Ushauri: Nina Tsh. Milioni 11 nataka kujenga

Ushauri: Nina Tsh. Milioni 11 nataka kujenga

Kagera utajenga na kuezeka na Milango utabakiza madirisha na finishing

11.Koko 2cubic 80,000

12.Cement 20 bags x 18000 = 360,000
Mkuu yani nyumba unaijenga mpaka finishi na madirisha alafu itumie mifuko 20 ya cement?
 
Mkuu yani nyumba unaijenga mpaka finishi na madirisha alafu itumie mifuko 20 ya cement?
Kujenga boma tu mifuko 20 na kule kagera vijijini wanajenga kwa kutumia udongo msingi wa mawe wanajenga na udongo juu ya msingi Wana weka mortar ya cement na mchanga kusawazisha au zege la nondo juu ya msingi wa mawe.
Na tofali ndogo za kuchoma wanajenga kwa kutumia udongo saruji inatumika katika msingi juu na katika Linta tu kwenye finishing sikuongelea.
 
Hiyo hela ni nyingi. Itakusogeza na utafika pazuri hata kama utakuwa hujamaliza. Anza sasa. Mie bado niko kwenye msingi. Najeng nyumba nimejipa miaka minne iwe imekwisha. Kwa mwaka huu natamani msingi (wa ghorofa) uwe umekamilika.
 
Hiyo hela ni nyingi. Itakusogeza na utafika pazuri hata kama utakuwa hujamaliza. Anza sasa. Mie bado niko kwenye msingi. Najeng nyumba nimejipa miaka minne iwe imekwisha. Kwa mwaka huu natamani msingi (wa ghorofa) uwe umekamilika.
 
Dah! Kwa ubishi huo hapo juu ndio maana mtu anaamua kufia kwenye nyumba za kupanga aisee
 
Asante,,lengo langu ni kupandisha boma na kuliezeka

Asant mkuuu,lengo langu ni kupandisha boma na kuliezeka kuweka milango na madirisha grills kwanza mambo ya vioo baadae
Kama mayoral unayo, itafanya mpaka kwenye bati
 
Wakuu sas naenda kasi sana na kaujenzi nilikowaambia,kumbe! Nyumba tunaziogopa bure!! Nkimaliza ntaileta nyumba muione wakuu
 
Nimeichukua ramani yako bila malipo mkuu asante maana kipindi naleta thread ya nia ya kujenga hata ramani nlkw cna kweli jf ni msaada,nmemuonesha wife hyo ramani kaifurahia xaxa tumeanza ujenzi
Kai_edit kwa mtaalam (mchora ramani) aingize majina yako (i.e aweke particulars) zako kabla hujaipeleka ofisi za mpango mji kupewa kibali.View attachment Ramani PDF.pdf
 

Attachments

Asante,,lengo langu ni kupandisha boma na kuliezeka

Asant mkuuu,lengo langu ni kupandisha boma na kuliezeka kuweka milango na madirisha grills kwanza mambo ya vioo baadae
Iñàwezekana kwa kupàndisha ña kupaua
 
Kagera utajenga na kuezeka na Milango utabakiza madirisha na finishing

1.Tofali za kuchoma 10,000 x 50 = 500,000

2.Bati 80 x 24,000 = 1,920,000

3.Mbao 2/4 - 100 pcs x 2500 - 250,000

4.Mbao 2/2 - 50 pcs x 1200 - 60,000

5. Misumari mbao 50kgs 200,000

6. Misumari bati kg 25 150,000

7. Nondo 12mm 15 x 24000 =360'000

8.Binding wire kg 3 x 5000 15000

9.Ring 8mm 45 pcs x 2000 45,000

10. Mawe Trip 5 x 70,000 350,000

11.Koko 2cubic 80,000

12.Cement 20 bags x 18000 = 360,000

13. Mchanga 2 Trips 70,000 = 140,000

14.Mengineyo 750,000

15.Milango na frem 8x200,000 =1,600,000
Bro tofari za kuchoma kwa idadi ulotaja hapo juu ni ndogo mno kulingana na ukubwa wa nyumba!

Pia mifuko ya saruji 20 bags haitoshi otherwise uniambie atajenga boma kwa tope then bim na nguzo ziwe!

Mabati ongeza idadi at least zifike 110 na bei yake inategemea ni bati ya aina gani na yenye ujazo UPI

Vitu vingi hapo ume under estimates!
 
Back
Top Bottom