Kwa ushauri Zaidi kuhusu shughuli za ufugaji, tuwasiliane kwa namba 0755815174. pia pata fursa kusoma ya Makala mbali na utaalamu kutoka kwenye mtandao wetu www.backyard.co.tz

Nimejaribu kuattach picha za baadhi ya kuku bora wanaofaakufugwa kienyeji na wakaleta tija kibiashara hapa chini. Neno langu si sharia, nakaribisha Michango

View attachment 385750
View attachment 385751
View attachment 385752
View attachment 385753
View attachment 385754
Makala yako ni nzuri, lakini kitaaluma na uandishi wa kitaaluma inaonekana kuegemea upande. Mimi naona kwa kuwa wewe tayari unafuga kuku chotala tayari ni mshindan wa kuku wa kienyeji hivyo huwezi kuwa neutral lazima utakuwa biased. Ningekuona umeandika kiasi juu ya uzuri wa kuku wa kienyeji, lakini umeandika changamoto tu, kuanzia kuwafuga, mayai kiasi kidogo, uatamiaji hafifu muda mrefu wa kuwafuga nk nk. Kuku wowote iwe wa kienyeji au wa kisasa utagaji wake unategemea lishe. Kuku wa kienyeji wa Tabora ni tofauti na wale wa Moshi. Hujatuambia inakuwaje ukichanganya mbegu hizi mbili ingawaje wapo wa Malawi na Zimbabwe hawa nao ukichanganya inakuwaje. Inakuwaje ukitumia mashine kutotolesha mayai, kwa sababu hata hao chotara ukiwafuga lazima utachanganya mbinu za kienyeji na za kisasa.
Nadhani, pamoja na andiko lako zuri unahitaji kwenda zaidi ya hapo ulipofikia.
Mimi nimewahi kuanza kufuga kuku mmoja wa kienyeji. Akataga mayai 11 na akatotoa vifaranga 11. Kwa bahati mzuri vifaranga wote wakakua kufikia kuanza kuataga. Nikawauza kwa bei ya shs 2500 kwa wakati huo. 2500x10= 25000. Nikanunua nguruwe. Baada ya miezi 6 nikampandisha na baada miezi minne nguruwe akazaa piglets 11 @ 10, 000 maana bei ilikwisha panda nikapata 110,000 nikanunua ngombe crossbreed na Mpwapwa na Fresian. Binafsi niona hayo ni maendeleo kuanzia na kuku mmoja wa kienyeji.
Mtandaoni hatudanganyani ila tunachosema ni kuwa ukiwa mtaji mdogo unaweza kufanya kitu. Development by definition means change. Change from one inferior stage to another a bit supperior stage. Tunataka kila mtu ajione anaweza hata yule aliyekuwa anafikiria everything is imposible aone angalao hili kwa kiasi hiki anaweza
 
Makala yako ni nzuri, lakini kitaaluma na uandishi wa kitaaluma inaonekana kuegemea upande. Mimi naona kwa kuwa wewe tayari unafuga kuku chotala tayari ni mshindan wa kuku wa kienyeji hivyo huwezi kuwa neutral lazima utakuwa biased. Ningekuona umeandika kiasi juu ya uzuri wa kuku wa kienyeji, lakini umeandika changamoto tu, kuanzia kuwafuga, mayai kiasi kidogo, uatamiaji hafifu muda mrefu wa kuwafuga nk nk. Kuku wowote iwe wa kienyeji au wa kisasa utagaji wake unategemea lishe. Kuku wa kienyeji wa Tabora ni tofauti na wale wa Moshi. Hujatuambia inakuwaje ukichanganya mbegu hizi mbili ingawaje wapo wa Malawi na Zimbabwe hawa nao ukichanganya inakuwaje. Inakuwaje ukitumia mashine kutotolesha mayai, kwa sababu hata hao chotara ukiwafuga lazima utachanganya mbinu za kienyeji na za kisasa.
Nadhani, pamoja na andiko lako zuri unahitaji kwenda zaidi ya hapo ulipofikia.
Mimi nimewahi kuanza kufuga kuku mmoja wa kienyeji. Akataga mayai 11 na akatotoa vifaranga 11. Kwa bahati mzuri vifaranga wote wakakua kufikia kuanza kuataga. Nikawauza kwa bei ya shs 2500 kwa wakati huo. 2500x10= 25000. Nikanunua nguruwe. Baada ya miezi 6 nikampandisha na baada miezi minne nguruwe akazaa piglets 11 @ 10, 000 maana bei ilikwisha panda nikapata 110,000 nikanunua ngombe crossbreed na Mpwapwa na Fresian. Binafsi niona hayo ni maendeleo kuanzia na kuku mmoja wa kienyeji.
Mtandaoni hatudanganyani ila tunachosema ni kuwa ukiwa mtaji mdogo unaweza kufanya kitu. Development by definition means change. Change from one inferior stage to another a bit supperior stage. Tunataka kila mtu ajione anaweza hata yule aliyekuwa anafikiria everything is imposible aone angalao hili kwa kiasi hiki anaweza
bantulile
Ahsante sana, kuna watu humu wanabeza watu wanaofanya vitu vidogo, hawajui kuwa hata vikubwa msingi wake ni kuanzia vidogo! Wewe ulinunua kuku mmoja ukafanya majaribio ukapata faida - SAFI SANA!
Mtu anakurupuka hajafanya jaribio kwa vitendo anakurupuka kuanza na kundi kubwa la kuku, wanakufa wote - anaingia mtandani kulalama eti kadanganywa!
 
