Ushauri Wangu Kwa ACT, CHADEMA, CUF na NCCR-Mageuzi

Ushauri Wangu Kwa ACT, CHADEMA, CUF na NCCR-Mageuzi

SUBE2021

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2011
Posts
348
Reaction score
103
UCHAGUZI WA WABUNGE WA AFRIKA MASHARIKI
Nimetafakari sana juu ya ukuaji wa Demokrasia na Nafasi ya Upinzani Imara Wenye Mshikamano na Umoja. Wakati huu kama alivyosema Mh Lema wakati wa Kongamano la ACT juu ya Azimio la Arusha, Ndio wakati wa Muhimu sana kuungana kuliko ilivyowahi kutokea. Namna gani tunaungani ni kwa kwenda na dhana ya give and take ili tufaidike lakini tujiimarishe kwa mstakabali wa kukuza demokrasia na kuongeza nguvu ya Mapambano. Bado hatujachelewa kutengeneza kitu kizuri chenye umoja. Ifikie pahalatofauti zetu na historia zitupe fundisho na tuzizike.

Tusipoangalia vizuri uchaguzi huu wa Wabunge wa East Africa utaacha umetugawanya kwelikweli na ikiwezekana kugawa hata UKAWA ili wafadhili wa Akina Bwana Yule Waendelee Kujenga nguzo za kubomoa Upinzani ambao ulikuwa unakua kwa kasi. Natumeshaanza kusikia Bwana Yule Karibuni Ataongeza nguvu ya Mjomba aliyeenda kupikwa kwenye Jungle. Mpaka imefikia Mjomba kutoka kwenye Jungle anasema Upinzani utakuwa umekufa kufikia 2020; Tungepiga picha ya mbeleni tungekuwa tumeona analenga nini.

Kama kanuni zinaruhusu na ACT na NCCR Mageuzi wawe na wagombea kwenye Bunge la Afrika Mashariki. Tukubaliene na Kugawana nafasi na mimi Sayansi Yangu inanituma Mgawanyo uwe hivi; Tuchukulie Nafasi Zile Tatu ni za Wapinzani na Wote Tuheshimu Uwakilishi Tulionao Tuitane na Tukae Pamoja na Kukubaliana kwamba. ACT na NCCR vyenye wabunge mmoja mmoja vitoe Majina Mawili halafu waje mbele ya wabunge wote wa Upinzani wajinadi halafu, wabunge wa Upinzani wapige kura apatikane Mtu mmoja ambaye vyama vyote viwili viridhie atakayeongoza ndo asimamishwe kugombea. Halafu zile nafasi mbili moja awepo Mgombea kutoka CHADEMA mmoja na Mwingine kutoka CUF mmoja. Na tutakachofanya sisi kama wapinzania tuwasilishe majina yetu hayo matatu tu. Tutakuwa tumeshinda fitina ya "Divide and Rule" Wagawe na Uwatawale.

Na Wagombea wetu watatu waende wakiwa ni wao tu na watapigiwa kura za ndiyo na Hapana na Ushindi Utakuwepo umefanyika Kimkakati lakini zaidi umoja uliokomaa miongoni mwa vyama vya upinzani utakuwa umeanza kujenga. Tusipofanya haya maana wapiga kura ndani ya Bunge si wabunge wa upinzani tu bali wabunge wote. Kuna Hatari ya kuamua kukomoana na kupandikiza Chuki ambazo hazipo. Yawezekana upande wa Pili wakajipanga kwamba Tupigie watu wa CUF tu na ACT ili CHADEMA ikose ili ujengwe mgogoro mwingine ndani ya UKAWA kuukomaza ule wa Bwana Yule na kuleta Mparaganyiko. Au Yawezekana wakaamua tumwangushe Mgombea wa ACT Wazalendo, Ili ACT aone anatengwa na Wenzie katika Upinzani na ageuke na kuwa Peke Yake. Yawezekana wakaamua tumpigie wa ACT au wa NCCR na wawili wa CHADEMA ili CUF waone wamehujumiwa na CHADEMA na hivyo kuleta Mgogoro kwenye UKAWA. Ebu Tushinde Kiakili na Tushinde kwa kuimarisha Mshikamano na Umoja.

