Ushauri na ombi kwa Wizara ya Ulinzi na Usalama

GIRITA

JF-Expert Member
Jul 4, 2016
4,128
5,236
Asalam aleykum wanajamii.

Moja kwa moja kwenye lengo nchi yetu pendwa ni moja kati ya nchi zinazompa Uhuru RAIA wake kuabudu dini yeyote aipendayo kikatiba.

Leo najikita zaidi kuiomba serikali na wizara husika kuwapa uhuru wa kuabudu watumishi wake.

Hapa nasimama kutoa hoja hii kama itafaa basi ifanyiwe kazi na vyombo husika, watumishi wa vyombo vya ulinzi na usalama, askari polisi, askari wa jeshi la wananchi, jeshi la zima moto, uhamiaji na jeshi la kujenga taifa.

Haya ni majeshi yanayoajiri watu wa dini zote hapa nchini na kuwapa uhuru wao wa kufanya ibada lakini kumekuwa na unyimwaji wa uhuru wa mavazi kwa waumini wa dini ya kiislamu hasa kwa waajiriwa wa kike.

Kwa mujibu wa dini ya kiislamu mwanamke anatakiwa kujistiri mwili wake popote alipo, sasa hapa kwetu mambo ni tofauti kidogo hakuna mavazi au sare katika majeshi yetu yanayompa uhuru mwajiriwa husika wa kike kujistiri.

Hivyo nashauri Wizara husika ziangalie uwezekano wa sare za kujihifadhi kwa hawa dada zetu wa kiislamu wapate angalau uwezekano wa kuficha nywele zao na mavazi yao yawe ya stara hata kama ni suruali basi ziwastiri kwa mujibu wa dini na imani yao.

Tunaweza kuangalia mifano kwa nchi zilizowapa uhuru wanawake wa kiislamu kujistiri wakiwa katika majukumu yao ya kijeshi, kwa kuwa nchi yetu haina dini basi haiwezi kuwa tatizo.

Kuna wakina dada wengi wanatamani kujiunga na majeshi yetu lakini wanaogopa kwenda kinyume na maamrisho kimavazi, zibuniwe sare ambazo zitawapa stara wakina dada wa kiislamu katika majeshi yetu ya ulinzi na usalama.

Huu ni ushauri na maoni yangu sijaleta malalamiko hapa.

Mungu ibariki Tanzania. Mungu ibariki Afrika. Mungu mbariki Rais wetu Dk. John Pombe Magufuli.
IMG_20191208_165226.jpg
IMG_20191208_165303.jpg
IMG_20191208_165344.jpg
IMG_20191208_165226.jpg
IMG_20191208_165303.jpg
IMG_20191208_165344.jpg
IMG_20191208_165226.jpg
IMG_20191208_165226.jpg
IMG_20191208_165344.jpg
 
Mkuu mtu anaamua kwenda kule akiwa mtu mzima.Anajua anachokifanya anajua anachoamua hii ni pamoja na kutambua description ya kazi anayotaman akaajiriwe nayo. (Utaratb wa mavazi,ratiba za kazi na aina ya majukum atakayo kwemda kuyatumikia)

Katika utu uzima wake huu mtu kama ni muislam au dini nyingine yoyote anakua anayafaham haya yote hivyo uchaguzi unabaki kwake kukubaliana nayo au kutokubaliana.Kukubali kuajiliwa maana yake unakubaliana na taratibu za kazi na miongozo yake.

Huwez kuingia ndani ya ajira halaf ndio uanze utaratibu wa kuomba miongozo ya kazi ibadilike.Ni ngumu.
Kwa niaba ya wizara, naomba taratibu ziachwe kama zilivyo wala zisibadikishwe jwa maslahi ya watu wachache pasipo kujal dini jinsia au tamaduni zao.

NB
1. Ukitaka kuruka ,agana na nyonga.
2. Maji ukiyavulia nguo,sharti uyaoge
3. Mtaka cha uvunguni, shart ainame.

Ongezea nyingine.....
.....
.....
 
Hapana mkuu,kwa nini kusiwepo na haki kwa wafuasi Wa dini zote tukizingatia maamrisho ya dini zao kwa mujibu Wa katiba.
Angalia Siku za mapumziko ya kazi ni siku za kuabudu kwa imani mojawapo kwa nini na hawa wasipate Uhuru wa kujistiri wakiwa kazini.
Japo kuwa ni watu wazima wanachagua kuingia huko lakini si vibaya ombi hili linafanyiwa kazi kuwapa fursa wale wanaoshindwa kuingia huko kwa kuhofia stara.
 
kalidegree,
Hizo habar za haki na usawa wakizitaka wakae huku uraian ambako na sisi na ww tupo.ww unawaza kuabud na kujistil i kwasababu kuna watu wameamua kuyatoa maisha yao ili ww uishi hivyo.
Waache watumikie nchi yao usiwasemee vitu ambavyo wao hawajavisema.

Kule kuna watu wanaojua dini hata kukuzid ww na pepon wataingia pengine hawa kukutabgukia ww.Hayo ni mambo yao na Mungu wao.Ndio mana wameamua kutulizana
 
AsajizzleDaGreat,
Mkuu huo ni mtazamo wako,hayo majeshi yenyewe yanawapa Uhuru wa kuabudu na kufuata imani uitakayo,sasa hili swala ni dogo sana kurekebisha unatetea upande wako kwa sababu hali hii ya sasa inakubeba.
 
Mkuu huo ni mtazamo wako,hayo majeshi yenyewe yanawapa Uhuru wa kuabudu na kufuata imani uitakayo,sasa hili swala ni dogo sana kurekebisha unatetea upande wako kwa sababu hali hii ya sasa inakubeba.
Appologies but huna input ya maana kwenye hili.
Ni pumba tu
 
Ukiona hapaendani na misingi ya dini na wewe ni kweli mshika dini achana napo!
Kazi zipo nyingi ... ... ...
Dini si kivazi tu..
 
Hayo unayoyataka hayatakaa yapelekwe kwenye hivyo vyombo ulivyotaja Na pia sio lazima wakaajiriwe huko. Kama wanaona hakuwafai wafanye kazi idara zingine! Kama haikuwezekana wakati wa Mzee Mwinyi basi sahau kwa nyakati nyingine!
 
Zaidi ya pumba, wakianza kuleta udini jeshini unategemea nini? Kuna watu muda wote wanawaza dini tu!
Let us abide na rules na regulation za kazi.
Miongozo ya kazi iachwe ifanye kazi vinginevyo tutazua tafran ambazo hazina mashiko
 
Zaidi ya pumba, wakianza kuleta udini jeshini unategemea nini? Kuna watu muda wote wanawaza dini tu!
Nani alete udini wewe kuwa muelewa basi,mbona mashuleni mabinti Wa kiislamu wanavaa hijab kwa sasa lakini miaka ya nyuma haikuruhusiwa baada ya wanaharakati kulisemea serikali ikawa sikivu.
 
Let us abide na rules na regulation za kazi.
Miongozo ya kazi iachwe ifanye kazi vinginevyo tutazua tafran ambazo hazina mashiko
Hamna tafrani yeyote hapo sijui wewe ni MTU Wa namna gani bro ,rejea swala LA hijab mashuleni.
 
Back
Top Bottom