Makala yako ni nzuri, lakini kitaaluma na uandishi wa kitaaluma inaonekana kuegemea upande. Mimi naona kwa kuwa wewe tayari unafuga kuku chotala tayari ni mshindan wa kuku wa kienyeji hivyo huwezi kuwa neutral lazima utakuwa biased. Ningekuona umeandika kiasi juu ya uzuri wa kuku wa kienyeji, lakini umeandika changamoto tu, kuanzia kuwafuga, mayai kiasi kidogo, uatamiaji hafifu muda mrefu wa kuwafuga nk nk. Kuku wowote iwe wa kienyeji au wa kisasa utagaji wake unategemea lishe. Kuku wa kienyeji wa Tabora ni tofauti na wale wa Moshi. Hujatuambia inakuwaje ukichanganya mbegu hizi mbili ingawaje wapo wa Malawi na Zimbabwe hawa nao ukichanganya inakuwaje. Inakuwaje ukitumia mashine kutotolesha mayai, kwa sababu hata hao chotara ukiwafuga lazima utachanganya mbinu za kienyeji na za kisasa.
Nadhani, pamoja na andiko lako zuri unahitaji kwenda zaidi ya hapo ulipofikia.
Mimi nimewahi kuanza kufuga kuku mmoja wa kienyeji. Akataga mayai 11 na akatotoa vifaranga 11. Kwa bahati mzuri vifaranga wote wakakua kufikia kuanza kuataga. Nikawauza kwa bei ya shs 2500 kwa wakati huo. 2500x10= 25000. Nikanunua nguruwe. Baada ya miezi 6 nikampandisha na baada miezi minne nguruwe akazaa piglets 11 @ 10, 000 maana bei ilikwisha panda nikapata 110,000 nikanunua ngombe crossbreed na Mpwapwa na Fresian. Binafsi niona hayo ni maendeleo kuanzia na kuku mmoja wa kienyeji.
Mtandaoni hatudanganyani ila tunachosema ni kuwa ukiwa mtaji mdogo unaweza kufanya kitu. Development by definition means change. Change from one inferior stage to another a bit supperior stage. Tunataka kila mtu ajione anaweza hata yule aliyekuwa anafikiria everything is imposible aone angalao hili kwa kiasi hiki anaweza

Nakubaliana na hoja yako mkuu, na nikupongeze kwa mafanikio. hakika hiki ndicho nachozungumzia pale naposisitiza ufugaji wa kibiashara. business model inaweza isiwe sawa kwa kila mfugaji ila ni vyema tukapeana mbinu kama hizi za namna ya kufanya ufugaji wa kibiashara. umetoa mwongozo mzuri na mbinu uliyotumia kwa hakika itawafumbua wengi Zaidi.
 
