Ushauri: Polisi na wananchi tupewe fair ground

Kaa la Moto

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
7,903
1,053
Nimeangalia TV na picha mbali mbali hapa JF na nimegundua katika purukushani ya Polisi na wananchi waliokuwa wakiandamana kwa amani Arusha, polisi walikuwa na zana za kivita wakati hakuna wananchi waliokuwa na kitu chochote cha kumdhuru mtu. Hii ilikuwa sio fair ground.
Naishauri serikali iwambie wananchi siku nyingine wakitaka kufanya maandamano waje wamevalia kijeshi tayari kwa ajili ya kukabiliana. Wawe na siraha za kila aina hata kama ni za kijadi na waingie kwenye ligi wote wakijua sasa kila mtu anamwinda mwenziwe.
Haya ya sasa ambayo polisi wanafanya kuwapiga watu wasio na siraha kwa siraha mbalimbali sio sawa. Nashauri next time kukiwa na maandamano watu wabebe kila wanachoweza ili hata wanapopigwa na ijulikane kuwa walikuwa na intention ya kupigana. Ni ujinga uliotukuka kumpiga mtu ambaye hana nia ya kupigana.
 
Back
Top Bottom