Ushauri wangu kwa Zuberi Zitto Kabwe

Siku zote mwanasiasa na hasa mbunge wa chama cha Upinzani unatakiwa kuwa kinyume cha maamuzi ya sera za chama tawala,

Nakushauri sana mkuu wangu achana na siasa za CCM inapofikia maswala ya kamati yako ya bunge. Kama mbunge wa Upinznai unachotakiwa ni kutafuta makosa ktk sera zao na kuweka wazi ubadhilifu unaofanyika laa sivyo hakuna sababu ya kuwa na upinzani maana sote tunakubaliana na sera za Chama tawala. Kazi yako ni kupinga sera hizo na sio kujaribu kurekebisha utekelezaji wa miradi ndani ya sera mbovu.. Siasa haijengwi hivyo mkuu wangu.!
M

Mkandara,

Upinzani wa kupinga kila kitu umepitwa na wakati.

Halafu kazi ya kamati sio kukosoa sera za Chama. Hii kamati ya POAC wanachofanya wao ni kama Auditing zaidi kuingia deep na kuainisha makosa ya kiutendaji na kushauri sasa unaposema afanye kazi za POAC kama mwanasiasa wa upinzani hapo sikubaliani na wewe labda useme wapinzani wakatae kabisa hata kuingia kwenye hizo kamati.

Kipindi cha Impeachment ya rais Clinton kule marekani walijitokeza hata wabunge wa Republicans wakaokoa jahazi wakati ilikuwa ni fursa nzuri ya kumtoa Clinton wao wachukue nchi. Siasa haziendi hivyo mazee.
 
Ushauri mdogo waraka wa kuusoma mpaka tunasinzia, jee, ungekuwa ushauri mkubwa ingekuwaje?
ni kawaida yako iyo sio kusoma sio kuandika..si unakumbuka siku ile ya mdahalo ulivokuwa unacopy na kupaste hata ufanyi editing bana...kumbe ni weakness yako kusoma eeeh...wapi Matola?
 
Last edited by a moderator:
Mimi nikiwa mmoja wa watu ambao tumeweka matumaini makubwa kwa chama cha Chadema kuleta mageuzi nchini nina ushauri mdogo sana kwa Zitto kuhusu SIASA zake na misimamo yake ambayo ndiyo sababu na chanzo cha yeye kuwa bangusilo ktk kila tukio la Upinzani..

Mheshimiwa Zitto amekuwa akisimama sana peke yake (independent) kwa fikra kwamba anaweza kuleta mabadiliko kupitia mwamvuli wa CCM. Hutumia sana maneno ya kwamba yuko huru na anafanya kile anbachokiamini yeye kuwa ndio haki na sahihi. Kwa fikra hizo amekuwa mstari wa mbele ktk tunzi za uwekezaji nchini wakati yeye kama mwanasiasa wa Upinzani hakutakiwa kabisa kugusa jambo hilo pasipo kuwepo makubaliano na ushirikiano wa vyama (Bipartisan) ktk kufuata sera (policies) zitakazo tumika..

Siku zote mwanasiasa na hasa mbunge wa chama cha Upinzani unatakiwa kuwa kinyume cha maamuzi ya sera za chama tawala, napengine kutumia nafasi hiyo kuweka shinikizo kwa chama tawala wakubali kufuata sera za Upinzani lakini wewe binafsi huwezi kutumikiwa na sera zile zile ambazo ndizo sababu ilokufanya wewe usimame upande wa pili, fikra hizi ni kuonyesha immaturity ktk ulingo wa siasa!

Nakushauri sana mkuu wangu achana na siasa za CCM inapofikia maswala ya kamati yako ya bunge. Kama mbunge wa Upinznai unachotakiwa ni kutafuta makosa ktk sera zao na kuweka wazi ubadhilifu unaofanyika laa sivyo hakuna sababu ya kuwa na upinzani maana sote tunakubaliana na sera za Chama tawala. Kazi yako ni kupinga sera hizo na sio kujaribu kurekebisha utekelezaji wa miradi ndani ya sera mbovu.. Siasa haijengwi hivyo mkuu wangu.