Nimeandika haya ili tuone jinsi navyoweza kufumbwa macho na tukazalisha mparaganyiko na mwisho wa siku Bwana Yule na Mjomba aliyepo Mafichoni wakawa washindi na Upinzani Ukawa umefifia au umeanguka Ndembendembe kufikia mwaka wa 2020.

Hatujachelewa viongozi wote wa vyama vya upinzane na vyenye uwakilishi bungeni ebu kutaneni haraka kwa dharura, chagueni kujenga nguza na UKUTA Imara usioruhusu risasi nyepesi na ngumu kupenya kwa njia yoyote ile. Mtaniambia kama hamtachagua kujenga siko siyo chache nimeota limgogoro hilo likubwa linakuja. Mnakuwa mnapigwa hata kwa kiwembe na upinde wala haitahitajika risasi na mitutu kuwamaliza.

Mwisho na declare interest, Mimi ni Mkereketwa, Mwanachama na mwana mabadiliko kupitia CHADEMA
 
Zitto usisikie yule anayekushauri kubomoa eti komaa. Hakujawahi kuwa na Ushindi katika Vita yoyote. Mshindi ni wakati tu. Kama mna vita au mafarakano. Utashinda Leo Nitashinda Kesho Utashinda Keshokutwa. Mimi nimeshauri ili tushinde Daima kumbukeni huu si ushauri wa chama chochote kwa Zito au Kwa wote niliowashauri. Huu ni Ushauri tu wa Mtu wa Kawaida Mimi niliye nje ya ulingo wa uongozi wa chama changu cha CHADEMA lakini naona mbali na kufikiria kujenga zaidi kuliko kubomoa. Wanaosema Zitto Komaa ni walewale wanaotaka ubomoe ili wao wanufaike na washerehekee.
 
Hawa Chadema badala ya kuwashawishi wabunge wa CCM, wanakomaa kuwarubuni ACT.!

Nimesema Post hii Si ya Chama Cha CHADEMA ni ya Mwanachama Mwenye Maono, Hivyo agument za CHADEMA inamrubuni Zitto siyo sahihi hata kidogo. Lakini Pia unapotafuta kujenga unaanza na rasilimali ulizo nazo ndani kabla hujaenda kuomba. Huwezi kwenda kuomba bati na Saruji huku huna kiwanja utakapojengea. Kujenga Umoja ndani ya upinzani ndiko kunaweza kuwasaidia kwa pamoja kuomba kura kwa wabunge wa CCM
 
Hawana strategy hao mzee slaa toka aondoke hawajui kipi ni kipi

Kalia hilo kwamba hawana strategy wakati hata hii iliyotolewa ni strategy tena ya Mwanachama wa Kawaida Kabisa Nisiyejulikana. Huku Kuna Hazina ya Strategy ndo Maana hata wakati wa Uchaguzi Mkuu kille Chama ambacho Leo Ilikuwa Ni Sikuku Yao Walilazimika Kuiba Kauli mbiu ya M4C na Chama cha CHADEMA kikawaachia kwa sababu hakuna great thinkers huko au hata wakiwepo lazima wafiche fikra zao nzuri mifukoni maana wakisema tu wanaitwa wasaliti. Ukitaka kujua Chama Chenu Kilivyo na Macoca ZERO kasikilize wimbo wa WAPO. AnyWay Heri Kwa Siku Yenu Ya Leo
 
