tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 26,025
- 25,432
Umoufia kwenu!
Wakuu nina shida ya kifedha na nimekwama kabisa kupata fedha kutoka vyanzo vingine ingawa nina uhakika 101% kwamba mchepuko wangu ana uwezo wa kunikopesha kiasi cha fedha (Tsh 900,000) ninachihitaji kumlipia mwanangu karo ya shule. Kama mjuavyo shule zitafunguliwa jumatatu hii ya tarehe 29/04/2019 na mzazi ambaye hajalipa ada mtoto wake hatachukuliwa na basi ya shule.
Lakini kila nikifikiria kumu-approach mchepuko huyu roho inakataa. Unajua mazoea yana taabu sana. Mimi siku zote nimekuwa nikijionyesha kutokuwa na shida ya pesa, hasa linapokuja suala la matumizi kwa ajili ya mchepuko wangu. Mchepuko ni mhasibu mwandamizi katika benki moja maarufu hapa Dar wakati mimi ni mwalimu wa shule ya sekondari katika Wilaya ya Kinondoni. Nina uhakika kuwa uwezo wa kunikopesha hata 1M leo anao, lakini nitaanzaje?
Kuna wakati nahisi kuomba fedha kwa mchepuko ni ishara ya UDHAIFU au kwamba anaweza kuniacha….kwa kudhani kuwa mimi sina manufaa yoyote kwake in future. Kwa kweli nipo njia panda. Najiuliza: Akikataa kunipa hizo fedha kisha akalala mbele, ina maana nitakuwa nimekosa vyote….chekeli na mbunye. Nami siko tayari kumkosa mwanamke huyu kwa gharama yoyote ile.
Swali jengine najiuliza: Je, nione aibu kuomba fedha dogo ashindwe kuhudhuria masomo hadi nikipata fedha from another source? Naona nitakuwa sijamtendea haki dogo kwa kumkosesha masomo. Sasa nifanyeje?
Naomba ushauri wenu katika hili maana niko njia panda. Sitaki kumpoteza mchepuko wala sitaki dogo akose masomo kwa uzembe wangu. Mnanishaurije?
Wakuu nina shida ya kifedha na nimekwama kabisa kupata fedha kutoka vyanzo vingine ingawa nina uhakika 101% kwamba mchepuko wangu ana uwezo wa kunikopesha kiasi cha fedha (Tsh 900,000) ninachihitaji kumlipia mwanangu karo ya shule. Kama mjuavyo shule zitafunguliwa jumatatu hii ya tarehe 29/04/2019 na mzazi ambaye hajalipa ada mtoto wake hatachukuliwa na basi ya shule.
Lakini kila nikifikiria kumu-approach mchepuko huyu roho inakataa. Unajua mazoea yana taabu sana. Mimi siku zote nimekuwa nikijionyesha kutokuwa na shida ya pesa, hasa linapokuja suala la matumizi kwa ajili ya mchepuko wangu. Mchepuko ni mhasibu mwandamizi katika benki moja maarufu hapa Dar wakati mimi ni mwalimu wa shule ya sekondari katika Wilaya ya Kinondoni. Nina uhakika kuwa uwezo wa kunikopesha hata 1M leo anao, lakini nitaanzaje?
Kuna wakati nahisi kuomba fedha kwa mchepuko ni ishara ya UDHAIFU au kwamba anaweza kuniacha….kwa kudhani kuwa mimi sina manufaa yoyote kwake in future. Kwa kweli nipo njia panda. Najiuliza: Akikataa kunipa hizo fedha kisha akalala mbele, ina maana nitakuwa nimekosa vyote….chekeli na mbunye. Nami siko tayari kumkosa mwanamke huyu kwa gharama yoyote ile.
Swali jengine najiuliza: Je, nione aibu kuomba fedha dogo ashindwe kuhudhuria masomo hadi nikipata fedha from another source? Naona nitakuwa sijamtendea haki dogo kwa kumkosesha masomo. Sasa nifanyeje?
Naomba ushauri wenu katika hili maana niko njia panda. Sitaki kumpoteza mchepuko wala sitaki dogo akose masomo kwa uzembe wangu. Mnanishaurije?