Ushauri wa bure kwa Tundu Lissu na CHADEMA

Mh Lissu ni mmoja kati ya wabunge wanaochangia sana bungeni. anajituma sana na hili ni jambo zuri! tatizo alilonalo ni kuwa na papara ya kuchangia. ni vizuri akatulia na kutamka maneno yenye uhakika. jana alipokua anachangia hotuba ya uchukuzi, lissu alimlaumu waziri mwakyembe kwa kutotoa kauli ya pole kutokana na ajali ya meli znz. alimtaka aombe radhi na aeleze kwa nini ktk hotuba yake hakutaja ajali hiyo.

alisimama mbunge wa ccm na kunukuu ukurasa ambao una maneno ya pole kutokana na meli ya znz. lissu alinywea na kuomba radhi. lissu licha ya kuwa mwanasheria ni mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani.

Cheo hicho kinahitaji mtu makini anaetumia ubongo kwa umakini mkubwa. Mifano ya kuteleza kwa Lissu bungeni ni mingi. takriban kila anaposimama lazima ateleze. nawashauri chadema kumteua mnadhimu mwengine la sivyo hadhi ya chadema itazidi kushuka bungeni kila uchao


wakatabahu: wakuziba
mzee wa maneno ya ukweli unao choma nyoyo

Unashangaa hiyo mbona malipo ya NSSF hadi kufikisha umri wa kustaafu (miaka 55) yalipitishwa bila wabunge kujua?
 
.......mie nadhani aendelee hivyo hivyo ili watu wa jipange wasiende ovyo ovyo , aou kufanya mambo kinyume na amadili ya utawala bora kwasababu wanajua LISU yupo kuuliza!!!!!!

BIG UP LISU......... TUPO PAMOJA NA WEWE
 
Sasa Lissu alikuwa anataka pole gani wakati Rais alishatoa.
Kilaza, Mwakyembe ni waziri mwenye dhamana aliegoma kujiuzulu, kutokana na ajali mbaya ya MV Skagit, hata kutoa pole na kugusia ajali anakwepa? ha ha ha ha nadhan mwakyembe atakua hajapona vizuri, that why anazuia watu wasichimbe dawa barabarani wakati hakuna public toilets katika high ways. nadhan hajawahi kumuona mtu mwenye kisukari, tunamsamehe kwakuwa anaumwa... na dhaifu anaendelea kuwa dhaifu
 
Kwa maana hiyo unasoma tu kurasa za mbele harafu nyingine unaacha?
Mkuu, unaangalia uzito wa swala lenyewe its cant be resposble minister ambae anatakiwa kujiuzulu anashindwa kuanza na pole kwa watz zaidi ya 100 wamefariki, anaanza kupongeza mke wake kwanza... huu ndio udhaifu wa mwenyekiti na baraza lake.
 
Mh Lissu ni mmoja kati ya wabunge wanaochangia sana bungeni. anajituma sana na hili ni jambo zuri! tatizo alilonalo ni kuwa na papara ya kuchangia. ni vizuri akatulia na kutamka maneno yenye uhakika. jana alipokua anachangia hotuba ya uchukuzi, lissu alimlaumu waziri mwakyembe kwa kutotoa kauli ya pole kutokana na ajali ya meli znz. alimtaka aombe radhi na aeleze kwa nini ktk hotuba yake hakutaja ajali hiyo.

alisimama mbunge wa ccm na kunukuu ukurasa ambao una maneno ya pole kutokana na meli ya znz. lissu alinywea na kuomba radhi. lissu licha ya kuwa mwanasheria ni mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani.

Cheo hicho kinahitaji mtu makini anaetumia ubongo kwa umakini mkubwa. Mifano ya kuteleza kwa Lissu bungeni ni mingi. takriban kila anaposimama lazima ateleze. nawashauri chadema kumteua mnadhimu mwengine la sivyo hadhi ya chadema itazidi kushuka bungeni kila uchao


wakatabahu: wakuziba
mzee wa maneno ya ukweli unao choma nyoyo

Sasa huu ushauri unampa Lissu au CDM? Nadhani wewe unapomsikiliza Lissu unaconcentrate kwenye kuteleza kwake. Unadai mifano ni mingi (kwenye red) af unaishia kutoa mfano mmoja...!!!??? Kweli akili yako inafanya kazi vizuri wewe? Kwa kua ni mmoja wa wabunge wanaochangia sana bungeni na umedai kila anapochangia lazima ateleza nilitarajia uje na mifano angalau isiyopungua mitano.

Hata kama mimi ningekua Lissu, ushauri wako nisingeufuata.....
 
