Ushauri mie nipo njia panda

Ushauri mie nipo njia panda

Dena Amsi

R I P
Joined
Aug 17, 2010
Posts
13,080
Reaction score
4,275
Nieleweke ni ndugu yangu 'Damu' mtoto wa Baba Mkubwa.

Kamaliza form four mwaka 2010 kafail alipata ziro na 'D' moja tu, 2011 akareseat ndo kavurunda kabisa, 2012 nikamwambia njoo huku nchi jirani nilipo mie akaja akaanza kusoma Diploma ya HR kaharibu mbaya semister ya kwanza kachemsha na vitabia fulani sio vizuri.

Nikamrudisha home nikamwambia chagua usome nini he jibu nililopata nusu nizimie 'Dada mie kusoma siwezi' nikasema wataka nini sasa. Ngoja nifikirie mie haya he kaenda kwa Mdingi wangu ambaye ni Mdogo kwa Baba yake kawashiwa moto hatari kwa ujinga wake na ushauri wa kipumbavu wa marafiki katoroka akaenda kuishi hostel na rafiki anayesoma CBE.

Jana nimekwenda mahali kula kiti ya moto mara namuona kabeba tray anakuja kunihudumia mie mdomo wazi. Namuuliza hii ndo kazi uliyotaka kufanya ama?? Anaanza kulia eti dada nisamehe nimekosa pesa ya kula imebidi nifanye hii kazi nisaidie.

Mwenzenu mate yalinikauka, maneno yalipotea sikujibu hata neno moja kiti ya moto yenyewe ilikuja nikafunga hata apetite yote iliyeyuka.

Naomba ushauri wenu nifanyeje
 
Basi kama ashakuambia awezi kusoma bora ukamsikilza kuliko kumpeleka tena shule na wewe ukawa unaharibu hela yako ya bure,kizuri amekua mkweli kuwa awezi kusoma.
Kama wataka kumsaidia tena kaa naye chini then muulize nikitu gani tofauti ma shule angependa kufanya ambacho anaona kinaweza kumsidia yeye.
Jibu atakalokupa basi na wewe jaribu kuangalia je nikweli linaweza kumsaidia kimaisha but mshauri asikate tamaa tu!!
 
Huyo sasa........inabidi umuulize yeye binafsi anataka kufanya nini........vinginevyo unaweza kumchinja hadharani.........

Yaani nakwambia 100000 Kshs sio mchezo na wakakataa kurudisha ada yaani natamani kumnyonya macho
 
kuna kazi ambayo wanaipenda sana hawa wasiopenda kusoma. si nyingine bali ni kushona.mpeleke huko kwenye cherehani labda ataweza.
 
Basi kama ashakuambia awezi kusoma bora ukamsikilza kuliko kumpeleka tena shule na wewe ukawa unaharibu hela yako ya bure,kizuri amekua mkweli kuwa awezi kusoma.
Kama wataka kumsaidia tena kaa naye chini then muulize nikitu gani tofauti ma shule angependa kufanya ambacho anaona kinaweza kumsidia yeye.
Jibu atakalokupa basi na wewe jaribu kuangalia je nikweli linaweza kumsaidia kimaisha but mshauri asikate tamaa tu!!

Nilishamuuliza hajanipa jibu namkuta anauza baa mweehh majanga
 
kuna kazi ambayo wanaipenda sana hawa wasiopenda kusoma. si nyingine bali ni kushona.mpeleke huko kwenye cherehani labda ataweza.

Shida hajanipa jibu anataka kufanya nini naona aibu sana ndugu yangu kuuza baa na uwezo wa kumsomesha ninao
 
kuna kazi ambayo wanaipenda sana hawa wasiopenda kusoma. si nyingine bali ni kushona.mpeleke huko kwenye cherehani labda ataweza.

kabisa, amnunulie tu vyerehani vyake. au hata akawe kinyozi pia itamfaa.
 
Nieleweke ni ndugu yangu 'Damu' mtoto wa Baba Mkubwa.

Kamaliza form four mwaka 2010 kafail alipata ziro na 'D' moja tu, 2011 akareseat ndo kavurunda kabisa, 2012 nikamwambia njoo huku nchi jirani nilipo mie akaja akaanza kusoma Diploma ya HR kaharibu mbaya semister ya kwanza kachemsha na vitabia fulani sio vizuri.

Nikamrudisha home nikamwambia chagua usome nini he jibu nililopata nusu nizimie 'Dada mie kusoma siwezi' nikasema wataka nini sasa. Ngoja nifikirie mie haya he kaenda kwa Mdingi wangu ambaye ni Mdogo kwa Baba yake kawashiwa moto hatari kwa ujinga wake na ushauri wa kipumbavu wa marafiki katoroka akaenda kuishi hostel na rafiki anayesoma CBE. Jana nimekwenda mahali kula kiti ya moto mara namuona kabeba tray anakuja kunihudumia mie mdomo wazi. Namuuliza hii ndo kazi uliyotaka kufanya ama?? Anaanza kulia eti dada nisamehe nimekosa pesa ya kula imebidi nifanye hii kazi nisaidie. Mwenzenu mate yalinikauka, maneno yalipotea sikujibu hata neno moja kiti ya moto yenyewe ilikuja nikafunga hata apetite yote iliyeyuka.