Ginner
Nimekuelewa Mkuu vizur sana
Ila napenda kukusahihisha kidogo kwenye utagaji mayai kwa kuku wa kienyeji
Kwa uzoefu wangu wa miaka mitano kwenye ufugaji wa kuku wa kienyeji, kuku mmoja jike kwa mwaka anaweza kutaga mayai 150.
Ninachokifanya mimi kuku akianza kutaga huwa nampunguzia mayai hadi idadi ninayoitaka ikamilike ndo nampatia mayai yote tayari kwa kuatamia.
Then akitotoa ninamwacha wiki moja akilea vifaranga baada ya hapo namtoa kwenye chumba cha kulelea vifaranga [namwacha huru] akitoka nje hukaa wiki moja kisha huanza kutaga tena.
Ina maana ukizungusha hivyo kwa mwaka kuku mmoja anaweza kukupa vifaranga 150~ 200
Sema Changamoto Iko Kwenye Soko

Nawasilisha...
nimefuga kuku wa kienyeji kwa muda mrefu, kuku akilalia na kulea kwa wiki hawezi kufika idadi ya mayai 100 kwa mwaka. labda useme vifaranga hivyo ni pamoja na mayai ya nyongeza toka kuku wemgine.
 
Vitu viwili nahisi ni muhimu kwenye huu ufugaji wa kuku wa kienyeji. Mbinu mbadala za ufugaji wa kuku na elimu kwa watumiaji kiubora ukilinganisha na kuku wengine (quality is better than quantity). Bado tuko nyuma kuelimishana.
 
Miezi 10 tu unalalamika khaaa ni mfanyabiashara gn kafanikiwa kwa kipindi kifupi.

Mfano muasisi wa Kali Linux ilimchukua miaka 10 mpk aka release tool hyo ,

Hakuna mjasiria Mali aliyetajirika kwa miezi 10

Hoja yako naipinga mkuu na ni invalid
 
nimefuga kuku wa kienyeji kwa muda mrefu, kuku akilalia na kulea kwa wiki hawezi kufika idadi ya mayai 100 kwa mwaka. labda useme vifaranga hivyo ni pamoja na mayai ya nyongeza toka kuku wemgine.
Samahani kuu naomba nitoe uzoefu wangu kwa hili la mayai.
Mm kuku wangu naofuga hua na stani wa kutaga mayai 15-17. Na kumchukua miezi miwili kutaga tena.haoa ipo hv namuwekea mayai analalia mpaka anatotoa.baada ya kutotoa tu,mm humnyang'anya vifaranga ck ya kwanza anayotoka na vifaranga ndani.hivo baada ya wiki mbili huanza tena kutaga.huu ndo mtindo natumia kwa kuku wng woote.
 
nimefuga kuku wa kienyeji kwa muda mrefu, kuku akilalia na kulea kwa wiki hawezi kufika idadi ya mayai 100 kwa mwaka. labda useme vifaranga hivyo ni pamoja na mayai ya nyongeza toka kuku wemgine.
Mwaka una wiki ngapi? 52
Kawaida ya kuku wa kienyeji ...
Anataga wiki 2
Anahatamia wiki 3
Analea wiki 1
Anapumzika wiki 1
Hizo ni jumla ya wiki 7
Chukua 52 gawia 7 = 7
Mizunguko 7 x vifaranga 12 = 84
JIBU LIKO WAZI, NA HAYA MAHESABU NIMEISHAYAFANYIA KAZI, CHANGAMOTO NI KWENYE KULEA VIFARANGA JAMANI.
 
Ndugu zanguni,
mimi pia nafuga hawa kuku wa kienyeji na ninao hawa kuku 142,wakati nawanunua nilikua namatarajio makubwa sana yaani niwalishe vizuri wakue nipate mayai lakini haikua hivyo badala yake wakawa wanataka kwa kusua sua na hapo tayari nimetumia pesa nyingi kuwatunza ikabidi niwauze tu kwani wamenitia hasara sana ,hivyo nimebakiwa na hao 142 ambao nao nimeamua niwaachie tu sasa wajitafutie coz nina eneo kubwa.Sasa hivi nimebahatikakupata kuku 42 wa mayai yaani wanataga mpaka najiuliza hivi nilikua wapi siku zote.Hivyo kibiashara fuga kuku wa kisasa ila kiafya fuga wa kienyeji
 
safi umenena vyema ila mie ninao matetea wakienyeji niliowanunua mkoani nianzishe mradi mkubwa na mwanzoni walitaga mayai 15 kwa msimu ila nilipofahamu njia yakuchanganya msosi wao walitaga non stop hadi nibadilishe ndo waweze kuatamia ila lazima uhakikishe hawaumwi na kuhusu majoo nilipataga mbegu ya jogoo chotara na niliwafuga kwa miez 9 wafikisha uzito wa kg 2.5 japo sikumaintain chakula....i think with a formular n well care its not wasteful

