John Gregory
JF-Expert Member
- Jul 14, 2019
- 1,060
- 1,957
- Thread starter
- #141
Baada ya mimi kukataa katu katu na kumtelekeza ndipo wazazi wakanihoji sababu haswa ni zipi,Baada ya kuwaelezea kwa kuwaonyesha ushahidi ndipo walipotaka kumhusisha huyo mchepuko ambaye niwe tu muwazi,Tangu nidukue mawasiliano yao (maana hata baada ya kumrejesha kwao hakugundua kuwa bado nafuatilia) niligundua kuwa tangu agundue ni mjamzito hakuwa na mawasiliano naye ya karibu wala hakuwahi kumjulisha habari za ujauzito.Kwa kifupi kati ya wote anaowasiliana nao hakuna hata mmoja aliyemweleza habari za ujauzito isipokuwa mimi (Kwa mujibu wa dukuzi).Kuhusu kuonekana dhaifu napenda tu utambue kuwa mtoto ndiye anayenifanya nionekane hivyo kutokana na kwamba,Hapa tuwe wawazi tu kuwa damu ni nzito kuliko maji,Endapo ikatokea mtoto kweli akawa wangu,Je italeta picha gani kwa mtoto hapo baadae? Hilo tu ndilo linanipa ukakasi.Mkuu ngoja nimsaidie jamaa.....kwamba wazazi walimlazimisha? mwenyewe binti yupo tayari kuishi bila wewe, ila wazazi wake ndio wanahofia atazeekea nyumbani......
Pia jamaa anakushangaa, kwamba unajisifia huyo jamaa amekupigia simu, eti kukwambia alitumia kinga, ni kwamba huyo msichana wako inawezekana amempanga jamaa aruke asilimia 100 ila ndio mhusika,
pia msichana wako anakujua huna uanaume ndani yako ndio maana akapata huo ujasiri, wa kumpanga hawara yake akupigie...
Pia jamaa ameshangaa ujasiri wa huyo jamaa na msichana wako unatoka wapi, yan wanapeana namba kukupigia na tena waanze kusema walitumia kinga kweli mkuu? ..... kwamba you are of no harm to them really??....
kama mwanaume, kuna ujinga huwezi kusikiliza kama kiteteo pia huwezi kupigiwa simu na jamaa ukamsikiliza huo ujinga, man you are too good for that cheap drama ya huyo msichana asie na adabu