Iko hivi
Hapo kuna mambo mengi kwa pamoja
1. Makuzi ni ufahamu unaji tunekukutengeneza wewe ujaye...ni katika kipindi hiki ndio mambo mengi huibuka kwa pamoja kama kutaka mafanikio au matokeo ya haraka, kukata tamaa hasira kujiona unakosea kujistukia kuwa hufai na unadhauliwa nk ....kikubwa hapa ni kujitahidi kufocus kwenye mazuri na kuyapiga chini yale mabaya...sio kazi rahisi lakini kwa kufanya hivyo unajitengenezea uwezo wa kuja kuwa na maamuzi binafsi yenye tija
2. Matatizo ya kisaikoloji...inferiority complex na superiority complex...hizi hali mbili hujitengeneza katika umri wa 17- 25 (crucial period ya maamuzi magumu)
Hapa ukikosea tu kidogo aidha utakuwa na tatizo la inferiority complex...kujidharau na kujikataa na kuona wengine ndio wanaweza. Hapa utakuwa ni mtu ambaye hujiamini na kujistukia...Ama la utapata tatizo la superiority complex, kwamba wewe ni bora sana kuliko wengine...hii itakutesa pia kwakuwa utataka kuwa juu ya wengine na watu wakikushanga utajikuta unaumia kihisia na kupata shida sana. ..jijenge kuwa mtu wa kutafakari kabla ya kutenda lolote
Watu wengi wanaojiamini sana mbele ya hadhira, ni watu wenye maumivu mengi moyoni kwakuwa wana mapungufu ya woga kujikataa na kujidharau, hivyo huficha hizo hali kwa kujijiengea ukuta mnene wa kujiamini ukorofi ubabe ujuaji nk...lakini nikwambie kitu huwa wakitoka hapo huumia sana..na hupenda kuwapa wengine maumivu ili wao wapate nafuu
Jaribu kufanya hili unapokumbana na hizo hali vuta pumzi ndefu tatu kisha tulia na kama una maji kunywa utaona maajabu