Ushauri wa haraka unahitajika

Ushauri wa haraka unahitajika

Mfagio

JF-Expert Member
Joined
May 13, 2014
Posts
703
Reaction score
877
Mimi ni kijana wa miaka 25 nilikuwa nakaa kwa kaka yangu ambaye nilikuwa na msaidia sana kazi za shamba na nyumbani, tatizo likaja mimi nililima shamba kama ekari 1 bila kumwambia sasa ajakugundua baada ya kukundua kanyangasha langu pia sikatai kuwa rasilimali zingine nilikuwa na chukua shambani kwake baada ya hapo ukatokea ugomvi na kwake kanitimua.

Naomba ushauri, nini nifanye?
 
Hebu waone kwanza wazazi usikie wanakushauri nini, kama hawapo mwachie shamba hilo katafute maisha mengine mbali na kwake. Japo nahisi kuna mengine hujayasema hapa.
Ni kwel sema nimeogopa uzi kuwa mrefu
 
Vuna mazao ya hilo shamba ulilolima, uza ufanye mtaji wa kumuacha kaka yako aendelee na maisha yako.
 
Kwa Nini ulimficha hilo jambo kaka yako Na lengo lako lilikua ni nini ?
Hapo kiongozi ndo nilifanya makosa nimejaribu kumuomba msamaha hata simu yangu hapokei wala kujibu message
 
Kumficha sio kosa sana.

Je una sababu zilizopelekea kumficha?.

Mfano, Labda ulitaka ujaribu kitu chako mwenyewe.
Labda ulihisi ukimwambia hatakubali na ataona unamuibia.
Labda ulihisi ukimwambia ataona hutumii muda mwing zaid kuangalia mashambq yake na utakuwa umejidhatiti kuangalia shamba lako.

Labda labda nadhan ni nyingi. Hizo haswaaa ndio zitumie kuombea msamaha.

Sio unaomba msahama kaka nisamehe , alaf unakaa kimya. Hakuna mtu angekuelewa
 
Mbaka hapo una shida mahala
Wewe unawezaje kukaa na kaka yako, Tena kwake, na malighafi zake, alafu ukafanya Jambo kubwa kama kulima heka 1, since kuandaa shamba,kupalilia,mbegu, n.k
Bila yeye kumpa taarifa.😲

Kwa haraka haraka we ni msiri na ni mbinafsi ukiendekeza tabia iyo utakuwa mchawi uzeeni.
 
Kumficha sio kosa sana.

Je una sababu zilizopelekea kumficha?.

Mfano, Labda ulitaka ujaribu kitu chako mwenyewe.
Labda ulihisi ukimwambia hatakubali na ataona unamuibia.
Labda ulihisi ukimwambia ataona hutumii muda mwing zaid kuangalia mashambq yake na utakuwa umejidhatiti kuangalia shamba lako.

Labda labda nadhan ni nyingi. Hizo haswaaa ndio zitumie kuombea msamaha.

Sio unaomba msahama kaka nisamehe , alaf unakaa kimya. Hakuna mtu angekuelewa
Kwa kwel umeongea kitu cha maana nitatumia ushauri wako asante sana
 
Mbaka hapo una shida mahala
Wewe unawezaje kukaa na kaka yako, Tena kwake, na malighafi zake, alafu ukafanya Jambo kubwa kama kulima heka 1, since kuandaa shamba,kupalilia,mbegu, n.k
Bila yeye kumpa taarifa.[emoji44]

Kwa haraka haraka we ni msiri na ni mbinafsi ukiendekeza tabia iyo utakuwa mchawi uzeeni.
Siwezi kabisa kwa saiz nimejifunza kitu tatizo tamaa za ujanani zinatutesa
 
Back
Top Bottom