Ushauri: Mume wa mtu niliyezaa naye watoto watatu amefariki na ameacha mali nyingi, nifanyaje kudai haki za wanangu pasipo Mume wangu kujua?

Huna chako hapo mamaa ungemkazia mapema kabla hajadedi akupe cha watoto mapema ili kuepuka shida huko Mbele!
 
Malaya unatafutaje ushauri kwa watu wastaarabu. Nani ukushauri kwa uchafu wako. Gunia za mkaa zinakuhusu wewe. Wanaume kazi ipo, yani watoto 3 nje ya ndoa.
 
Ndoa yangu ina miaka 12 mimi na mume wangu hatuna shida, kabla ya mume wangu kuna mwanaume nilikua naye, alikua ni mume wa mtu, nilibeba mimba yake nilipomuambia akaikataa,

Kwakuwa kupindi hicho ndiyo nilikua nimeanza mahusiano na mume wangu nilibambikizia mimba na akanioa. Baada ya kuolewa yule Baba alirudi akaomba msamaha na kusema yuko tayari kuhudumia mwanae hata kama atatumia jina la mume wangu.

Basi nilimkubalia na tangu kipindi hicho alikua anahudumia mwanae kwa kila kitu. Kwakua alikua ananijali na kipato chake ni kikubwa basi nilijikuta narudiana naye, nikabeba mimba yake ya pili, nilimuambia mume wangu ni yake naye akawa anahudumia ila bado yule baba aleindelea kujali wanae mopaka kuwasomesha.

Mume wangu kipato ni cha kawaida ila mimi nafanya kazi pia, anajua nchukua mikopo kwaajili ya ada lakini ukweli Baba yao ndiyo anawasomesha. Niliamua kumazalia mume wangu mtoto mmoja ambaye ndiyo mwanangu wa tatu, lakini mtoto wangu wa nne ni wa yule Baba.

Baadhi ya ndugu zake alishawatambulisha na wanajua watoto ni wao kwani nilishawapeleka kwa dada yao. Mwaka jana alianza kuumwa na mwezi huu mwanzoni alifariki dunia. Nilienda kwenye msiba kama watu wengine.

Sababu ya kuja kwako ni hivi, Baba wa wanangu kaacha mtoto mmoja tu na mke wake, lakini ana mali nyingi sana, ana nyumba 9, magari ya mizigo zaidi ya kumi na vitu vingi.

Nimefuatilia na kugundua kuwa hakuacha wosia, ina maana mali zake nyingi zimebaki kwa mwanae aliyezaa na mke wake kwani ndugu nao wana mali zao hawahaangaiki naye. Natamani kwenda kudai haki za wanangu kwani kwakua dada yao ananifahamu na anawafgahamu watoto wa kaka yake naamini nitapata.

Hofu yangu ni kama huyo mke wake atakataa na kusema hanitambui, nahofia kama ikiwa kwenda Mahakamani labda mume wangu atajua. Kusema kweli nimechanganyikiwa, ndoa naitaka lakini nikiwaza haki za wanangu natamani kwenda hata mahakamani.

Mimi ndiyo napaswa kupata kikubwa kwani nimemzalia watoto wa 3 wakati mke wake ana mmoja tu!
Yani hii story umeiba kwa Iddi Makengo au ww ndo Idd mwenyewe.
 
Back
Top Bottom