Huwezi kurekebisha utekelezaji wa sera za CCM kwa kutumia kiti cha upinzani -HAIWEZEKANI isipokuwa utatumiwa muda wote na kuwa the weakest link kwao kumaliza upinzani, maana kinachowezekana kutekelezeka kinatokana na sera zenyewe ambazo wewe kama Mpinzani hukubaliani nazo.

Brother, kitumikie chama chako, simama nyuma ya sera za chama chako na pingana na sera za chama tawala kama mpinzani na sii kutekeleza sera za chama Tawala kwa fikra zile zile zilizotufikisha hapa tulipo. Mtazame mwenzako January Makamba, he is smart kisiasa na siku zote husimama nyuma ya chama chake hata kama hakubaliani na mtu ndani ya chama. Mtazame Lowassa, he is smarter hata kama hakubaliwi na watu wengi nje ya CCM lakini ameendelea kujijenga ndani ya chama kuliko nje kwa sababu huko ndiko alikozaliwa - Hutaki yote haya Unaacha!

Mkadara,

Ni matumaini yangu kuwa ujumbe huu utamfikia Mh Zito akiwa na afya njema na akili za kutambua na kufikiri zikiwa timamu kabisa na hataacha kufuata hata chembe ya waraka huu.

Most Welcome Hon Zito.
 
Asante sana mkuu, tena asante sana, mungu akupe na akuzidishie busara zaidi za kuongea mambo yenye maana na ya kujenga kwa kweli nimesoma michango mingi lazima nikiri wewe umeni konga moyo wangu! Nami sina cha kuongeza hapo bali chama kiangalie na kitafakari ushauri wako.Mungu akubari.
 
Basi usimuongeze
ni kawaida yako iyo sio kusoma sio kuandika..si unakumbuka siku ile ya mdahalo ulivokuwa unacopy na kupaste hata ufanyi editing bana...kumbe ni weakness yako kusoma eeeh...wapi Matola?
 
Last edited by a moderator:
Ushauri wa nyongeza kwa Zitto leo kwenye press conference yake atangaze kujiuzulu nyadifa za Uenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mashirika ya Umma (POAC). Mashirika ya Umma yameendelea kutafunwa, kuyumbishwa na mengine kuelekea kufilisika yeye akipita huko kila mwaka na kamati yake hii kwa miaka yote saba!
Nafasi ya unaibu KUB pia haimfai kwa sasa kwa kuwa hakufanikiwa hata kuwashawishi wenzake wa CHADEMA kuachana na POSHO za vikao vya Bunge. Zitto aliongoza katika kutafuta sahihi kumwondoa Pinda madarakani sioni yeye anapata kigugumizi gani kutangaza kuachia nafasi hizi huku yeye akiwa ni mmoja wa watuhumiwa!
 
Nilikuwa namdharau sana James Mbatia lakini kwa sasa ndio mwanasiasa ninayemuheshimu kuliko mwingine yeyote. Huyu hakufuga maradhi haya ya Zitto Kabwe kupitia huyu Kafurila na sasa NCCR Mageuzi mambo tambalale, nawashangaa Chadema kila siku wanacheka na sisimizi.

Sikutalajia Kafurila na kiburi chake chote kama angetokwa na machozi baada ya NCCR kumfuta Uanachama, the same way to Zitto Kabwe huyu siku ya kurushiwa virago hata uharo utamtoka, hivi nathubutu kuviita viburi vya Kigoma. ( Sory kama nimemuinsult mwana Kigoma aliye safi) but i have to say.
Bado sijamsahau Amaan Walid Kaborou.
 
Nilikuwa namdharau sana James Mbatia lakini kwa sasa ndio mwanasiasa ninayemuheshimu kuliko mwingine yeyote. Huyu hakufuga maradhi haya ya Zitto Kabwe kupitia huyu Kafurila na sasa NCCR Mageuzi mambo tambalale, nawashangaa Chadema kila siku wanacheka na sisimizi.

