Nina rafiki yangu ambaye urafiki wetu una muda mrefu kidogo na amenizoea sana amekuwa akiniomba ushauri kwa lolote yuko huru nami namuona kama mtu wangu wa karibu sanaa. Kuna mtu aliwahi kuniambia kuwa huyo rafiki yako anajihusisha na mapenzi na watu wa jinsia yake, mimi sikuamini nikajua ni umbea tu wa watu nikapuuzia ila cha kushangaza juzi yeye mwenyewe kaniambia.
Akasema una kifua! Kuna kitu nataka nikwambie nikasema sema chochote usiwe na shaka akaniambia dada yangu unajua kuwa mimi ni shoga dahh nikapatwa na mshangao kwanza nilijua ananitania ila akasema huo ndio ukweli ila akasema kwa sasa ana miezi mitatu hajafanya mchezo huo na akaniomba mie nimsaidie ili aache tabia hiyo eti ataiacha kabisa endapo nitakuwa upande wake na ukimuona huwezi jua kama anafanya huo mchezo jinsi alivyo ni tofauti sana na matendo yake nimsaidiaje best yangu huyu.