Ushauri: Nimemfumania na mwanamke ndani kwake

Ushauri: Nimemfumania na mwanamke ndani kwake

Pole sana rafiki" najua ni maumivu makali!!! Usijali mungu yupo pamoja na ww" malipo yake yapo hapahapa duniani.
 
Hili ni gumu sana,pole sana mdada,sioni mustakabali mwema na huyu mtu,he is selfish and ungrateful.he is not worthy your love and pains let go of him.
 
Shetani alimpitia?
Huyu shetani siku akiibuka huko alipo, patachimbika sana hapa duniani maana kila kitu shetani alinipita. Na haya majibu aliyoyatoa ni shetani ndo alimwambia aseme hivyo?

Dada uchumba tu unalia, je kwenye ndoa itakuwaje, now anamsingizia shetani sijui baadae atamsingizia nani, kifupi huyu sio mwaminifu so sio mwanaume wa kuolewa nae, utalia kila siku, hakufai but changanya na za kwako haya ni mawazo yangu

Pamoja na hayo alichojibu baada ya kumtaka kumfaham aliyenae ni hiki,
1. Huna haja ya kufaham marafiki zangu ulishajulikan kwa ndugu zangu basi.
2. Huyu nlianza nae mahusiano kabla yako
3. Nina uwezo wa kuwa hata na wanawake 10 ni maisha yangu.


Naumia sana wandugu sijui la kufanya, ameomba msamaha kuwa ni shetan tu kampitia. Nishaurini ndugu zangu nifanye nn na maumivu haya makali nliyonayo.

Asanteni.
 
Wee utakuwa mwanamke mzuri sana wa kuoa atiii. Hebu ona hizi mambo;
  1. Una hela za kumtunza (una mzidi mshahara mara 3),
  2. Unakuta meseji za wapenzi unatulia,
  3. Unapigiwa simu kuna mwanamke ndani unaomba ruhusa ya kwenda,
  4. Unamkuta na mtu ndani na maneno machafu juu bado hujajua cha kuamua,
  5. Unaonekana una dalili za kurudi tena akija kupiga goti vizuri!!!
Asee hebu njoo huku kwangu buanaa....wee ndo wa kuoa atii
 
Fikiria future itakuaje hapo, atazaa nao kwa kisingizio hicho hicho halafu ndo hataachana nao kabisa kwa kuwa watakuwa wazazi wenzie.

Anakujibu hovyo kwa sababu anajua huna kwa kwenda na unampenda sana. Ushauri wangu ni huu, huyo mjinga hana dudu ya dhahabu ukae unagombania na wanawake wenzio, hakusaidii kwa lolote tena inawezekana anataka akushikilie coz una hela zako so hatahitaji kukuhudumia na hela zake ni za matanuzi na vimada huku anaendelea kukumega.

Mi nina ndugu wa kiume wanaotambulisha watu kibao na mwisho harusi surprise mtu mwingine kabisa. Dada hayo yapo yamekuta wengi wewe sio wa kwanza. Jipe moyo, huyo mtu tupa kule yupo anayestahili mapenzi yako ya kweli. Kama unaamini Mungu sali tu, tubu kwa kwenda kwa akili zako mwenyewe muombe akuondolee uchungu.

Men never change hasa baada ya kukupata. You deserve better dear, yeye nani akuumize hivyo.
 
Wee utakuwa mwanamke mzuri sana wa kuoa atiii. Hebu ona hizi mambo;
  1. Una hela za kumtunza (una mzidi mshahara mara 3),
  2. Unakuta meseji za wapenzi unatulia,
  3. Unapigiwa simu kuna mwanamke ndani unaomba ruhusa ya kwenda,
  4. Unamkuta na mtu ndani na maneno machafu juu bado hujajua cha kuamua,
  5. Unaonekana una dalili za kurudi tena akija kupiga goti vizuri!!!
Asee hebu njoo huku kwangu buanaa....wee ndo wa kuoa atii
Mh! na wewe nawe ndio mambo gani ya kumshauri mwenzio
 
Mkuu ikiwa wewe kweli hujawahi kushiriki tendo hilo basi uwe wa kwanza kumtupia jiwe huyo binti.... Unajua kila jambo linawakati wake?? Huu siyo wakati wa kumshambulia kwa kushirikiana ngono na yule kijana muhuni.... Hata malaya wanaojiuza wakienda kupimwa na kukutwa nao huwahawashambuliwi.... Wanapewa nasaa kawaida tu... Anza na familia yako... Then wakiacha kufanya ngono kabla ya ndoa hamia mitandaoni sasa

Every case should be judged on its own merits.Kosa la mwingine halihalalishi kosa lako.Wote ni wezi uyu Katoty na huyo anayemwita mpenzi wa zamani wa mtarajiwa wake huyo,Ninachoona hapa ni mwizi kutaka asiibiwe na mwizi mwezie.Ila kizuri ninachokiona hapa mleta mada anasema alimfumania na mpenzi wa zamani hivyo nothing much to worry ila kitu kingine tunachoweza ku-note hapa huyu si mpenzi wa zamani kama bado wanaendelea ni bora Katoty ukamwita uyo mdada mpenzi mtangulizi wa mtarajiwa wako kwani wanafanya mapenzi hadi leo.Kikubwa Katoty kaa na uyu mtarajiwa wako mujadili the way forward kwani yalotokea yameshatokea ili mufikie maamuzi/uamuzi wa pamoja kwa mustakabali wa maisha yenu ya baadae.
 
Aliye kataza sex kabla ya ndoa sio mimi au familia yangu, ni Mungu, ukiwa unataka kumrushia mawe Mungu, we mrushie yeye sio mimi, si unaona vipi wewe kichaa.


Afu kwenye familia yangu, si unajua Babu yangu aliowa wake wanne, sijui kama hakuna wanamna hio lakini nikija wakuta. Ujuwe Al shabab hafai kitu, watajuta kuzaliwa.
Shekh mbona mkali???? Ni kweli ni hairuhusiwi kugegedana kabla ya ndoa ila ni ngumu sana kuishi bila hiyo kitu... Mahusiano hayatafika popote... Dada zetu hawa wanamambo mengi sana.. Usipomgegeda wewe wenzio watamgegeda tu... Hilo ndo tatizo haswaaaaa... Kwanza sisi tunaambiwa yeyeto akimtazama mwanamke kwa kumtamani tu kishazini naye... Kwa mustakabali huo basi wanaume wote vijana kwa wazee uzinifu ni dhambi yetu ya asili coz kwa siku unaweza kuwatamani hata wanawake 10 tofauti....

Halafu tukirudi upande wenu nyinyi mnafundishwa siyo kufanya tu.. Bali msiikaribie zinaaa kabisahhh...!!!! Kwa mantiki hiyo basi kuangalia pono... Phonesexing... Kuzungumzia mambo haya ya uzinifu tayari tunadhambi machoni pa mwenyezi Mungu... Narudia tena.. Kila mtu hapa ni mchafu.. Aliye msafi basi amtupie huyu mwali jiwe...
 
Pole mdogo wangu.
Mi nakushauri umsamehe, ila sasa ujue huyo shetani aliempitia ni sehemu ya familia yenu. Kwa hiyo usiumie tena, delete maumivu kabisaa..

Si amesema alikuwa nao 4 kabla hako? Huyo ni mmoja wao? Muombe kwa kumbembeleza akukutanishe na hao 3 waliokutangulia ili hata ukikutana nao uwape heshima yao. Hao ndo waliomcoach mpenzio hadi akafikia kiwango cha L.Messi. Wape heshima zao na wakitaka kupima kiwango alichonacho sasa waruhusu tu ili wajue bado ana pumzi.

Harusi ni lini? Utushirikishe tuchangie na kama utahitaji matron na patron, mimi na paw tuko tayari. Tutajigharamia nguo na pia tutawasindikiza fungate kwa gaharama zetu

Mnh! KATOTY hapa inabidi ukae chini na kuutafakari kwa makini ushauri huu. Natumaini utaupata vizuri ujumbe uliomo na kuchukua hatua stahiki. Pole lakini.
 
Last edited by a moderator:
Every case should be judged on its own merits.Kosa la mwingine halihalalishi kosa lako.Wote ni wezi uyu Katoty na huyo anayemwita mpenzi wa zamani wa mtarajiwa wake huyo,Ninachoona hapa ni mwizi kutaka asiibiwe na mwizi mwezie.Ila kizuri ninachokiona hapa mleta mada anasema alimfumania na mpenzi wa zamani hivyo nothing much to worry ila kitu kingine tunachoweza ku-note hapa huyu si mpenzi wa zamani kama bado wanaendelea ni bora Katoty ukamwita uyo mdada mpenzi mtangulizi wa mtarajiwa wako kwani wanafanya mapenzi hadi leo.Kikubwa Katoty kaa na uyu mtarajiwa wako mujadili the way forward kwani yalotokea yameshatokea ili mufikie maamuzi/uamuzi wa pamoja kwa mustakabali wa maisha yenu ya baadae.

Mkuu nimependa hiyo point kwamba wote ni wezi ila mwizi wa mwanzo anaona kama ndo mmiliki halali...

Tukija ktk ushauri wako pia naona nu wazo zuri wakiyazungumza.. Ila tatizo ni... Huyo jamaa hatoweza kuvumilia kuwa na mwanamke mmoja.. Lazima atawagegeda wengine.. Sasa yote ya nini hayo ujicommit ktk matatizo wakati upenyo upo..

Mungu ananjia nyingi sana za kumfunua mnafiki kutoka ktk kichaka cha dhambi.. Ningekuwa ni mimi ndiyo yamenikuta haya ningepiga magoti na kumshukuru Mungu kwa aliyonionyesha... Yakitokea ktk ndoa haya yanamaumivi mujarabu sana...
 
Shekh mbona mkali???? Ni kweli ni hairuhusiwi kugegedana kabla ya ndoa ila ni ngumu sana kuishi bila hiyo kitu... Mahusiano hayatafika popote... Dada zetu hawa wanamambo mengi sana.. Usipomgegeda wewe wenzio watamgegeda tu... Hilo ndo tatizo haswaaaaa... Kwanza sisi tunaambiwa yeyeto akimtazama mwanamke kwa kumtamani tu kishazini naye... Kwa mustakabali huo basi wanaume wote vijana kwa wazee uzinifu ni dhambi yetu ya asili coz kwa siku unaweza kuwatamani hata wanawake 10 tofauti....

Halafu tukirudi upande wenu nyinyi mnafundishwa siyo kufanya tu.. Bali msiikaribie zinaaa kabisahhh...!!!! Kwa mantiki hiyo basi kuangalia pono... Phonesexing... Kuzungumzia mambo haya ya uzinifu tayari tunadhambi machoni pa mwenyezi Mungu... Narudia tena.. Kila mtu hapa ni mchafu.. Aliye msafi basi amtupie huyu mwali jiwe...
Umeongea point nzuri sana.

Narudia tu kwenye kale ka point ulikosema mimi Shekhe, mimi ni kama wewe si shekhe. Kuwa shekhe si kazi ndogo, mimi najizuia tu kuzini nje ya ndoa, wewe nadhani hujiziwi hio ndio tofouti yetu.
 
Pole mdogo wangu.
Mi nakushauri umsamehe, ila sasa ujue huyo shetani aliempitia ni sehemu ya familia yenu. Kwa hiyo usiumie tena, delete maumivu kabisaa..