Sikutalajia Kafurila na kiburi chake chote kama angetokwa na machozi baada ya NCCR kumfuta Uanachama, the same way to Zitto Kabwe huyu siku ya kurushiwa virago hata uharo utamtoka, hivi nathubutu kuviita viburi vya Kigoma. ( Sory kama nimemuinsult mwana Kigoma aliye safi) but i have to say.
Bado sijamsahau Amaan Walid Kaborou.
Matola,
Jamaa wa KIGOMA ni wabishi tu. Hawana wanaloweza kusimamia likafika mwisho. Wana misimamo mipya kila asubuhi, Jumatatu hadi Jumapili! Unamkumbuka yule aliyekuwa Katibu Mkuu wa klabu ya Simba, Mwina Kaduguda?
 
Well spoken; mwenye macho haambiwi tazama na wala mwenye masikio haambiwi sikiliza! ZZK kuchangia hoja bungeni na kuongea na vyombo vya habari usikUfanye hobby!! it gonna nip your nascent political career in the bud!!
ZZK unajichanganya sana, watu hawajasahau ulivyojikanganya kuhusu mitambo ya dowans! leo unashupaa kuwakingia kifua kina Mhando si uache na wengine waseme au uombe kikao cha CDM party caucus mkalijadili swala kwanza mpate msimamo wa kichama ndio ukalonge!? stop shooting like a loose cannon! identify your target, aim, take a deep breath then shoot. lots of people wanajaribu sana kukutofautisha na Shibuda wanashindwa! wakikulinganisha na madiwani wa CDM waliofukuzwa Arusha wanakwama! wakijiuliza ZZK wa sakata la Buzwagi yuko wapi? hawapati jibu! ZZK you have become a blank shadow of yourself!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!; Give us a break ZZK! your blurred vision is confusing the lot of CDM faithfuls; you are doing your party a huge diservice.
 
Mpaka sasa hakuna Mwanasiasa aliyevunja rekodi ya Zitto kabwe, huyu ndiye Mwanasiasa pekee hapa duniani aliyetanga kugombea Ubunge kwenye majimbo matano mwaka 2010, lakini cha kushangaza alivyorudi kugombea kwenye jimbo lake la Kigoma kaskazini alishindi kwa ushindi pungufu kuliko ule alioupata mwaka 2005. na bado akabaki na kauli mbiu yake eti ushindi wa Heshima!!!.....
 
Ndugu yangu Mkandara,

Umesema kuwa Nyerere alipata watu muhimu ndani ya TAA na TANU wakamwamini na kumuuza kwa wenzao, tena kwa gharama kubwa....Je, Zitto anao watu wa namna hiyo ndani ya chama? Na kama hana, anajaribu kuwavuta watu ili wawe upande wake au anawatimulia mbali??

Pamoja na uzuri wa Zitto, makosa ya kiufundi anayoyafanya, ama kwa kujua au kutojua, lazima yatamzuia kufikia malengo yake.

Tatizo kubwa la sisi wanadamu (including Zitto), ni kuhangaika kutafuta wabaya wetu wanaotukwamisha badala ya kujifanyia tathmini sisi wenyewe ili kuona ni kwa kiasi gani tumechangia kujikwamisha!

aamini shida ya ndugu yetu huyu ni kudhani kwamba yeye pekee 'atosha' kwamba yeye ni RAMBO wa siasa, anaweza kushinda akijitegemea kama Rambo anavoshinda jeshi zima yeye pekee kwenye sinema za kufikirika. Kwenye siasa kunahitajika oganaizesheni ya hali ya juu na mikakati mingi ambayo huitaji timu inayocheza pamoja, hata uwe ni mwanasiasa mahiri kupitiliza (kitu ambacho naamini Zitto sio) huwezi shinda uongozi ukiwa kivyakovyako.
 
kaonjeshwa mahela machafu ya akina jk na rostam and he is now financially ridiculous rich,stubborn to even those who helped him to spot light!
 
