Ushauri wenu ni muhimu sana kwangu

Ushauri wenu ni muhimu sana kwangu

Private Pasua kichwa sanaaa,niliacha kazi private mshahara 1m nikaenda serikalin mshahara laki 5 napata baada ya miez sita mwajir kapata mapigo mengii sahv mshahara unalipwa kwa mbinde kwa waliobak na umepunguzwa sababu hali sio nzuri na kupata tarehe 55 au 60 kawaida

Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
 
Baki kwenye uhasibu. Somea CPA. Timiza ndoto zako.
 
Ushauru wangu

Fanya kazi hapo private lkn fungua biashara yako binafsi haraka sana.
 
Uhasibu unakupa fursa yakukutana na watu wenye pesa na waliofanikiwa, ila uwalimu unakukutanisha na watu wenye msongo wa mawazo na waliokata tamaa.Sasa ni wewe uamue,uwe karibu na anayenukia pafyumu au uwe karibu na anayenukia jasho.
 
Ushauru wangu

Fanya kazi hapo private lkn fungua biashara yako binafsi haraka sana.
Haraka sana eti???? Miezi sita 1.5 mil kama una familia sio hela ya kudhani itabadilisha maisha yako mzee yani na vile private wanakuwa busy na kazii utajikutaa unamaliza miezi sita huna hata mia na Omba sana wakuongeze mkatabaa..
 
Piga chini hiyo kazi ya binafsi ,nenda serikalin karipoti Fanya kazi mwaka mmoja ingia benki chukua mkopo wekeza kwenye unachoona kitakufaaa .kazi za private zina stress sanaaa inaweza isha kesho na pia unatumika sanaa.

serikalin raha yake kama una akili mda upo wa kufanya mambo yako tena kazi yenyewe ualimu ni rahisi sanaa unashika somo lako unafundisha miaka yote hilo hilo inafika mda unakuwa kama unaimba pambiao tu maana hutumii nguvu kufundisha ,kutunga mitihan na kujua vijana wako ufanye vipi wafaulu

Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
Best comment ever, Kuna wengine wanakushauri uendelee hapo wakati wao Ni watumishi wa serikali na hawataki kuachia nafasi, mkuu nenda serikalini hizo private company unafanya mwez mmoja unatukuzwa au kampun inafilisika naww ndo serikalin huwei Tena ingia kwa sabab ulishachaguliwa uka kataa nafasi.
 
Haraka sana eti???? Miezi sita 1.5 mil kama una familia sio hela ya kudhani itabadilisha maisha yako mzee yani na vile private wanakuwa busy na kazii utajikutaa unamaliza miezi sita huna hata mia na Omba sana wakuongeze mkatabaa..
Lakini mtoa mada amesema kuna option ya kuongeza mkataba
 
Ukiona kitu hakina changamoto ujue hakilipi... Ualimu ni kazi ya kimaskini na ya kinyonge nenda kawe mhasibu experience tu ya mwaka mmoja ya uhasibu ni mtaji kuliko kiinua mgongo cha mwalimu. Kama ukienda kwenye ualimu kubali utaiona hela ya maana siku ya kupokea kiinua mgongo.
Maisha yana mengi anaweza pia kufa kabla ya kupokea kiinua mgongo.
 
Nimepata kazi ya "UALIMU" katika hizi ajira ambazo zimetoka juzi. Lakini wakati naomba hii ajira ya Ualimu sikuwa na kazi.

Ila katika kipindi hiki cha kusubiria ajira ya Ualimu nimepata kazi nyingine ya UHASIBU katika moja ya taasisi kubwa sana hapa Tz ya mtu binafsi ambayo pia ni fani yangu na mshahara wake ni 1.5mil.

Nimepewa mkataba wa miezi 6 kwa kuanzia then baadae nitapewa mwingine na mshahara utaongezeka baada ya Probation kuisha.

Je, niache hii kazi niende kufundisha au niendelee na kazi yangu hii ninayofaifanya?

Nisaidie ushauri wenu?
Mkuu fanya hivi nenda kwenye ualimu serikalini kaa mwaka mmoja ukisha thibitishwa kazini ka wilikilishe cheti chako cha uhasibu na uombe kubadilishwa muundo utafanyiwa re categorization kuwa mhasibu Kuna uhaba wa wahasibu kwny halmshauri nyingi achana na iyo kazi ya mtu binafsi job security ni 0
 
Lakini mtoa mada amesema kuna option ya kuongeza mkataba
Yaan ijulikane kwamba kazi yangu sio ya leo wala kesho ni miaka na miaka nikiperfom vzr nitaedelea nayo mpaka hata nistaaf. Na walivyonichukua moja ya swali wameniambia hatutaki ambae tunamuajiei leo kesho anaondoka. Tunataka mtu wa kukaa mda mrefu. So ni mm tu.
 
Haraka sana eti???? Miezi sita 1.5 mil kama una familia sio hela ya kudhani itabadilisha maisha yako mzee yani na vile private wanakuwa busy na kazii utajikutaa unamaliza miezi sita huna hata mia na Omba sana wakuongeze mkatabaa..
Kaka hiyo 1.5 nimeanza nayo tu. Huko mbele mambo mazuri sana. Sio kwamba ni fixed salary. Noo baada ya probation nitapewa contract nyingine na salary nyingine
 
Kama ni jinsia ke nenda ualimu, kama ni jinsia me baki uhasibu.

By the way kama ushakusanya mtaji kiasi ambao unaweza kuanzisha biashara kwa sasa nenda ualimu huku unasimamia biz au mradi wako.
 
Kama ni jinsia ke nenda ualimu, kama ni jinsia me baki uhasibu.

By the way kama ushakusanya mtaji kiasi ambao unaweza kuanzisha biashara kwa sasa nenda ualimu huku unasimamia biz au mradi wako.
Mimi ni Me. Nashukuru kwa ushauri wako
 
Ingekuwa inawezekana mm kureplace nafasi yako ya ualimu bc ningekushauri uendelee na hiyo kazi ya uhasibu, nadhani umenielewa nini namanisha. 1.5m ni hela kubwa mkuu na nina uhakika kama umesota kitaa bc matumizi yako kwa mwez hayawez kuzidi 500k, kama ndiyo bc 1M weka bank itulie, mkataba ukikata kama hawatakuongezea bc 6M uliyoweka bank miezi 6 itakusaidia kibiashara na mambo mengne!
Kaka mm nipo single. Matumizi yangu hata hiyo 500k haiishi, sinywi pombe wala sina madem. Ila nendelea kupata shauri mbalimbali then before 14 days kuisha nitakuwa nimepata jawabu.
 
Back
Top Bottom