Naomba ushauri wenu NIFANYYEJE
Dada mimi naona mpe uhuru wa kuchagua afanye nini maana amerudia sana hivyo kisaikolojia imemwathiri na sidhani kama atafanya vizuri,mwite kwa upendo kabisa na upole mtoke sehemu nzuri ya kula na kunywa soda na juice mpe pole kwa kujaribu kwake na usimkasirikie baada ya hapo mwambie achague apendacho na mhakikishie kumsupport kama dada yake just show your love to her she will change drastically after all she is just your young sister so show your sister-hood(mwonyeshe upendo wa dada na si ategemee kwa viboyfriend vivalia mlegezo)
 
Shida hajanipa jibu anataka kufanya nini naona aibu sana ndugu yangu kuuza baa na uwezo wa kumsomesha ninao

sio kila mtu lazma aende shule ndio afanikiwe, kuna wengine shule zishawashinda tukubali matokeo.
 
dunia mama! chukua ndugu yako nenda naye nyumbani keshajifunza, sasa hivi ukimuuliza unataka nini atakueleza. kuna jirani yetu mmoja wakati sisi tuko wadogo alikuwa na mtoto wa kike, alichetuka hasa mpaka wazazi kumkana, akaondoka nyumbani sijui hata alienda wapi miaka kama miwili, akarejea kuomba radhi kwa wazazi wakakataa, akaenda kupata hifadhi kwa jirani nyumba ya tatu, kwenda kumwombea msamaha kwa wazazi wakakataa tena kwamba wanamfahamu vizuri hajajirudi, yule jirani akaamua kukaa naye. dada wa watu kaanza kusoma elimu ya watu wazima "taasisi", siku moja akakutana na mama yake njiani amevaa uniform!!...mama wa watu alilia sana, wakamchukua akaendelea na shule, leo hii ni mwalimu, ameolewa ana familia!!
 
Pole mwaya kwa hayo matatizo ya ndugu yako
inabidi uongee naye anataka afanye nini kwani uwezo wa kusoma naona hana
mjaribu aweze fanya biashara au shughuli yoyote njema yenye kumuingizia kipato
nahisi hapo atakuwa na maisha mazuri usimfanyie chochote mwite na ongea naye
kish a atakapolkujibu amua maamauzi atakayokwambia uwe na amani bestito
 
Shida hajanipa jibu anataka kufanya nini naona aibu sana ndugu yangu kuuza baa na uwezo wa kumsomesha ninao

kama itaonekana taabu sana kwenda shule (labda ana kichwa kizito kuzidi) mnaweza kumfungulia hata glocery, kama anapendezwa na kuuza bia! cherehani haiwezi kumsaidia kitu, ni afadhali hata akasome urembo sjui upambaji veta then mumkopeshe pesa afungue saluni!
 
Maisha ni ruti ndefu sana
dunia mama! chukua ndugu yako nenda naye nyumbani keshajifunza, sasa hivi ukimuuliza unataka nini atakueleza. kuna jirani yetu mmoja wakati sisi tuko wadogo alikuwa na mtoto wa kike, alichetuka hasa mpaka wazazi kumkana, akaondoka nyumbani sijui hata alienda wapi miaka kama miwili, akarejea kuomba radhi kwa wazazi wakakataa, akaenda kupata hifadhi kwa jirani nyumba ya tatu, kwenda kumwombea msamaha kwa wazazi wakakataa tena kwamba wanamfahamu vizuri hajajirudi, yule jirani akaamua kukaa naye. dada wa watu kaanza kusoma elimu ya watu wazima "taasisi", siku moja akakutana na mama yake njiani amevaa uniform!!...mama wa watu alilia sana, wakamchukua akaendelea na shule, leo hii ni mwalimu, ameolewa ana familia!!
 
Dada mimi naona mpe uhuru wa kuchagua afanye nini maana amerudia sana hivyo kisaikolojia imemwathiri na sidhani kama atafanya vizuri,mwite kwa upendo kabisa na upole mtoke sehemu nzuri ya kula na kunywa soda na juice mpe pole kwa kujaribu kwake na usimkasirikie baada ya hapo mwambie achague apendacho na mhakikishie kumsupport kama dada yake just show your love to her she will change drastically after all she is just your young sister so show your sister-hood(mwonyeshe upendo wa dada na si ategemee kwa viboyfriend vivalia mlegezo)

Hivo vivaa milegezo ndo shida vinamdanganya saana nasikia kulia aisee
 
Unasubiri jibu gani wakati umeshamuona anafanya kazi baa?

Mfungulieni restaurant awe anauza maana inaonekana hiyo kazi yenyewe anaiweza.
Usije ukafikiri kazi ya baa siyo kazi. Akiisimamia vizuri inalipa zaidi hata ya ajira za kuajiliwa just mfanyieni fair tu maisha yasonge.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom