Ushauri: Nimpe zawadi gani mke wangu?

Ushauri: Nimpe zawadi gani mke wangu?

chifu77

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2014
Posts
902
Reaction score
597
Heshima kwenu wanajamvi. Mimi nimeoa na tumejaliwa kupata watoto 2. Mke wangu nimwaminifu, sijawahi kuona dalili zozote za kunisaliti; kwa kifupi hajawahi kuchepuka. Pia ana bidii sana katika kulea watoto wetu na ananitia moyo pale tunapopita ktk changamoto za kimapato au kijamii. huwa namshukuru kwa kuwa mke mwema na mama mzuri kwangu mimi na kwa watoto we2. TAKRIBAN mwezi sasa nafikiria nimpe zawadi gani? Ila bado sijapata jibu kwa sababu siwezi kumudu kitu kikubwa kama gari. NAOMBENI ushauri mwanamke wa aina hii anastahili zawadi gani?
 
Mpende, mthamini, uwe muaminifu na kumjali. Mnunulie maua na chocolate na umwambie jinsi gani unamshukuru Mungu kwa kukupa mke mzuri in every sense kama yeye. Muahidi uaminifu na upendo wako siku zote za maisha yako. Huu ni ushauri toka kwa MWANAMKE
 
Mpende, mthamini, uwe muaminifu na kumjali. Mnunulie maua na chocolate na umwambie jinsi gani unamshukuru Mungu kwa kukupa mke mzuri in every sense kama yeye. Muahidi uaminifu na upendo wako siku zote za maisha yako. Huu ni ushauri toka kwa MWANAMKE
Nitazingatia haya maana najisikia nina deni kubwa kwake.
 
Kwanza hongera [emoji122][emoji122][emoji122],pili wewe ndo unamfahamu mkeo vizuri na utakua unajua anapenda kitu gani au kitu gani huwa anatamani kuwa nacho...mnunulie kitu anachopenda...au una budget ya bei gani tukusaidie zawadi kumchagulia.
Nimekuwa nikitenga pesa kidogo kidogo mpaka sasa nina laki 1 na elfu 70. Ndo nimezitenga kwa ajili ya zawadi
 
Back
Top Bottom