Kuachwa na ndege iwe ugenini au nyumbani huwa ni kielelezo Cha uzembe na poor planning ability ya mtu
Hujawahi kuachwa na ndege ndugu, na labda waliotangulia kuelezea hawajatoa mazingira tofauti tofauti. Sikia hii...
Nilikuwa natoka Ottawa via Montreal to Zurich then Bongo. Hali ya hewa ilikuwa ni winter kali Feb 2015, na kusababisha ndege kuchelewa kuondoka Macdonald-Cartier Intl airport. Tulikaa taxiing lane kama dk 40 hivi then kuruka na safari ya kama 1.30hrs au 2hrs. Ile Kufika Montreal-Dorval airport (au Trudeau kwa sasa) pipa la kuunganisha to Zurich ndio linakula mawingu, kimbembe kikaanzia hapo mzee.
Mfukoni nina $5 tu ya Canada, simu hazikamati mtandao, wenge likanijaa mwanaume. Sema penye matatizo akili nayo huwa inachaji fasta, ikabidi niwafate kwenye meza ya ndege husika. Nikapambana nao kama lisaa hivi mpaka kilipoeleweka na wakanipa na coupon ya $10 kwa ajili ya msosi manake route ikabadilika sasa kupitia Heathrow kisha Addis mpaka Bongoland.
Kwahiyo sio kila kuachwa kunatokana na uzembe na kutokujipanga mapema kisafari