Si amesema alikuwa nao 4 kabla hako? Huyo ni mmoja wao? Muombe kwa kumbembeleza akukutanishe na hao 3 waliokutangulia ili hata ukikutana nao uwape heshima yao. Hao ndo waliomcoach mpenzio hadi akafikia kiwango cha L.Messi. Wape heshima zao na wakitaka kupima kiwango alichonacho sasa waruhusu tu ili wajue bado ana pumzi.

Harusi ni lini? Utushirikishe tuchangie na kama utahitaji matron na patron, mimi na paw tuko tayari. Tutajigharamia nguo na pia tutawasindikiza fungate kwa gaharama zetu
Huu ushauri wako inaonyesha unahasira ila umeweza ku control hizo hasira ndo ukatoa ushauri kama huu. mwenye akili ataelewa unamaanisha nini
 
huyo atakusumbua mbele ya safari na wahenga wanasema kuvuja kwa pakacha..........kwa huo mwenendo wake utaletewa wake wenzio hadi chumbani kwako kwa mtazamo wangu mtupilie mbali huyo maana si muaminifu
 
Pole sana dada yangu, thats what LOVE is, hakuna mahausiano ya kimapenzi hapa duniani yasiyokuwa na changamoto, hayo yaliyokukuta ndio changamoto zenyewe na sio jambo la busara kwa msomi kama wewe kushindwa kukabiliana na hizo changamoto tena ni ndogo sana wakati kuna mambo makubwa zaidi ya hao ambayo yanawakuta watu na wanayapatia ufumbuzi.

Usione watu wameweza kuishi maisha ya ndoa au kukaa kwenye mahusiano kwa muda mrefu na mpaka sasa wanaishi maisha yenye furaha na penzi lao lina afya tele ukafiriki ni kazi rahisi ndio imewafikisha hapo, walipatwa na majaribu kibao kuliko hata ya kwako na wamefanikiwa kuyashinda na sasa wanaenjoy maisha.

Kama kwenye fikra zako utajenga slogan ya KUACHA basi wewe tambua kuwa mapenzi yamekushinda, utaachana na John, kesho utaanza na Maiko utakuta ana tabia ya ushoga then utaachana naye, unaanza tena na Joel sio malaya wala shoga ila analala bar, mamboyatakuw magumu kwako itabidi umwache kwa sababu mind set yako imetawaliwa na KUACHA, utajaribu na Shamsi ambapo ndugu zake ni watu masimango, wenye chuki na roho mbaya ukichanganya na umbea uliokithiri, kwa sababu sio mtu wa kuvumilia itabidi uachane naye.

Hakuna uhusiano ulio perfect, hivyo nakushauri kama umempenda huyo mpenzi wako basi ni jukumu lako wewe kumbadilisha hizo tabia zake, kitendo cha yeye kugawa penzi nje ina maana kuna kitu anakosa kwako hivyo kaa tafakari kiundani zaidi wapi umekosea na ufanye nini ili umteke mpenzi wako asione umuhimu wa kwenda nje, hili suala la kusema eti ni tabia yake sugu mimi binsfi nalipinga kwani ni kauli ya wakata tamaa waliokubuhu
 
Bidada pole sana,huyo haonekan kuwa na mapenzi ya dhati kwako ila anafanya kukupotezea muda tuu ukiona haeleweki we achane naye "a right person will just come"
 
Pole sana kweli huyo Masikini jeuri.

1. Hivi hukumuelewa wakati mnaanza mahusiano kuwa historia yake tayari alikuwa na wanawake wa 3?
2. Hukumuuliza tatizo lilikuwa nini mpaka anaachana na hao wanawake japo angejitetea na kuonekana hana makosa?
3. Hukufikiria kuwa wewe unaingia kama wa 4 kwenye history kwa mujibu wake japo inaonyesha wewe hata hukuwa wa 4 inawezekana hata 15?
Haya ujiulize tu mwenyewe mie nakushauri achana nae coz hana msaada kwako zaidi ya salamu za Morning, g9t na kula tunda lako bure tu.
 
Back
Top Bottom