Mkuu unaweza nisaidia formula ya kuchanganya msosi wa kuku ili watage vizuri?
safi umenena vyema ila mie ninao matetea wakienyeji niliowanunua mkoani nianzishe mradi mkubwa na mwanzoni walitaga mayai 15 kwa msimu ila nilipofahamu njia yakuchanganya msosi wao walitaga non stop hadi nibadilishe ndo waweze kuatamia ila lazima uhakikishe hawaumwi na kuhusu majoo nilipataga mbegu ya jogoo chotara na niliwafuga kwa miez 9 wafikisha uzito wa kg 2.5 japo sikumaintain chakula....i think with a formular n well care its not wasteful
 
Jamani nahitaji mayai ya kanga, please
Mayai ya kanga mimi ndiye mzalishaji mkubwa na nakaa Dodoma. Kwa uzoefu wangu kanga hutaga kuanzia mwezi wa kumi mpaka may maka unaofuata. Kwa sasa kanga wamenipungua sana ninao kama mia mbili na ushee. Katika msimu wa utagaji huwa sikosi trei tatu kwa siku na yai moja nauza mia tano. Ukipenda vifaranga pia utapata kwani ninayo mashine ndogo ya kutotoresha yenye uwezo wa mayai 96, na kifaranga kimoja nauza sh 1500 cha siku moja. Kikifika kipindi hicho tuwasiliane kwa simu na 0786775663 /0757284076 /0715557342 . Pia ninafuga kuku wa kienyeji ( crosbreed) kwa sasa ninao zaidi ya mia tatu na pia nafuga bata mzinga ila soko linanishawishi kuacha kuwafuga.
 
aiseee... umeongea sana nimependa... sio mfugaji... ila tatizo hapa mi nililo liona halipo kwa kuku hawa wa kienyeji... tatizo lipo kwako mfugaji, ni kusema kua kuku hawa hawana tija kibiashara nimekataa kidogo kwa sababu hizi.

1. ubunifu kwako ndio imekua tatizo... kama kuku wa kienyeji hawawezi kutaga mayai mengi kwa mwaka maana yake unatakiwa uangalie njia gani ufanye ili waweze kutaga mayai mengi... kuanzia lishe mpaka ufugaji... kwanini huyu kuku akitaga kama ulivyosema anataga siku 10 kumaliza... akimaliza ukiyachukua... ili akae mda kidogo aje kutaga tena itakuaje..? au ata susa kutaga tena.?
na kama utunzaji wake hayatakiwi kuwekwa sehemu yenye joto, firdge zimejengwa za nini, supermarkets gani hizo zisizo na A/C kufanya mazingira yawe ya baridi?
2. nyama... usishindanishe nyama ya kuku na samaki... kwani kila mteja ana ladha anayopenda... wateja wa nyama hugawana, unataka kuniambia hawa kuku wakilishwa vizuri hawa nawiri na kuongezeka kilo, kama ni kutaka kuku wengi... na kimsingi kuku hawa ni lazima warutubishwe na jogoo... tetea wakisha taga na na mayai yakatotoleshwe na mashine ili tetea watage tena haiwezekani?

kila biashara ina tija endapo utakua mbunifu... na hakuna biashara isiyo na changamoto... na kuku hawa ndio kuku wanaotoa nyama na mayai yenye virutubisho vingi ukilinganisha na hao kuku wengine... sio busara kusema hii biashara sio ya kufanya... cha msingi ni kuangalia na kutafakari njia gani zitumike kurahisisha na kuipa tija biashara ya kuku wa kienyeji.
 
safi umenena vyema ila mie ninao matetea wakienyeji niliowanunua mkoani nianzishe mradi mkubwa na mwanzoni walitaga mayai 15 kwa msimu ila nilipofahamu njia yakuchanganya msosi wao walitaga non stop hadi nibadilishe ndo waweze kuatamia ila lazima uhakikishe hawaumwi na kuhusu majoo nilipataga mbegu ya jogoo chotara na niliwafuga kwa miez 9 wafikisha uzito wa kg 2.5 japo sikumaintain chakula....i think with a formular n well care its not wasteful
ni kweli kabisa... ni ubunifu na kufata taratibu za ufugaji... hawa kuku hawawezi kua na hasara.
 
98 Reactions
Reply
Back
Top Bottom