Ushauri wenu: Nilimuahidi, nifanyaje?

Ushauri wenu: Nilimuahidi, nifanyaje?

Miaka mi4 umemtumia weeew mpaka uliposema fyokonyoko naona mwingine,huoni aibu? Umechezea hisia za mwenzio na mwili wake pia for 4 years then unakuja kulalamika anadai ulichomuahidi. Mlipe asepe faster we chalii niadje buana
 
We timiza, kama ulikuwa na nia kwanini hukutimiza kabla hajaolewa? Umesubiri kaolewa ili upate kisingizio!!!
 
Achana nae broo...hiyo ni hatari licha ya kuwa,ulimuahid...kumfungulia saloon kwanza kutaendeleza enzi lenu istoshe ameshaolewa
Ataachana naye vipi wakati anamfuata mpaka ofisini? Bro umesema una uwezo, lipa deni block mawasiliano. Akikufuata tena hapo anataka mengine.
 
Kisheria hakufanyi chochote maana mkataba wenu hauna mashahidi.Ni sawa na unapomuahidi mkeo kuwa mwakani utamnunulia gari usipofanikiwa hawezi kukufanya lolote.Ama ukaenda kanisani pesa unayo ila ukagoma kutoa sadaka hakuna kosa kwa kuwa hakuna mkataba na kama mkataba haupo basi hakuna sheria na kama sheria haipo basi uko huru. Ila nakushauri umwite sehemu mkae faragha muongee kwa kirefu mpe kilichopo then kingine mpigane tarehe ila unaonekana bado unamtafuna tu na hana ujanja amaa kweli mapenzi noma.
 
Mkuu kumbuku aliahidi lakini! Na ahadi ni deni!

Suluhisho ni kumfungulia hiyo saluni mkuu. Labda tu kama kuna vipengele mliwekeana katika makubaliano yenu.

Mfano, kama angeolewa basi usingetekeleza ahadi yako. Ila kama hiyo ahadi haikuwa na masharti yoyote basi wewe fanya kama ulivyoahidi. Ni wajibu wako kwakuwa uliahidi.
Hivi wewe kama mke wako aliahidiwa huko nyuma na jamaa utakubali huyo jamaa atimize ahadi aliyo muahidi mke wako.
Mfano tu.

Sent from my SM-J100H using JamiiForums mobile app
 
Habari zenu wana wa MMU!!! Kwa heshima kubwa, naombeni msaada wa mawazo.

Mimi ni mume wa mtu. Ila kabla sijaoa nilikuwa na mpenzi ambaye nilidumu nae kwa takribani miaka 4, lakini bahati haikuwa yetu, hatukuweza kuoana.

Nilipomueleza kuwa naoa mwanamke mwingine, aliumia sana na alilia sana. Katika kupooza, nilimpa ahadi kuwa sitamuacha hivi hivi. Nikamwambia achague, nimfanyie nini? Yeye akachagua, nimfungulie saluni ya kike, na baada ya kufanya quotation tukabaini kuwa shilingi milioni 2 zingetosha. Mimi kiasi hicho cha pesa, ninakimudu.

UGUMU UNAANZIA HAPA.

Huyu dada (mpenzi wa zamani), alipata mwanaume akaolewa kwa ndoa kabisa. Baada ya ndoa yake, amekuwa akinipigia mara kwa mara, na mara zote anaulizia ahadi yangu kwake (kumfungulia saluni).

Kila nikimueleza kuwa, wewe sasa ni mke wa mtu nitakufunguliaje saluni? Hanielewi. Na amekuwa akinifuata, hadi kazini kwangu.

NIFANYAJE? Ni kweli niliahidi, na nilikuwa na nia hiyo. Ila, kwa sasa ni mke wa mtu. Ni hatari kwa mustakabali wa maisha ya ndoa yake na kwangu pia

Kama ni hivyo timiza ahadi! Mtie noti yake atajua mwenyewe afungue saluni Au akanunue maandazi, baada ya hapo mwambie asikuzoee utamuitia mwizi akija ofisini Kwako.
 
Mfungulie saloon acha visingizio, we si uliahidi ukiwa na mke sasa mtimizie nae akiwa na mme.....
Wakati unaahidi huku ukiwa na ndoa we hukuangalia mustakabali wa ndoa yako?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom