Manyerere Jackton
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 2,438
- 4,461
Awali ya yote niseme watu wanaothubutu kuitibua JF ili isiwe hewani, ni wa kulaaniwa.
Nchi inayoamini katika uhuru wa habari haiwezi kuwavumilia watu wa aina hiyo.
Pili, leo kwenye magazeti mengi, Mzee Samuel Sitta, ametamba kweli kweli. Anautaka u-Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mzee Sitta, anajijengea umaarufu mkubwa wakati wa uongozi wake wa Bunge mwaka 2005-2010. Kipindi kilichofuata alipambana na sifa ngumu ya ama kubadili jinsi ili awe na sifa ya kuwania tena u-Spika, au aendelee na jinsi yake na kwa hiyo aukose u-Spika. Akaukosa.
Akaingia kwenye Bunge la Katiba kama Mwenyekiti (Spika). Huko akafanya madudu kadri alivyoweza.
Alichuma aibu kubwa kwa kufinyanga mapendekezo murua yaliyokuwa kwenye Tume ya Jaji Warioba. Baada ya hapo akawa hana amani. Akawa mtu wa kushambuliwa kwa maneno makali.
Serikali ya Awamu ya Tano ndiyo hiyo imeshabisha hodi. Sitta, ameibuka kwa kasi ya aina yake akiutaka u-Spika. Licha ya umri wake kumtupa mkono, bado anaamini ni yeye mwenye uwezo wa kulimudu hili Bunge jipya.
Sijui kitu gani kimemvuta (ulevi wa madaraka?), labda anataka "kufukia mashimo" aliyosababisha kwenye Bunge Maalum la Katiba.
Ushauri wangu: Sitta aachane na madaraka haya anayotaka. Atachuma aibu kama wazee wenzake-Piusu Msekwa, John Malecela, na juzi tu; Mzee Steven Wasira.
Mabadiliko wanayotaka Watanzania hayawezi kuletwa na watu wa aina ya Mzee Sitta. Tangu Awamu ya Kwanza hadi Awamu ya Tano awe kiongozi tu-haiwezekani. Kibaiolojia, umri mkubwa unapunguza na hata kuondoa uwezo wa nguvu kimwili na kiakili. Watanzania hawawezi kuyapata mabadiliko wanayoyataka kama wataendelea kuongozwa na mashine zile zile za tangu Uhuru.
Kama Mzee Sitta, anapita humu Jukwaani, apokee ushauri wangu. Kama hapiti, basi afikishiwe ujumbe huu. Ameshakuwa Agazo la Kale, na sasa Watanzania wanataka Agano Jipya! Wanaomtakia heshima njema aliyobaki nayo kazi alizolifanyia Taifa watamwambia: "Mzee pumzika, usimalizie heshima kidogo iliyobaki baada ya kuvurunda kwenye Bunge la Katiba".
Nawasilisha.
Nchi inayoamini katika uhuru wa habari haiwezi kuwavumilia watu wa aina hiyo.
Pili, leo kwenye magazeti mengi, Mzee Samuel Sitta, ametamba kweli kweli. Anautaka u-Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mzee Sitta, anajijengea umaarufu mkubwa wakati wa uongozi wake wa Bunge mwaka 2005-2010. Kipindi kilichofuata alipambana na sifa ngumu ya ama kubadili jinsi ili awe na sifa ya kuwania tena u-Spika, au aendelee na jinsi yake na kwa hiyo aukose u-Spika. Akaukosa.
Akaingia kwenye Bunge la Katiba kama Mwenyekiti (Spika). Huko akafanya madudu kadri alivyoweza.
Alichuma aibu kubwa kwa kufinyanga mapendekezo murua yaliyokuwa kwenye Tume ya Jaji Warioba. Baada ya hapo akawa hana amani. Akawa mtu wa kushambuliwa kwa maneno makali.
Serikali ya Awamu ya Tano ndiyo hiyo imeshabisha hodi. Sitta, ameibuka kwa kasi ya aina yake akiutaka u-Spika. Licha ya umri wake kumtupa mkono, bado anaamini ni yeye mwenye uwezo wa kulimudu hili Bunge jipya.
Sijui kitu gani kimemvuta (ulevi wa madaraka?), labda anataka "kufukia mashimo" aliyosababisha kwenye Bunge Maalum la Katiba.
Ushauri wangu: Sitta aachane na madaraka haya anayotaka. Atachuma aibu kama wazee wenzake-Piusu Msekwa, John Malecela, na juzi tu; Mzee Steven Wasira.
Mabadiliko wanayotaka Watanzania hayawezi kuletwa na watu wa aina ya Mzee Sitta. Tangu Awamu ya Kwanza hadi Awamu ya Tano awe kiongozi tu-haiwezekani. Kibaiolojia, umri mkubwa unapunguza na hata kuondoa uwezo wa nguvu kimwili na kiakili. Watanzania hawawezi kuyapata mabadiliko wanayoyataka kama wataendelea kuongozwa na mashine zile zile za tangu Uhuru.
Kama Mzee Sitta, anapita humu Jukwaani, apokee ushauri wangu. Kama hapiti, basi afikishiwe ujumbe huu. Ameshakuwa Agazo la Kale, na sasa Watanzania wanataka Agano Jipya! Wanaomtakia heshima njema aliyobaki nayo kazi alizolifanyia Taifa watamwambia: "Mzee pumzika, usimalizie heshima kidogo iliyobaki baada ya kuvurunda kwenye Bunge la Katiba".
Nawasilisha.