WATU WALIOCHANGIA HAWAJAKUPA UKWELI NGOJA MIMI NIKUPE UKWELI.
NI hivi Tangu lini Mjukuu akarithi Mali ya Babu? Huo utaratibu umeanza lini?
Mama yako mzazi ndiye mwenye haki ya kurithi na Kama alishafariki KABLA hajarithishwa Mali Basi wewe sahau kurithishwa Mali kwa mgongo wa mama yako!!!
Na Kama unadai ulirithishwa Hilo Shamba na Babu yako lazima uwe na ushahidi wa maandishi au wa mdomo na Kama NI ushahidi wa mdomo lazima uwe na mashahidi zaidi ya wanna Kati yao wawepo Ndugu wa karibu na wengine wasio ndugu.
Je unao ushahidi wowote wa maandishi au wa mdomo kuwa Babu yako alikupa Hilo Shamba lotelote?Kana unao kafungue kesi mahakamani na Kama huna Hama haraka Sana kwenye Hilo eneo.
Unadai uliliendeleza Hilo eneo tangu ukiwa mdogo. NI SAWA uliliendeleza na ilikuwa NI jukumu lako kwa kuwa ulikuwa unatunzwa na Babu yako, Unakula,KULALA na kusomeshwa bure Sasa Kwanini na wewe usisaidie kazi za nyumbani? Ulitaka uwe Unakula bure,Kusomeshwa bure na KULALA bure na wewe usishiriki kazi za happy nyumbani kwa Babu yako?
Pia kuliendeleza eneo lisilo lako bado litabaki kuwa siyo lako hata Kama ungejenga ghorofa!!! Bado eneo Hilo litabaki kwa mwenye eneo tu!! Wewe ulipanda miti kwenye Shamba la Babu yako bado Hilo Shamba NI la Babu yako na akifa watarithi Watoto wa Babu yako we huna kitu hapo!! Vinginvyo uwe alikupa mbele ya mashahidi tofauti na happy eneo siyo lako ondoka haraka na kesi hiyo huwezi kushinda.
Cha msingi umwangukie mjomba wako akupe miti kidogo uvune na wewe ukaanze Maisha yako sehemu nyingine. Huo Ndiyo ukweli ninaokupa maana wachangiaji wengi WANAISHIA KUKUAMBIA time et ACHANA nao hawakwambii wewe huna haki pale, Kama huna ushahidi wa kurithishwa Hilo eneo WEWE HUNA HAKI, HUNA CHAKO PALE NA HIVYO HAMA HARAKA SANA
MTUMAI CHA NDUGU HUFA MASIKINI.