Ushauri: Upinzani ushughulike vipi na Lipumba

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,301
33,920
Kihistoria Lipumba hakuwahi kuwa mwanasiasa bali alikuwa anatumiwa na chama cha siasa kufanikisha malengo yake ya kisiasa. Lakini kwa bahati mbaya sana chama kilichokuwa kinamtumia kwa mambo ya siasa kilidharau kumshughulikia kisiasa pale alipoonekana mwaka 2015 anataka kutumiwa kisiasa na CCM.

Leo Lipumba ni kikwazo kikubwa sana ndani ya CUF si kwa sababu ana nguvu za kisiasa (hajawahi kuwa nazo) bali ni kutokana na mwendelezo wake wa kutumika kisiasa dhidi ya CUF.Kwenye uchaguzi wa 2010 Lipumba alitumika kisiasa dhidi ya CHADEMA na kwa maneno yake mwenyewe ilikuwa ni "kuokoa jahazi lisizame". Leo ni zamu ya Lipumba kutumiwa na CCM dhidi ya CHADEMA.

Lakini la kujiuliza ni kwa nini siku zote hizo CUF walivumilia Lipumba kutumiwa kisiasa na CCM dhidi ya vyama vingine pinzani kwa CCM? Tangu Uchaguzi wa mwaka 1995 Lipumba alikuwa anapambana kugawa kura za wapinzani dhidi ya CCM. Inavoonekana Lipumba ana "kazi maalum" ya kuhahakikisha kwamba kura za wapinzani wa CCM haziunganiki kwa hali ama njia yoyote ile.

Ushauri wangu kwa vyama vya Upinzani hasa chama cha CUF na CHADEMA ambavyo ndiyo vinalengwa na CCM, kwa sasa vibadili mbinu za kupambana na Lipumba. Watendaji wa Serikali wanaomuunga mkono Lipumba hawafanyi hivyo kwa kuwa wanaamini kwamba Lipumba yuko sahihi, bali wanafanya hivo kwa kuwa hawana kingine cha kufanya kubakia kwenye ajira zao.

Kwanza kuwe na Mkakati wa pamoja tena yakinifu wa kupambana na wanaomtumia Lipumba na wanaosaidia CCM kumtumia Lipumba. Lipumba anapowafukuza wabunge anaamini kwamba CUF haitashinda uchaguzi ukirudiwa na CCM ndilo walitakalo. Lazima UKAWA wawe wamoja bila ya hivyo watapigwa!
 
Hahahahahaha hv ukisema mwanasiasa jabari aliyebaki wa upinzani Tanganyika Lipumba ni number moja rudi maktaba kapekue ni mwanasiasa gani aliyeanzisha vuguvugu la kisiasa ambalo Dr Slaa alikuja kucopy na chadema kutake over 2010 - 2015 chini ya katibu mkuu Dr Slaa cjuh kama nafasi ya Dr slaa chadema walishaijaza? au bado ipo wazi

Hakuna mwanasiasa Tanganyika aliyefikia record ya Lipumba kuanzia kisiasa na kiharakati za kisiasa
 
huo ukawa unahusiana vipi na mambo ya ndan ya chama???haya ya cuf chadema yanawahusu nn?? Mzee haji duni alisema kule chadema kila mtu kambale

Sent using Jamii Forums mobile app
Sababu walisign MoU kati ya vyama washiriki wa UKAWA!!! Hivyo lazma matters zenye kuhudu uhai wa vyama ushughulikiwe pia na vyama washirika

Ndo maana hta wakati wa kampeni lipumba alipowatelekeza CUF mbona hulalamiki chadema walivyowashika mkono hadi cuf wakachanua bara kwa majimbo ya rekodi!!!
 
Aendelee kuzigawa tu hizo kura, maana hata mkiungana hakuna la maana mnalolifanya zaidi ya matamko na maandamano yasiyotekelezeka.
 
Kwanini haya mambo ya alikua anatumika hamuyaongelei toka mwanzo had I mambo yakishaharibika ndio mnajitokeza kuyasema???
 
Hahahahahaha hv ukisema mwanasiasa jabari aliyebaki wa upinzani Tanganyika Lipumba ni number moja rudi maktaba kapekue ni mwanasiasa gani aliyeanzisha vuguvugu la kisiasa ambalo Dr Slaa alikuja kucopy na chadema kutake over 2010 - 2015 chini ya katibu mkuu Dr Slaa cjuh kama nafasi ya Dr slaa chadema walishaijaza? au bado ipo wazi

Hakuna mwanasiasa Tanganyika aliyefikia record ya Lipumba kuanzia kisiasa na kiharakati za kisiasa
Acha ushabiki wa kitoto hivi ukiweka track record ya mbowe na huyo lipumba mafanikio ya mbowe ndani ya miaka kumi utalinganisha na mafanikio ya uongozi wa lipumba unaofikia miaka 20 soon?????

Kwa ufupi licha ya madhaifu alionayo ila kiongozi imara zaid katika historia ya upinzani ni mbowe na dr slaa na seif ila hao kina lipumba hana cha maana alichofanya no wonder miaka 15 ya utawala wake walishindwa fikidha hata majimbo 5 bara nzima
 
Kwanini haya mambo ya alikua anatumika hamuyaongelei toka mwanzo had I mambo yakishaharibika ndio mnajitokeza kuyasema???
Anaweza kuwa hajatumika kwa miaka 18 ila kwenye huu mgogoro obviously anatumika..... huwezi sema unarudi kuokoa chama chako kisife afu ukarudi kwa nguvu je kama aliombwa kwanni asingesubiri uchaguzi ili apite kwa kishindo??

Hivi kma unakipenda chama chako ndio kuna haja gani Ya kutimua wabunge na viongozi mbalimbali wakubwa wakati ukijua unaua chama???? Kma kweli anakpenda chama na anaona kurudi kwake kunaleta madhara kwanni asisepe tu mapema??? Yaani unaona kuna mgogoro afu hupishi tu??
 
Ushauri wangu kwa vyama vya Upinzani hasa chama cha CUF na CHADEMA ambavyo ndiyo vinalengwa na CCM, kwa sasa vibadili mbinu za kupambana na Lipumba. Watendeji wa Serikali wanaomuunga mkono Lipumba hawafanyi hivyo kwa kuwa wanaamini kwamba Lipumba yuko sahihi, bali wanafanya hivo kwa kuwa hawana cha kingine cha kufanya kubakia kwenye kazi zao.
Badala ya kupanga mbinu kupambana na ccm,manapanga kumalizana wenyewe kwa wenyewe.Tukisema upinzani Tanzania ni wababaishaji mnakuja juu
 
Badala ya kupanga mbinu kupambana na ccm,manapanga kumalizana wenyewe kwa wenyewe.Tukisema upinzani Tanzania ni wababaishaji mnakuja juu
Sisi siyo Mungiki kwa ivo huwezi kusema tunamalizana wenyewe kwa wenyewe!
 
Badala ya kupanga mbinu kupambana na ccm,manapanga kumalizana wenyewe kwa wenyewe.Tukisema upinzani Tanzania ni wababaishaji mnakuja juu

Mkuu sisi tunazungumzia vyama vya siasa vya kiraia na sio kikundi cha kijeshi. Umewahi kuona ccm inajenga hoja za kisiasa zaidi ya kutumia jeshi kujibu hoja? Ccm ni chama cha kijeshi na sio chama cha siasa.
 
Back
Top Bottom