Ushauri: Upinzani ushughulike vipi na Lipumba

Ushauri: Upinzani ushughulike vipi na Lipumba

Achana nao basi. Mnawafanya hao Cuf wajinga kumbe ukweli ni, inawauma wanavyotumiwa na Ccm. Kwa ufupi, mnataka muwatumie nyie.
NCCR au CHADEMA hawaItumii CUF bali wanashirikiana nao dhidi ya CCM kwa kuwa malengo yao yanafanana. CUF inataka kuiondoa CCM na NCCR na CHADEMA pia. CCM inapotaka kushirikiana na Lipumba lengo ni lao ni kufanya nini?
 
NCCR au CHADEMA hawaItumii CUF bali wanashirikiana nao dhidi ya CCM kwa kuwa malengo yao yanafanana. CUF inataka kuiondoa CCM na NCCR na CHADEMA pia. CCM inapotaka kushirikiana na Lipumba lengo ni lao ni kufanya nini?
Kwahiyo unaposhikia bango huo ushirikiano wa kuing'oa Ccm swali langu kuhusu Mtatiro somehow hukuliona eh??
 
Kwahiyo unaposhikia bango huo ushirikiano wa kuing'oa Ccm swali langu kuhusu Mtatiro somehow hukuliona eh??
Nimeliona. Anatropia Theonest keshalitolea maelezo mara kadhaa. Kwa maelezo yake na kwa vielelezo vya Tume yeye alishajitoa kugombea lakini tume ilikataa kujitoa kwake. Lakini Lubuva alipoulizwa akasema kama Anatropia angeshinda asingeapishwa kwa kuwa alishaandika barua ya kujitoa, lakini cha ajabu kura zake zilitambuliwa na kumnyima ushindi Mtatiro.
 
izzo CHADEMA wamegundua CCM inalitumia Jeshi la Polisi kupambana na wananchi wasio hatia na mwisho wa siku wanadai wapinzani hupambana na Serikali wakati ukweli wa mambo ni CCM ndiyo inapambana na wapinzani wake kwa kutumia Jeshi la Polisi.
Ndugu unajua kuwa wanasiasa na wananchi wa Africa hawajui hata maana,mifumo na taratibu za kupata democrasia ya kweli so hatujui tunadai nini lakini tunakidai tu
Democrasia ya ukweli mpaka kutimia ni lazima vitu 12 vitekelezwe lakini wazungu wenyewe pamoja na kuona wana demo kubwa wanatekeleza v2 4 tu wakat waafrica tunatekeleza kimoja 2 ambacho ni uchaguz tu
Siasa ni sayansi na nature ya sayansi ni uwezo wake wa kubadili chochote kutoka chuma mpaka uji chadema wameshndwa kutumia wasomi kupanga mikakati ya kufanya siasa za sayansi wamebak kufanya siasa za kiki kama wasanii
Ni vzr kutumia akili ulizopewa bure na Mungu kuliko kutumia nguvu ambazo zitakugharimu kuzpata
 
Rais Mkapa wazr wa fedha mzee wa mtakula nyasi IGP Mahita mzee wa ngunguli CDF Mboma utatokea wapi waulize wapemba na wanabuguruni ndio wanajua Mkapa vzr si hawa wapaka inna wa ufipa sidhani kama list hyo hapo juu Lissu pamoja na wenzie wangeleta ujinga wao wa mahakamani na mitaani

Ndio maana nawambiaga chadema nyinyi ni soft sana kujilinganisha na Cuf na Lipumba kwa mala ya kwanza Tanzania ilitoa wakimbizi wakati nchi aina vita leo lissu anatoka jela then hapo hapo mahakamani anatukana then mnasema hakuna democrasia then unakwenda kulala kwako mpaka asubui

Ok...!! Mboma alikuwa CDF na Mahita alikuwa IGP.

Wakimbizi walienda Mombasa kulikuwa hakuna blah! blah!

Wanzanzibar wanamkumbuka Mkapa hadi leo.
 
