Ushauri wa fasta fasta unahitajika..

Ushauri wa fasta fasta unahitajika..

FirstClass

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2016
Posts
1,149
Reaction score
1,470
Hivi kwa binti unayempenda, yani unamalengo nae. Ikitokea amekuomba pesa. Ukamjibu ' sina '. Kisha akakata mawasiliano gafla. Jeh unahaja ya kuendelea kuwa na malengo nae..??

Kuna ndugu yangu anaomba ushauri..

Nilichomshauri mimi..
Kwanza nilimuuliza.....

Mimi- mna muda gani na binti huyo..?

Yeye- Mwezi1

Mimi- Jeh imewahi tokea ukampa pesa yeyote alipokuomba..?

Yeye- Hapana, huwa namuungia bando tu. Hajawai niomba pesa kabla..

Mimi - Mlikutana wapi kwa mara ya kwanza..?

Yeye- Stand ya daladala

Mimi- Alikuomba bei gani..?

Yeye- Elf30

Mimi- Ulimpatia majibu gani ?

Yeye- Nilimwambia kwa sasa sina..

Mimi- Umejuaje kama amekata mawasiliano.. ?

Yeye- Nikimpigia hapokei..


Mimi - Umempgia mara ngapi..?

Yeye- Zaidi ya mara5..


Mimi - Kwanini unajipa tabu kwa mtu asiyepokea simu yako kwa sababu ya elfu30..?

Yeye- Kimya..

Interview ikaishia hapo..

Mshaurini na nyie huyu jamaa. Maana amekuja kunikopa hapa..
 
Apige chini hiyo chombo,atapata wengine wanaoelewa hali ya sasa,yaani yeye akiomba lazima uwe na hela ya kumsaidia,maana siku hazilingani ati
 
Kinachoniuma n ktendo cha mimi kukopwa.. Yani mrembo anasababisha presha kwa tusiohusika kabisa..
Mkuu kwa jinsi inavyokuuma huyo mtu utakuwa ni wewe tu. Hakuna cha ndugu yako wala nini. Ushauri wangu kwako ni huu "mtafute umpe hiyo elfu 30,000 ikiwezekana mpe hata zaidi ya hiyo. Mapenzi ya mwanzomwanzo bila ulimbo wa pesa hayaendi. Ukishakula mara mbili tatu hizo habari za pesa zitapungua sana. Kwa sasa kubali kuumia kwa faida ya baadae"
 
Hapana mkuu.
Si mimi.. Tumshauri tu ndugu yetu..
Mkuu kwa jinsi inavyokuuma huyo mtu utakuwa ni wewe tu. Hakuna cha mshikaji wako wala nini. Ushauri wangu kwako ni huu "mtafute umpe hiyo elfu 30,000 ikiwezekana mpe hata zaidi ya hiyo. Mapenzi ya mwanzomwanzo bila ulimbo wa pesa hayaendi. Ukishakula mara mbili tatu hizo habari za pesa zitapungua sana. Kwa sasa kubali kuumia kwa faida ya baadae"
 
Kwa sasa hali ilivyo mbaya bint ukiweza kumlisha tuu anakung'ang'ania tena pesa ndogo tuu anakuona kama baba ake mzazi....
HUYO BINT ACHANA NAE MAN MPIGAJI TUU "KANYAGA..KANYAGA"
 
Mtxt aje achukue hiyo pesa akikujibu jiongeze asipokujibu basi
 
Kanyaga mafuta, ongeza mwendo. Huna mpenzi hapo.
Tafuta mwingine mbona wako wengi sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom