afande kifimbo
JF-Expert Member
- Aug 31, 2015
- 6,254
- 2,678
DUHHuwa naingia jamii love connect kweny nyuzi za wadada wanaotafuta waume. Huwa nacheka sana siyo kwa dharau lkn najikuta nacheka kwa vigezo walivyoweka. Kuna mwingine alikuwa anaitwa kihuba vigezo vingi mwisho wa siki anatafuta mume wa kuzaa naye. Duh
Mtu anafika stage anasema anahitaji mpenzi mweny mapenzi ya dhati ha ha ha, anayejali. Shetani kuna wakati naye hujifanya mtakatifu. Upendo wa dhat hutoka moyoni mwa mtu, na huwezi kumlazimisha mtu awe na mapenzi ya dhati ila unaweza kumfanya au usimfanye mtu awe au asiwe na mapenzi ya dhati.
Ukiona wengi wanasema wanahitaji mtu mwenye upendo wa dhati, wengi wamechezea yaan walipendwa wakauchezea sasa wanakuja kutamalaki kumeshakucha. Utakuta mtu ana miaka 25 lkn anaweka vigezo utafikiri maombi ya kazi, angalau huyu wa 25, mwenye 30 huyo atajikuta ni mzee. Km ulikuwa na miaka 22-28 haujakutana naye mwenye vigezo vyako na unategemea umpate JF ni hatari sana. Ni sawa na kucheza biko au 3 mzuka.