Nguvu za kiume au za kisiasa?kama za kisiasa cuf walikuwa wapo serikalini huko zanzibari 2010-2015,chadema walikuwa wana nguvu gani hapo
Kwahyo nguvu ni kupewa uongozi wa nchi yenye watu ambao hawafiki hata nusu ya wanachama wa chadema ama???? Yaani majority ya bungeni na kura za urais na halmshauri plus wanachama hao cuf walikuwa wanawakutia wapi chadema???? Kwa ufupi chadema inawahitaji cuf sababu ya kura za zenji na kura za pwani huo ndio ukweli wenyewe ila bara kwenye wapiga kura 80% sijui geita sijui mpanda huko cuf ipo kweli embu tuwe wakweli muda mwingine basi
 
Kwahyo nguvu ni kupewa uongozi wa nchi yenye watu ambao hawafiki hata nusu ya wanachama wa chadema ama???? Yaani majority ya bungeni na kura za urais na halmshauri plus wanachama hao cuf walikuwa wanawakutia wapi chadema???? Kwa ufupi chadema inawahitaji cuf sababu ya kura za zenji na kura za pwani huo ndio ukweli wenyewe ila bara kwenye wapiga kura 80% sijui geita sijui mpanda huko cuf ipo kweli embu tuwe wakweli muda mwingine basi
Vizuri umekiri kwamba chadema ni chama cha upande fulani,na mnatamani kafu ife ile mpate watu zanzibar na pwani
 
mbowr yupo kwenye 'chama chetu mbadala'..ambacho wakati cuf ipo juu tulijitahid kukibeba hata kwa media ili cuf cha waswahili kipotee..hivyo tukajitahid sana kuipora majimbo cuf kuwavunja nguvu wafuasi
Duh unaingiza udini tena mkuu!!! Kwamba chadema ilibebwa kisa ni ya wakristo??? Yaani cuf iliyopewa mpaka wizara kibao za serikali 2010-15 haijabebwa kisa udini ila chadema ndio imebebwa kidini duuuh kazi ipo!!!!
 
Lipumba hakuwahi kujenga chama chake nyumbani kwake anakotokea.

Hana hata kiti kimoja cha Ubunge nyumbani kwao Tabora.
Kama nyumbani kwao peke yake hawamkubali iweje watu wa maeneo mengine wamkubali,?

Lipumba angekua na busara angesubiri uchaguzi ndani chama chake ukifika achukue Form za kugombea uenyekiti kwa kuwa alikua ameshajiuzulu na kubakia kama mwanachama wa kawaida.
Well said
 
Vizuri umekiri kwamba chadema ni chama cha upande fulani,na mnatamani kafu ife ile mpate watu zanzibar na pwani
Duh sasa udini unaingiaje hapa mkuu!!! Kwani kujijenga zanzibar na bara kunauhusiano na dini?? Mbona ccm zenji inafutika kwani haina waislan ccm ya zenji???? Au mbona cuf ina nguvu pwani kwani ina maana ccm haina waislam wa kutosha ???? Acha udini mkuu siku cuf ikifa bara ndio ujue pwani itaendelea kuwa ya ccm sasa nani anataka tufikie hivo?? Unafkiri dar tungeshinda chadema bila nguvu ya cuf??? Udini haukusaidii mkuu dar 70% ni waislam ila madiwani wengi wametokea chadema unachokiita chama cha wakristo

Shame on u
 
Duh unaingiza udini tena mkuu!!! Kwamba chadema ilibebwa kisa ni ya wakristo??? Yaani cuf iliyopewa mpaka wizara kibao za serikali 2010-15 haijabebwa kisa udini ila chadema ndio imebebwa kidini duuuh kazi ipo!!!!
hivi kwa nini cuf haikupendwa na vyombo vya habari kama ipendwavyo chadema!?..kuhusu uwaziri,rejea usemi wa lisilo budi hutendwa
 
Duh sasa udini unaingiaje hapa mkuu!!! Kwani kujijenga zanzibar na bara kunauhusiano na dini?? Mbona ccm zenji inafutika kwani haina waislan ccm ya zenji???? Au mbona cuf ina nguvu pwani kwani ina maana ccm haina waislam wa kutosha ???? Acha udini mkuu siku cuf ikifa bara ndio ujue pwani itaendelea kuwa ya ccm sasa nani anataka tufikie hivo?? Unafkiri dar tungeshinda chadema bila nguvu ya cuf??? Udini haukusaidii mkuu dar 70% ni waislam ila madiwani wengi wametokea chadema unachokiita chama cha wakristo

Shame on u
Mbona sijataja udini mie?hebu nisome tena mkuu sana
 
Ndugu siwez kukubishia coz ur junior nataka kukwambia mission ya chama chochote cha siasa ni kuongoza serikali for ur info Cuf tayali wameshatumia magari ya STK na ving'ora Zanzbar hayo ni mafanikio makubwa sana ya kisiasa kumbuka mafanikio hayo na Lipumba ameshiriki pia unatakiwa kujua kuna watu walikufa na wengine kukimbia nchi ktk harakat za kisiasa hasa CUF lipumba ni mwanasiasa aliyepata misukosuko ya serikali kuliko wanasiasa wote Tanganyika leo ingekuwa miaka ile ya 2000-2005 unadhani Lissu angeleta ujinga kwa Mkapa? acheni kuongea tu enz ya upinzani wa Cuf ulikuwj ni hatari sana kuliko leo chadema
Nimecheka sana uliposema Mbowe mpinzani duniani hakuna mpinzani mfanyabiashara na Africa hakuna mpinzani ambae ajaonja mahabusu au vipigo vya police
Kwahyo hamad rashid na yule mwenyekiti wa UPDP nao vyama vyao vimepaa sababu tu wapo serikali ya ccm pia act na tlp nao ni vyama vikubwa kisa tu mrema na mghwira wanapigiwa ving'ora 😀😀 😀😀 yaani we jamaa bhana unanchekesha sana

