Ushauri wa Bure kwa TBC1!

LordJustice1

JF-Expert Member
Jan 19, 2011
2,263
530
Mara nyingi nimeona TBC1 wakiwaalika wabunge wa CCM na CUF katika kipindi cha Jambo Tanzania na mara nyingi Wabunge hao wamekuwa wakijaribu kujibu hoja zilizotolewa na CHADEMA Bungeni na kutoa lawama kwa chama hicho kikuu cha upinzani! Lawama nyingi za CCM na CUF zimekuwa hazijibu hoja za CHADEMA moja kwa moja bali zimekuwa ni 'calculated move' ya kukipaka matope CHADEMA!
Unless TBC1 nacho ni chombo cha kisiasa, nashauri wawe wanawaalika na Wabunge wa CHADEMA ili kupata upande mwigine wa shilingi!
Au mnasemaje wakuu?
 
Uko sawa mkuu,Hata mimi sijui kwa ninin hawa tbc wanafanya kitu namna hii. Watuhumiwa ni CDM, kwenye kutoa maelezo hawaitwi, wanaitwa watu wale wale, sasa sisi wanamchi ambao tbc ni ya kwetu, tutapata wapi maelezo ya upande wa wanaotuhumiwa?? Wabunge wa ccm walobaki bumngeni hawajadili huu muswada, na badala yake kila anayesimama ni kumshabulia MH. Tundu Lissu personally. Wengine wamekwenda mbali hata kuhoji weledi wake kwenye sheria, tena kwa kebehi. Mh Lissu ni msomi aliyebobea kwenye fani yake: WaTanzania wanajua hivyo na dunia nzima inajua hivyo!!Hii siyo haki kabisa,TBc angalieni mnachokifanya hakisaidii katika kumaliza utata huu. Kama alivyosema Machali wa NCCR, wananchi ndo wanaotaka muswada huu ungesomwa mara ya kwanza. Kwanini serikali ina haraka kupitisha?? Hii katiba ni ya wananchi na ndiyo wanaotaka washirikishwe katika hatua hii, kwa nini serikali inyoitwa "sikivu" imeziba masikio katika hili?? Kunakitu hapa. Tunawasubiri hao wabunge wa ccm warudi tuwaulize walikuwa wanawakilisha mawazo ya nani kwenye huu mchakato. Labda wote wabaki huko huko Dodoma au wakimbilie Dar kama walivyozoea.
 
Uko sawa mkuu,Hata mimi sijui kwa ninin hawa tbc wanafanya kitu namna hii. Watuhumiwa ni CDM, kwenye kutoa maelezo hawaitwi, wanaitwa watu wale wale, sasa sisi wanamchi ambao tbc ni ya kwetu, tutapata wapi maelezo ya upande wa wanaotuhumiwa?? Wabunge wa ccm walobaki bumngeni hawajadili huu muswada, na badala yake kila anayesimama ni kumshabulia MH. Tundu Lissu personally. Wengine wamekwenda mbali hata kuhoji weledi wake kwenye sheria, tena kwa kebehi. Mh Lissu ni msomi aliyebobea kwenye fani yake: WaTanzania wanajua hivyo na dunia nzima inajua hivyo!!Hii siyo haki kabisa,TBc angalieni mnachokifanya hakisaidii katika kumaliza utata huu. Kama alivyosema Machali wa NCCR, wananchi ndo wanaotaka muswada huu ungesomwa mara ya kwanza. Kwanini serikali ina haraka kupitisha?? Hii katiba ni ya wananchi na ndiyo wanaotaka washirikishwe katika hatua hii, kwa nini serikali inyoitwa "sikivu" imeziba masikio katika hili?? Kunakitu hapa. Tunawasubiri hao wabunge wa ccm warudi tuwaulize walikuwa wanawakilisha mawazo ya nani kwenye huu mchakato. Labda wote wabaki huko huko Dodoma au wakimbilie Dar kama walivyozoea.

Ni hii hii katiba tunayojaribu kuiepuka ndio inayowafanya TBC wawe vibaraka wa CCM. Katiba hii ya kale inampa mamlaka Rais kuteua watu muhimu na wenye nguvu kabisa ktk MIKOA na WILAYA na kuwafanya wawakilishi wake kwa wananchi badala ya wao kuwawakilisha wananchi kwake. Kwa maneno mengine hawa WAKUU WA MIKOA na WILAYA hawawajibiki kwa wananchi badala yake wanawajibika kwa Rais aliyewazawadia vyeo. Kwa minaajili hii, kujipendekeza kwa serikali ni sera binafsi ya kila mfanyakazi wa idara nyeti ktk habari ili siku moja awe kama Betty Mkwasa, Halima Kihemba na wengineo ambao kwa kuongea kwao vizuri kuhusu serikali wamezawadiwa. Unaweza kuona juzi hapa Betty Mkwasa ambaye kitaaluma ni mwanahabari, alikuwa mstari wa mbele kuwazuia wanahabari wenzake kufanya kazi yao ktk tukio la uvunjaji wa kihuni wa nyumba pale DODOMA. Huu ni ukibaraka ambao Watanzania inabidi tuukemee kwa nguvu zote.
 
Mara nyingi nimeona TBC1 wakiwaalika wabunge wa CCM na CUF katika kipindi cha Jambo Tanzania na mara nyingi Wabunge hao wamekuwa wakijaribu kujibu hoja zilizotolewa na CHADEMA Bungeni na kutoa lawama kwa chama hicho kikuu cha upinzani! Lawama nyingi za CCM na CUF zimekuwa hazijibu hoja za CHADEMA moja kwa moja bali zimekuwa ni 'calculated move' ya kukipaka matope CHADEMA!
Unless TBC1 nacho ni chombo cha kisiasa, nashauri wawe wanawaalika na Wabunge wa CHADEMA ili kupata upande mwigine wa shilingi!
Au mnasemaje wakuu?

Hili halina shaka. TBC1 wanakasoro kubwa tena kubwa. Nadhani wamekusoma
 
Ni kweli tbc hata mimi nimenote hii ila wajue kuwa ccm haitakuwapo milele na hawana uhakika kama hata kesho,wiki ijayo,mwezi ujao,mwaka ujao ama miaka ijayo hiyo ccm itakuwepo wanatakiwa watende haki hao wanaowabagua wanaweza kuwa ndo viongozi wao sasa sijui wataacha kazi ama??wajirekebishe wananchi tunawaona!!!!!!!
 
Mambo yote haya tunaweza kuyaweka katika neno moja KATIBA. Katiba ya sasa inawapatia CCM mamlaka ya ku-hire and fire mtu yeyote wanayeona hafanyi kazi za CCM kwa nafasi waliyompatia. Hawa TBC kama waganga njaa wengine wanatetea unga wao kwa mabwana wao waliowaweka. Usitarajie TBC kuwa huru na haki kwa hali ya sasa.

Kama TBC ingekuwa na Board yake iliyohuru inayoendeshwa kitaalam ingeajiri wataalam. TV za wenzetu kama BBC et al. Habembelezwa mwanasiasa hata awe ni mtawala.
 
hata mimi nimeliona hili siku nyingi na linanikera.Angalau ITV,MLIMANI TVna STARTV wanajitahidi kutuelimisha.Kweli TBC ya ukweli ilikuwa ya TIDO na hii ya sasa ni ya CCM kwani hata watangazaji wake wameshakuwa empty kimitazamo
 
Back
Top Bottom