Huyoy hashauriki ana msimamo mkali
ha ha ha, No comment. Ukiilamba asali hutaiasha eenh. ngoja nisikilize wimbo mmoja wa taarabu, binti mmoja wa kizanzibar anaimba kwa busara kweli kweli.
 
Bob Mkandara,

Huwa unanigusa sana na maandiko yako. Nilwahi kusema Zitto hayupo juu ya chama. Akishaelewa hilo basi atajirekebisha.

Nahisi (sina uhakika) Zitto hana washauri wazuri. Ambitions zake za kua rais zilihitaji calculated move sio hii ya kubwabaja tu.

Angali kijana angesubiria naamini zamu yake ingefika.

Ushauri wako ni mzuri, na ndivyo tufanyavyo humu. Unapata ushauri wa bure. kazi inabakia kwako.
 
Well spoken; mwenye macho haambiwi tazama na wala mwenye masikio haambiwi sikiliza! ZZK kuchangia hoja bungeni na kuongea na vyombo vya habari usikifanye hobby; it gonna nip your nascent political career in the bud!!
ZZK unajichanganya sana, watu hawajasahau ulivyojikanganya kuhusu mitambo ya dowans! leo unashupaa kuwakingia kifua kina mhando si uache na wengine waseme au uombe kikao cha CDM party caucus mkalijadili kwanza mpate msimamo wa kichama ndio ukalonge; stop shooting like a loose cannon! identify your target, take aim, take a deep breath then shoot. lots of people wanajaribu sana kukutofautisha na Shibuda wanashindwa! wakikulinganisha na madiwani wa CDM waliofukuzwa Arusha wanakwama! wakijiuliza ZZK wa sakata la Buzwagi yuko wapi? hawapati jibu! ZZK you have become a blank shadow of yourself!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!; Give us a break ZZK! your blurred vision is confusing the lot of CDM faithfuls; you are doing your party a huge diservice.
His target is the presidency so enemy number one automatically becomes Dr Slaa.
 
  • Thanks
Reactions: Awo
MKANDARA NAKUBALIANA NAWE, ILA SIKUPENDEZWA NA ATTACK ZA JOSEPH SELASINI MAANA KTK HOJA HII MH. SELASINI HAKUWA MKWELI NAFSIN MWAKE NA ALILENGA KUJIPATIA POPULARITY KIBUNGE TOKA PANDE ZOTE....NAOMBA NIKUBALIANENA LISSU, MNYIKA, NYERERE NA HATA COMRADE LUGORA STYLES. ZITTO AMEANDIKA KITU HAPA HEBU SOMENI. ANAUONA UKWELI WA HOJA YAKO ILA BADO ANASUMBULIWA NA TYPE ZA KINA SELASINI HUKO CDM KWAO ILA NASISITIZA SANA AUZINGATIE USHAURI WAKO.
MAELEZO BINAFSI YA MHE. ZITTO ZUBERI KABWE DHIDI YA TUHUMA ZA RUSHWA HUSUSAN KUELEKEA KATIKA KUPITISHA BAJETI YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI
Ndugu Waandishi,
Nalazimika kukutana nanyi kutoa maelezo juu ya tuhuma zenye shinikizo la kisiasa zinazoelekezwa kwangu binafsi kwamba hata mimi nimeshiriki katika vitendo vya rushwa, kwa nafasi yangu kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma. Taarifa hizo, kama kawaida ya uzushi mwingine wowote zimesambazwa kimkakati na kwa kasi kubwa kiasi cha kuukanganya umma.
Nafahamu nabeba dhamana kubwa ya uongozi, taswira yangu ya uongozi daima imeakisi njozi na matumaini ya wananchi wa Kigoma Kaskazini, wananchi wanyonge na vijana kote nchini bila kujali itikadi zao za kisiasa, jinsia zao, makabila yao na rika zao. Hivyo, nawajibika kupitia kwenu kuwatoa hofu juu ya hisia potofu zinazopandikizwa kwao na wale wasiopenda kuona baadhi yetu tukiwaunganisha na kuwasemea watanzania wasio na sauti, dhidi ya vitendo vya hujuma na vyenye dhamira ovu kwa taifa.
Mkakati huo wa kuniunganisha na baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wanaotuhumiwa kwa kupokea Rushwa unatekelezwa kwa njia zifuatazo:

  1. Kumekuwa na kauli za watendaji wa serikali ambao wamekuwa wakizieneza na hususan kutoa taswira kwamba baadhi ya kauli zangu zinatokana na ushawishi wa rushwa;
  2. Kuna taarifa ambazo zimeandikwa tena katika kurasa za mbele za baadhi ya vyombo vya habari zikidai ''Zitto kitanzini'' ama ''Zitto sawa na popo nundu'' zikiashiria kwamba na mimi ni mla rushwa; na
  3. Waandishi wa habari na jamii kwa ujumla wamefikia kuaminishwa habari hizi kiasi cha wengine kuuliza kwa nini Mhe. Zitto Kabwe hakutajwa katika orodha iliyotolewa na Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani.
Ndugu Waandishi,
Naomba kutoa ufafanuzi wa hicho kinachoelezwa kwamba nina ushiriki katika masuala ya rushwa hususan kwenye masuala yanayohusu sekta ya Nishati na Madini:-

  1. Mara baada ya bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Usambazaji wa Umeme Tanzania (TANESCO) chini ya Uenyekiti wake Meja Jenerali Mstaafu Robert Mboma kutangaza kwamba imemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Nd. William Mhando ili kupisha uchunguzi wa baadhi ya vitendo/mwenendo wake, Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) ambayo mimi ni Mwenyekiti wake ilimuandikia Mhe. Spika kumuomba aridhie ili Kamati iweze kuwaita Bodi ya TANESCO, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali (CAG) na pia Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kujiridhisha na tuhuma zote zinazotajwa zinafanyiwa uchunguzi wa kina na hatua kuchukuliwa;
  2. Kamati ya POAC ninayoiongoza ilimuomba Mhe. Spika kuwaita wahusika tajwa kwa kuwa zilikuwapo tetesi kuwa kusimamishwa kazi kwa Mkurugenzi huyo siku chache kabla ya Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kulikuwa na lengo la kufunika 'madudu' makubwa zaidi kwa kulichagiza Bunge na tukio hilo dogo, mkakati ambao naona umefanikiwa sana. Isitoshe, Kamati kutaka kujiridhisha na hatua za Bodi ni sehemu ya msingi ya utekelezaji wa majukumu ya Kamati yaliyowekwa kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge na pia Shirika la TANESCO ni moja kati ya mashirika ambayo yanawajibika kwetu kwa hesabu zake na pia ufanisi wake kwa ujumla. Tumefanya hivyo pia katika mashirika mengine, hili la TANESCO sio tukio la kipekee;
  3. Kitendo hiki cha halali na kwa mujibu wa Kanuni kilichofanywa na Kamati yangu kimetafsiriwa kwa makusudi na baadhi ya watu kwamba ni ishara ya kuwa sisi au zaidi kwamba mimi nina maslahi binafsi na TANESCO na hususan Mkurugenzi wake Injinia Mhando, ndio maana tumetaka maelezo ya Bodi. Ukweli kwamba Kamati ya POAC tumewaita pia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu (CAG) na Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kwa jambo hilo hilo umefichwa kwa makusudi!
  4. Baada ya tukio hilo, nikiwa hapa Dodoma, mwandishi wa habari wa gazeti moja alinifuata akiniambia kuwa wamekutana na Mhe. Waziri Mhongo na Katibu Mkuu wake, Nd. Eliachim Maswi hapa hapa Bungeni na wamewaambia kuwa mimi nimepewa rushwa. Hakutaja nimepewa rushwa na nani, kiasi gani na wala kwa lengo gani!
  5. Nimejaribu kumtafuta kwa simu Mhe. Waziri Mhongo na Katibu Mkuu wake ili wanipe ufafanuzi juu ya mimi na Kamati ya POAC kuhusishwa na tuhuma hizi bila mafanikio, hali ambayo inaniondolea mashaka juu ya ushiriki wao katika kueneza au kuthibitisha uvumi huo. Najaribu sana kujizuia kutokuwa na mashaka na ushiriki wao huo ikizingatiwa uzito na taswira ya nafasi zao katika jamii, lakini wameshindwa kunidhihirishia tofauti.
Sasa naomba kutoa ufafanuzi rasmi kuhusu mlolongo wa matukio hayo tajwa ambayo yanatumiwa na baadhi ya wanasiasa kuonesha kwamba eti nimehusika na vitendo vya rushwa.