Mbowe keshalala selo sana mkuu hadi aliwahi hukumiwa kifungo mwaka 2015 kabla hajakata rufaa na kushinda kma ni virungu kule mwanza alikula virungu sana tu mwaka 2010 alipoenda kampeni za wenje!!!! Kaporwa jengo, katajwa list ya wauza madawa kipi bado hajafanyiwa uamini ni mpinzani kweli???

Unasema lisu asingemuweza mkapa unasahau alipokuwa mwanasheria wa LEAT alikuwa anapambana na nani??😀😀 .Hivi alichaniwa shati tarime na kulala selo hulo nyamongo hadi akakimbilia trip ya uingereza Rais alikuwa nani??? Alipokuwa akikamatwa kisa uchochezi kwenye kipindi cha pambanua enzi hizo za 2003 rais alikuwa nani??? We bhana acha utani na lisu kuwa serious kabisa

Haya unasema cuf ilikuwa imara kuliko chadema mbona hawakuwahi fikisha hata wabunge watatu bara nzima 😀😀..... mboma waliposakiziwa kuwa ni chama cha kiislam kilijifia kabisa hasa bara walipojaa makafiri😀😀😀....... uzuri wa mbowe ni consistency yaank nccr na cuf vilikuwa vyama vikubwa ila kwa msimu vikapotezwa na ccm ila chadema wameishindwa labda ife kwa makosa ya viongozi wa chadema wenyewe sio sababu ya hila na njama za ccm na wwe unajua hilo

Long live mbowe long live maalim long live UKAWA
 
hivi kwa nini cuf haikupendwa na vyombo vya habari kama ipendwavyo chadema!?..kuhusu uwaziri,rejea usemi wa lisilo budi hutendwa
Mkuu cuf kilihit enzi ambazo mass media haikuwa imekuwa kma ssa ndio maana ila chadema imehit 2005-15 muda ambao itandawazi ulishakuwa mkubwa sana hivo tu ila hayo ya udini hayana maana kabisa
 
Lowasa mlituambia fisadi akawapa pesa mkaufyata mkamtangaza mtakatifu kwenye Vita ya ufisadi hamna mchango wa maana
Kwahyo hyo pesa tuliohongwa mbona takukuru haijafungua kesi au ni uongo mnaposema rais wenu ni mchukia rushwa?????

Hivi kwa hali ilivyokuwa 2015 nani alimuhitaji mwenzie zaidi??? Mpaka ahonge??? Hivi kweli lowasa alihitaji kuhonga ili agombee urais?? Mbona dr mihogo na chuki zote kwa lowasa hakuwahi sema alimhonga mbowe???
 
Mkuu cuf kilihit enzi ambazo mass media haikuwa imekuwa kma ssa ndio maana ila chadema imehit 2005-15 muda ambao itandawazi ulishakuwa mkubwa sana hivo tu ila hayo ya udini hayana maana kabisa
ulikuwa na umri gani wakati vyama vingi vimerudi!?chadema ilihit 2005!!?na cuf ilikuaje hiyo 2005!? kuwa mkweli kwa nafsi yako..
 
ulikuwa na umri gani wakati vyama vingi vimerudi!?chadema ilihit 2005!!?na cuf ilikuaje hiyo 2005!? kuwa mkweli kwa nafsi yako..
Since kina zitto waingie bungeni plus wangwe na mdee na slaa waliipaisha sana chadema kwa hoja zao murua ingawa walikuwa wachache sana na 2005 ndio uchaguzi wa mwisho cuf kuwa na nguvu bara hasa baada ya mahita kuuaminisha umma kuwa cuf ni chama cha magaidi, waislam wa siasa kali na hivyo kupelekea umaarufu wao kushuka hasa bara kulikojaa makafiri kwank nadanganya??? Na toka hapo bara nzima ikahamia kwa chadema na ndio maana nkasema 2005-15 hivyo sijui unataka kukataa nni mkuu
 
Back
Top Bottom