Wabunge wa Chadema wa kuchaguliwa ni 23 hao wengine wa kupewa mie siwatambui, sasa Lissu alikuwa anataka pole gani wakati Rais alishatoa.
1. who are you?
2. Rais wa Zanzibar ana uhusiano gani na Pole ya Mwakyembe kama waziri ambaye alizembea mpaka kusababisha ajari na vifo vya watanganyika na wazanzibar zaidi ya 100. ama unaongelea rais huyu dhaifu ambae ameamua kuwa jaji na kutoa hukumu?
 
Lissu anafanya vizuri na kutimiza wajibu wake vema bungeni.Makosa madogomadogo ni ya kibinadamu na yanarekebishika
 
Lissu jana aliumbuka kwa kutosoma vifungu ya hotuba akajikuta ananyamazishwa na mbunge wa Ole, Kassim Mbarouk, akamwambia mbona kaishatoa pole pitia ukurasa wa 3 (6) katika hotuba yake.

Bila kumtaja Slaa hujaona siku zako?
 
Mkuu, unaangalia uzito wa swala lenyewe its cant be resposble minister ambae anatakiwa kujiuzulu anashindwa kuanza na pole kwa watz zaidi ya 100 wamefariki, anaanza kupongeza mke wake kwanza... huu ndio udhaifu wa mwenyekiti na baraza lake.

Wewe kweli POMPO ueleweki Tundu Lissu alisema hivi bungeni "Mheshimiwa mwenyekiti kila mbunge aliyesimama hapa anatoa pole kwa ajali za MV Skagit ni Spice Islanders, lakini Waziri hakuna popote kwenye hotuba yake katoa pole, najua anaweza kuwa amepitiwa lakini Watanzania hawatamuelewa"

Hapo hapo Mwigulu Nchemba akaomba mwongozo kisha kumtaka Lissu ayafute maneno yake ya uongo ili kuweka kumbukumbu sahihi kwenye Hansard..

Mbunge wa Ole, Kassim Mbarouk aliomba tena mwongozo kisha kulieza bunge kwamba Waziri alitoa pole katika ukurasa wa 3. Hatimaye Lissu akukubali amepotoka.
 
Last edited by a moderator:
Mh Lissu ni mmoja kati ya wabunge wanaochangia sana bungeni. anajituma sana na hili ni jambo zuri! tatizo alilonalo ni kuwa na papara ya kuchangia. ni vizuri akatulia na kutamka maneno yenye uhakika. jana alipokua anachangia hotuba ya uchukuzi, lissu alimlaumu waziri mwakyembe kwa kutotoa kauli ya pole kutokana na ajali ya meli znz. alimtaka aombe radhi na aeleze kwa nini ktk hotuba yake hakutaja ajali hiyo.

alisimama mbunge wa ccm na kunukuu ukurasa ambao una maneno ya pole kutokana na meli ya znz. lissu alinywea na kuomba radhi. lissu licha ya kuwa mwanasheria ni mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani.

Cheo hicho kinahitaji mtu makini anaetumia ubongo kwa umakini mkubwa. Mifano ya kuteleza kwa Lissu bungeni ni mingi. takriban kila anaposimama lazima ateleze. nawashauri chadema kumteua mnadhimu mwengine la sivyo hadhi ya chadema itazidi kushuka bungeni kila uchao


wakatabahu: wakuziba
mzee wa maneno ya ukweli unao choma nyoyo

Duh! Hivi pole huandikwa au hutamkwa? Mh Dr Mkwakiembe alishindwa nini kutamka pole alipotoa hotuba yake na kusubiri watu waisome kwenye kabrasha?
 
Wewe kweli POMPO ueleweki Tundu Lissu alisema hivi bungeni "Mheshimiwa mwenyekiti kila mbunge aliyesimama hapa anatoa pole kwa ajali za MV Skagit ni Spice Islanders, lakini Waziri hakuna popote kwenye hotuba yake katoa pole, najua anaweza kuwa amepitiwa lakini Watanzania hawatamuelewa"

Hapo hapo Mwigulu Nchemba akaomba mwongozo kisha kumtaka Lissu ayafute maneno yake ya uongo ili kuweka kumbukumbu sahihi kwenye Hansard..

Mbunge wa Ole, Kassim Mbarouk aliomba tena mwongozo kisha kulieza bunge kwamba Waziri alitoa pole katika ukurasa wa 3. Hatimaye Lissu akukubali amepotoka.

Kumbe Lisu ni muungwana hivyo? Hana haja ya kuweka ligi na ubishi wa kijinga sio? Anapopotoka huwa anakiri na mambo yanaendelea mbele. Big up TL
 
No body is perfect,na huyo anaonekana ni kiongozi mzuri yupo makini,and he knows what he is talking about,sawa kuna wakati kwa namna moja au nyingine kama binaadamu anaweza kukosea,na kiongozi mzuri akilijua hilo,anaomba radhi na mambo yanaendelea.
 
[kikwete hajawahi kutoa pole ya wabunge waliokatwa mapanga na wahuni wa ccm
 
Back
Top Bottom