Nimesema Post hii Si ya Chama Cha CHADEMA ni ya Mwanachama Mwenye Maono, Hivyo agument za CHADEMA inamrubuni Zitto siyo sahihi hata kidogo. Lakini Pia unapotafuta kujenga unaanza na rasilimali ulizo nazo ndani kabla hujaenda kuomba. Huwezi kwenda kuomba bati na Saruji huku huna kiwanja utakapojengea. Kujenga Umoja ndani ya upinzani ndiko kunaweza kuwasaidia kwa pamoja kuomba kura kwa wabunge wa CCM
Mkuu mawazo yako ni ya msingi sana... Tatizo ni kwamba Chadema hakijawahi kuwa rafiki wa kweli wa vyama vidogo vya upinzani hadi pale wanapotafuta maslahi yao ndio wanavikumbuka..

Chadema inaungana na vyama vidogo kutetea maslahi yake tu na si vinginevyo...

Hawa hawa Chadema walimkosesha Matatiro jimbo licha ya kuwa wote wapo ukawa.... Matokeo yake yule aliemharibia Mtatiro akapewa viti maalum...
 
Tafa
CHADEMA achene uroho wa madaraka kwenye uchaguzi mkuu mlipewa majimbo mengi na vyama vingine sasa hivi ni zamu ya ACT Wazalendo sasa


Tafadhali CHADEMA Haijaandika Makala, Hii nimeandika mimi huu mtazamosi wa Chama Changu Cha CHADEMA. Ni mawazo na fikra zangu mimi niliyeshauri. Lakini CHADEMA haikuizuia ACT kugombea kwenye Majimbo na ACT Wazalendo Haikuwa Mwanachama ndani ya umoja wa UKAWA bali walisimama wao kama wao
 
Mkuu mawazo yako ni ya msingi sana... Tatizo ni kwamba Chadema hakijawahi kuwa rafiki wa kweli wa vyama vidogo vya upinzani hadi pale wanapotafuta maslahi yao ndio wanavikumbuka..

Chadema inaungana na vyama vidogo kutetea maslahi yake tu na si vinginevyo...

Hawa hawa Chadema walimkosesha Matatiro jimbo licha ya kuwa wote wapo ukawa.... Matokeo yake yule aliemharibia Mtatiro akapewa viti maalum...


Ukitaka kuijua vizuri issue ya Mtatiro Ongea Nae Vizuri Ujue Ilikuwaje. Pia Muulize Mtatiro faida na Hasara za UKAWA. Changamoto Zipo Penye Wengi na Zinatafutiwa Tiba ili Kwenda Mbele. Akikujibu Faida Za UKAWA utakuwa na jibu zuri la kama kweli CHADEMA huungana kuumiza vyama vingine.

Aidha kabla ya Muunga na Baada ya Muungano wa UKAWA fanya Objective Analysis uone kama kuna mabadiliko, faida na Hasara
 
Tafa



Tafadhali CHADEMA Haijaandika Makala, Hii nimeandika mimi huu mtazamosi wa Chama Changu Cha CHADEMA. Ni mawazo na fikra zangu mimi niliyeshauri. Lakini CHADEMA haikuizuia ACT kugombea kwenye Majimbo na ACT Wazalendo Haikuwa Mwanachama ndani ya umoja wa UKAWA bali walisimama wao kama wao
kwa nini sasa hivi wasiviachie vyama vingine vya UKAWA nao wapate wawakilishi wengi bungeni mfano CUF,NCCR Mageuzi wao CHADEMA kila nafasi wanataka wao tu achene uroho wa madaraka
 
Ushauri mzuri sana! Mnaoweza kuwasiliana Nao kwa simu washaurini! Vinginevyo huu uchaguzi utatuacha tumenuniana na chama cha magamba watacheka sana!
 
Ukitaka kuijua vizuri issue ya Mtatiro Ongea Nae Vizuri Ujue Ilikuwaje. Pia Muulize Mtatiro faida na Hasara za UKAWA. Changamoto Zipo Penye Wengi na Zinatafutiwa Tiba ili Kwenda Mbele. Akikujibu Faida Za UKAWA utakuwa na jibu zuri la kama kweli CHADEMA huungana kuumiza vyama vingine.