  1. Binafsi sijawahi kuwa na mawasiliano ya aina yeyote na uongozi wa TANESCO kushawishiwa juu ya hatua ambazo POAC ndio imezichukua za kutaka kujiridhisha juu ya utaratibu uliotumika. Ieleweke wazi kabisa kuwa, hakuna wakati wowote, popote ambapo mimi binafsi au Kamati yetu imekataa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO kuchunguzwa kwa tuhuma zozote. Ambacho tumesisitiza wakati wote ni ufuatwaji wa taratibu, kanuni na sheria, hili nitalisimamia iwe masika au kiangazi;

  1. Ni kwa sababu hiyo, na kwa kujiamini kabisa nimeunga mkono suala la tuhuma za rushwa zinazotajwa zichunguzwe na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa kina;

  1. Nimekwenda mbali zaidi kukiomba chama changu CHADEMA kifanye pia uchunguzi na tathmini yake kwa kina kujiridhisha na tuhuma hizo;

  1. Natumia fursa hii pia kuomba vyombo vya Dola vichunguze tuhuma hizo kwa nafasi yake ili kuweza kupata ukweli;

  1. Ninaahidi kushiriki kikamilifu iwapo nitatakiwa katika uchunguzi wowote utakaofanywa na niko tayari kuwajibika iwapo nitakutwa na hatia yeyote.
Napenda niwatoe hofu wananchi wa jimbo la Kigoma Kaskazini walionituma kuja kuwawakilisha hapa Bungeni na Watanzania wote kwa ujumla kwamba:-

  1. Mimi Zitto Zuberi Kabwe sina bei, sijawahi kuwa nayo na sitarajii kuwa nayo huko mbeleni. Daima nimesimamia kidete maadili ya uongozi bora katika maisha yangu yote ya siasa, na nawaahidi sitarudi nyuma katika mapambano dhidi ya rushwa katika nchi hii pamoja na mikakati ya aina hii ya kunidhoofisha na kunivunja moyo;

  1. Nafarijika na salam mbali mbali zinazotolewa kunifariji na kusisitiza kuwa nisilegeze kamba katika mapambano haya, nimepokea ujumbe mwingi kwa simu, sms, tweeter na hata facebook na niko pamoja nanyi Watanzania wenzangu kamwe sitarudi nyuma hadi kieleweke. Naamini katika nchi yetu tunazo rasilimali za kutosha mahitaji/haja ya kila mmoja wetu lakini si ‘tamaa/ulafi' wa baadhi ya watanzania wenzetu;

  1. Napenda kuweka rekodi sawa kwa Watanzania kwamba nimekuwa Mbunge hiki ni kipindi cha pili, Mimi ni Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) huu ni takriban mwaka wa saba sasa, Kamati yangu inasimamia mashirika 259 ya Umma na si TANESCO peke yake. Mchango wa Kamati hii katika Bunge na kwa ustawi wa Mashirika ya Umma ni bayana na haujawahi kutiliwa shaka. Kamati yetu imeokoa upotevu mkubwa wa mali za umma na kuokoa fedha za umma kutokana na umakini wake. Tumefanya hivyo CHC hivi karibuni, Kiwira na kwenye mashirika mengine mengi. Kote huko uadilifu na uzalendo wa Kamati hii haujawahi kuhojiwa. Inatuwia vigumu kuona kuwa tunahojiwa katika suala hili la TANESCO. Hapa pana kitendawili.

