Mimi sikuachwa na ndege ugenini, bali hapahapa Bongo!
ilikua mwaka 2017 nimepata safari kwenda Germany! tiketi yangu ilikua inaonesha ndege inaondoka saa kumi jioni! (QATAR AIRWAYS). Kutokana na ushamba wangu enzi hizo sikujua kuwa natakiwa kuangalia mara kwa mara my flight schedule ili kama kuna changes za muda niweze kuona.
Kumbe bwana ndege ilibadilisha muda few days kabla ya safari, badala ya saa 10 jioni, ikabadilishwa saa saba mchana, me sikujua hilo.
Basi siku hio nmejipanga safi kwa safari, saa saba kamili niko airport, nafika reception ya qatar nakuta hamna mtu bas nkajitutumua nikadhani me ndio nimewahi wa kwanza kufika



.
nikafika kwa ajili ya kufanya check -in! Wakaniuliza unaelekea wapi, nikasema angalieni ticket naelekea Munich - Germany! Shabaaaash wakasema mbona ndege yako ndio inaondoka saa hizi gate wamefunga dakika chache zilizopita! Damn it nliishiwa nguvu! ntaambia nini watu na nlishaaga


Basi wakasema huo uzembe wangu nilipe fine usd 50 wafanye booking ticket ya kesho. Nikasema huo ni izembe wenu kama mli change muda mlipaswa kutoa taarifa kwa wateja wenu, kama mnachukua email na namba zetu na hamtupatii taarifa za changes je nini maana ya customer service?. Tukabishana mpaka akaja boss wao bas wakakubali makosa ni yetu mimi nna kosa kutoangalia my flight na wao wana makosa kutotoa taarifa.
bas wakasema watanipa free accomodation wana schedule ndege ya kesho! basi tukaondoka wakanipeleka serena hotel.. sikuamini macho yangu kwa mara ya kwanza nililala serena hotel sehemu ambayo sikuwahi kuwaza hata katika ndoto.
basi kesho yake wakaja kunichukua saa saba mchana na nikaondoka saa 10 tukapaa mpaka Doha then nika change flight to Munich - Germany. Nikafika saa 12 alfajiri.