Aidha kabla ya Muunga na Baada ya Muungano wa UKAWA fanya Objective Analysis uone kama kuna mabadiliko, faida na Hasara
hakuna cha kuongea nae inafahamika wazi Mtatiro amekoseshwa ubunge makusudi na CHADEMA....CHADEMA walijua Mtatiro akiingia bungeni atawafunika sana walichofanya ni kumkosesha ubunge na aliemkosesha ubunge akazawadiwa viti maalum
 
kwa nini sasa hivi wasiviachie vyama vingine vya UKAWA nao wapate wawakilishi wengi bungeni mfano CUF,NCCR Mageuzi wao CHADEMA kila nafasi wanataka wao tu achene uroho wa madaraka


Hivi si Viti Vya Wabunge, Bunge la Jamhuri ya Muungani ni Viti vya Bunge la Afrika Mashariki. Bado CHADEMA ina haki na nafasi pia ya kushiriki katika bunge hilo. Lakini swala kama ni wenye viti vichache kuachiwa na wenyeviti vingi vya ubunge basi ili uwe na uchambuzi wa kina ungelikishauri hata Chama Chako cha CCM chenye Viti Vingi Kuacha Hizo nafasi za Afrika Mashariki kwa Vyama vyenye wabunge wachache. Kuweni analytical not spectators.
 
hakuna cha kuongea nae inafahamika wazi Mtatiro amekoseshwa ubunge makusudi na CHADEMA....CHADEMA walijua Mtatiro akiingia bungeni atawafunika sana walichofanya ni kumkosesha ubunge na aliemkosesha ubunge akazawadiwa viti maalum

It is Because of Your Understanding Capacity; BASHITEISM.
 
Hivi si Viti Vya Wabunge, Bunge la Jamhuri ya Muungani ni Viti vya Bunge la Afrika Mashariki. Bado CHADEMA ina haki na nafasi pia ya kushiriki katika bunge hilo. Lakini swala kama ni wenye viti vichache kuachiwa na wenyeviti vingi vya ubunge basi ili uwe na uchambuzi wa kina ungelikishauri hata Chama Chako cha CCM chenye Viti Vingi Kuacha Hizo nafasi za Afrika Mashariki kwa Vyama vyenye wabunge wachache. Kuweni analytical not spectators.
sawa lakini kumbuka CHADEMA iko kwenye muungano wa UKAWA ndio maana hata kwenye uchaguzi waliachiana majimbo na hata kwenye urais walimwachia mgombea wa CHADEMA huu ni muungano mkuu sasa huo muungano una maana gani kama kila chama kitaweka mgombea wake? hujui hata ruzuku ya CHADEMA nyingi imetokana na huu muungano? kwa nini inapokuja kwenye kugombea madaraka CHADEMA wanawadhulumu UKAWA wenzao?
 
sawa lakini kumbuka CHADEMA iko kwenye muungano wa UKAWA ndio maana hata kwenye uchaguzi waliachiana majimbo na hata kwenye urais walimwachia mgombea wa CHADEMA huu ni muungano mkuu sasa huo muungano una maana gani kama kila chama kitaweka mgombea wake? hujui hata ruzuku ya CHADEMA nyingi imetokana na huu muungano? kwa nini inapokuja kwenye kugombea madaraka CHADEMA wanawadhulumu UKAWA wenzao?


Hakuna CHADEMA walipowadhulumu wenzao kwenye uchaguzi wowote. Kumbuka Kinachojadiliwa mada iliyopo mezani ni Wabunge wa Afrika Mashariki. Rejea Mwongozo wa Spika halafu useme CHADEMA imewadhulumje wenzake. Argue with substance. Usidandie Gari kwa Mbele.
 
Back
Top Bottom