  1. Zipo hoja pandikizi za kutaka Kamati ya POAC ivunjwe na haswa zikinilenga mimi binafsi. Nafahamu kiu ya wasioitakia mema nchi yetu kuiona POAC ikivunjwa au sura zikibadilishwa kwa kuwa Kamati hii imekuwa mwiba kwa mikakati yao ya kifisadi. Kwa maoni yangu, Kamati ya POAC isihusishwe na tuhuma hizi kwa vyovyote vile. Niko tayari nihukumiwe mimi kama mimi na sio kuhusisha wajumbe wengine ambao hawatajwi mahala popote katika tuhuma hizi mbaya sana katika historia ya Bunge letu. Nitakuwa tayari kunusuru Kamati ya POAC na maslahi ya taifa letu kwa kujiuzulu Uenyekiti iwapo itathibitika pasipo shaka kuwa nimehongwa. Kamati ya POAC ni muhimu zaidi kuliko mimi.

  1. Nafahamu pia kuwa kuna wanasiasa hasa wa Upinzani ambao wanautaka sana Uenyekiti wa POAC na wanafanya kila njia kutaka kuidhoofisha. Lakini hawajui kuwa anaepanga wajumbe wa Kamati ni Spika wa Bunge.

  1. Msishangae pia kuja baadae kubaini kwamba baadhi ya wanasiasa wenye midomo mikubwa ya kutuhumu wenzao wao ndio vinara wa kupokea rushwa.

  1. Ni lazima tufike mahali kama viongozi kwamba utaratibu unapokiukwa na yeyote yule, au uongo unapotolewa hadharani tuseme bila kuogopa. Hili ndio jukumu letu kama wabunge na viongozi. Kusimamia ufuatiliaji wa utaratibu ni jukumu letu kama Kamati ya POAC na ndio sababu ya msingi ya kuanzishwa kwa mamlaka kama CAG na PPRA. Haiwezekani, tuwe na set ya kanuni kwa kundi fulani na nyingine kwa makundi mengine, au kuhukumu ufuataji wa taratibu kwa kuangalia sura ya mtu usoni
Mwisho
Kumejengeka tabia hivi sasa ya kuwamaliza wanasiasa wenye kudai uwajibikaji na uzalendo. Kumeanzishwa kiwanda kwenye medani ya siasa cha kuzalisha majungu na fitna zenye lengo la kuwachonganisha wanasiasa wa aina hiyo na wananchi kwa kutumia vyombo vya habari na nguvu ya fedha. Naamini mbinu hizi chafu, kama nyingine nyingi zilizojaribiwa kwangu huko nyuma nazo zitashindwa.
Naamini katika kweli na kweli daima huniweka huru. Naamini kuwa mwale mdogo wa mwanga wa mshumaa hufukuza kiza. Kwa imani hiyo, sitasalimu amri mbele ya dhamira zao ovu hata nitakapobaki peke yangu katika mapambano hayo ya kulinda na kutetea rasilimali za taifa zinufaishe watanzania wote.
Daima nitaongozwa na busara ya Hayati Shabaan Robert isemayo, ‘Msema kweli huchukiwa na marafiki zake, nitakapofikwa na ajali hiyo, sitaona wivu juu ya wale wawezao kudumu na marafiki zao siku zote, siwezi kuikana kweli kwa kuchelea upweke wa kitambo, nikajitenga na furaha ya kweli itakayotokea pale uwongo utakapojitenga".
Ahsanteni sana.
Zitto Zuberi Kabwe
 
Nilishasema Zitto ni mpumbavu, sasa hiyo statement yake ndio kusema kuna wabunge wenzake wa Chadema wanamuonea wivu yeye kuwa Mwenyekiti wa hiyo kamati ya POC na wanataka ang'olewe ili wapewe wao!! kweli nyinyi Chadema mnaamini Zitto ni mwenzenu na mnajenga chama kimoja?
Hongera sana James Mbatia sisimizi kama huyu Zitto Kabwe huwa hauwafugi.
 
bwana zito sizani kama ni kweli kila mtu akusingizie wewe tu
mi nachokuomba jitahid kujirekebisha tu
 
Back
Top Bottom