Kwa sasa hivi kama sio Mh Zitto atakuwa ni nani atakayewasemea wasiotaka mambo yanayofanywa bila taratibu zilizowekwa yasifanywe? Kutoweka kwa Zitto kwa njama zozote maana yake ni moja tu; kuwanyamazisha wanaotafuta ukweli na haki katika taifa letu
Sauti iliyobaki ni ya Mh Zitto, na kama jambo lolote baya likitokea kwa Zitto sasa hivi itaeleweka bila ya shaka yoyote, kama ilivyokuwa kwa Mh Lissu ni nani atakuwa ni mhusika kwa kutoweka huko.
Watu waliopofushwa na kuleweshwa na madaraka wanaweza wasione madhara yoyote kwao kwa kufanya hivyo. Lakini, ni nani ajuae?