Mwanzoni mwa mwaka huu, kaka yangu mpedwa kafugwa jela miaka 30 kwa kosa ambalo si vyema kuliweka wazi hapa jamvini.
Kaka alikuwa anauwezo kiasi fulani lakini kesi na muda aliokaa mahabusu ulimaliza pesa zake sana. Baada ya kuwa amehukumiwa ameiacha familia yake katika mazingira magumu. Nilicho fanya ni kumpa uwezo mke wake kaka yangu ambaye ana watoto naye 3.
Pamoja na yote nimekuwa natoa matumizi ya shule kwa watoto zangu. Ili mpaka hapo mama yao atakapo kuwa amesiama vyema nipunguze support.
Sasa kibembe ambacho kimenitokea jioni ya leo hii ndio hasa dhumuni la kuomba ushauri nifanyaje. Shemeji ameniambia anashukuru kwa kumjali na kujali familia yake. ila simtimizii haja zote kwa hiyo nani ampatie. Anamaanisha mambo yetu yalee, jamani simuelewi.
Kuna mawili, mruhusu agegedwe nje, au kama una ka-wivu, chukua wewe, lakini ukumbuke kuwa uhusiano wako na kaka yako utaishia hapo, kwa sababu lazima atakuja kubaini.Sijamjibu kitu, nimepiga kimya tu.
\Mkuu hapo naamini wewe una mchumba mtarajiwa na una matarajio ya kuwa na familia yako
kaka yako tayari ana watoto watatu na huyo mwanamke na sidhani kwa hali ilivyo ungependa wewe uingie kwa mke wa kaka yako au uendeleze familia ya kaka yako ila ungependa zaidi wewe uoe na uwe na familia yako
Heshimu mipaka yako kama mdogo wa kaka yako na shemeji kwa huyo mama
Kama una msimamo na mpango wa kuanzisha familia yako heshimu hilo na mwambie wazi kabisa natoa msaada kama mdogo mtu na kwa ajili ya watoto wa kaka yangu na kuhakikisha wewe unasimama kuweza kuisimamia familia yako na baada ya hapo ni lazima wewe kama wewe usimamie familia yako
Msaada unaotoa ni kwake kuweza kusimama na sio kutaka wewe uchukue nafasi ya kaka yako
Imagine may be kaka yako akatoka kwa msahama wa rais na akukute wewe umechukua nafasi yake na umelala na mke wake ni nini kitampata au hata wakati unaenda kumtembelea uende na mke wake tumbo hilo au ana mtoto wa nne na anaambiwa wazi ni wa mdogo wako huoni kuwa litamuumiza sana kaka yako
japo sheria ya ndoa inaryuhusu mwanamke kuolewa iwapo mume atafungwa kifungo kirefu sana usiruhusuliwe kwako labda useme huna tena mpango wa kuoa na utaichukulia familia ya kaka yako kama yako na kumchukua huyo mwanamke kuwa mke wako
Mkuu bado mambo ya kurithishana yanaendelea
Swali muhimu wewe je umeoa kwanza au bado halafu ushauri ufuate
\Mkuu hapo naamini wewe una mchumba mtarajiwa na una matarajio ya kuwa na familia yako
kaka yako tayari ana watoto watatu na huyo mwanamke na sidhani kwa hali ilivyo ungependa wewe uingie kwa mke wa kaka yako au uendeleze familia ya kaka yako ila ungependa zaidi wewe uoe na uwe na familia yako
Heshimu mipaka yako kama mdogo wa kaka yako na shemeji kwa huyo mama
Kama una msimamo na mpango wa kuanzisha familia yako heshimu hilo na mwambie wazi kabisa natoa msaada kama mdogo mtu na kwa ajili ya watoto wa kaka yangu na kuhakikisha wewe unasimama kuweza kuisimamia familia yako na baada ya hapo ni lazima wewe kama wewe usimamie familia yako
Msaada unaotoa ni kwake kuweza kusimama na sio kutaka wewe uchukue nafasi ya kaka yako
Imagine may be kaka yako akatoka kwa msahama wa rais na akukute wewe umechukua nafasi yake na umelala na mke wake ni nini kitampata au hata wakati unaenda kumtembelea uende na mke wake tumbo hilo au ana mtoto wa nne na anaambiwa wazi ni wa mdogo wako huoni kuwa litamuumiza sana kaka yako
japo sheria ya ndoa inaryuhusu mwanamke kuolewa iwapo mume atafungwa kifungo kirefu sana usiruhusuliwe kwako labda useme huna tena mpango wa kuoa na utaichukulia familia ya kaka yako kama yako na kumchukua huyo mwanamke kuwa mke wako