CARDLESS
JF-Expert Member
- Apr 2, 2017
- 7,868
- 16,005
Habari za jioni wana JF. Nimuombe Mungu azidi kuwajaalieni Afya, riziki, na nguvu zaidi.
Haya twendeni kwenye mada.
Kwa wiki kadhaa sasa SA kumekuwa na wimbi la maandamano sehemu mbalimbali za miji kama JOBURG (JOZ), DEBENI (DURBAN) nk. Maandamano haya wameyaita kwa jina la OPERESHINI DUDULA.
OP hii imelenga kuleta uhuru kamili kwa wazawa, hapa wanadai kuna maeneo hata hao wazawa hawawezi kupita au kwenda au kuingia kisa WAGENI (FOREIGNERS) hasa wasio na vibali (ILLEGALLY). Pamoja na yote haya lkn wameenda mbali sana wakiwashutumu wageni hao kuwa ni WEZI, WAUAJI, NA WANAWANYIMA FURSA ZA AJIRA. Pia wazawa wanadai hata wawapo kwenye vituo vya daladala (TAX RANKS) bado hawako salama, wazamiaji wanamiliki bastola na bunduki na polisi hawafanyi kitu.
Operesheni hiyo ilipaswa kusogea mpaka HILLBROW na hapa ndipo niliposhtuka kidogo.
Mitaa hiyo imejaa Watz sana, huwezi pita hatua ishirini au 50 usisikie kiswahili, (OYAAA), mitaa hii imejaa vijana Masikini wa kitanzania, na wale madon wa SEMBE/NGADA wako kibao pia.
Sasa lengo sio hizo biashara zao, lengo ni vibali vya kuishi.
Namnukuu mmoja wa viongozi wa hiyo DUDULA "Sisi hatujali, kama watakuja kistaarabu tutakuja nao hivyo, na wakija na bunduki tutawakabili kwa bunduki."
Kauli hii inaonesha chuki kubwa juu ya wageni wakijificha kwenye kichaka cha VIBALI vya kuishi.
Kama raia wa SAUZ ana haki kisheria kukagua documents zako?? Kwann wajichukulie sheria mkononi?? Na kwanini wana deal na weusi wenzao tu??
USHAURI
Ndugu zangu WATZ mlioko huko na mnaotarajia kwenda huko, zama zimebadilika, tafuta passport yako, ingia kwa halali, muda wa kustay ukiisha rudi nchi jirani kisha inga tena utagongewa mpakani au lipia VISA uishi kwa amani angalau kidogo.
Sehemu yoyote ukienda kwa halali hata kama hauna ndugu ni rahisi kupata ndugu, tunaona hata hapa mtu kumpokea mhamiaji haramu ni mziki.
Hivyo basi nendeni mkapate passport halali na kama imeisha sogea hapo kwa Balozi wetu hapo PT.
Pia waTZ mnawawekea wenzenu maisha magumu pindi wanapopita mipakani kisa tabia zenu mbovu hasa za kuuza ngada na uhuni wa kifala.
Kama huna shule, fani, mtaji, ndugu au hata kazi maalumu usiende AFRIKA KUSINI.
Nawasilisha.
Haya twendeni kwenye mada.
Kwa wiki kadhaa sasa SA kumekuwa na wimbi la maandamano sehemu mbalimbali za miji kama JOBURG (JOZ), DEBENI (DURBAN) nk. Maandamano haya wameyaita kwa jina la OPERESHINI DUDULA.
OP hii imelenga kuleta uhuru kamili kwa wazawa, hapa wanadai kuna maeneo hata hao wazawa hawawezi kupita au kwenda au kuingia kisa WAGENI (FOREIGNERS) hasa wasio na vibali (ILLEGALLY). Pamoja na yote haya lkn wameenda mbali sana wakiwashutumu wageni hao kuwa ni WEZI, WAUAJI, NA WANAWANYIMA FURSA ZA AJIRA. Pia wazawa wanadai hata wawapo kwenye vituo vya daladala (TAX RANKS) bado hawako salama, wazamiaji wanamiliki bastola na bunduki na polisi hawafanyi kitu.
Operesheni hiyo ilipaswa kusogea mpaka HILLBROW na hapa ndipo niliposhtuka kidogo.
Mitaa hiyo imejaa Watz sana, huwezi pita hatua ishirini au 50 usisikie kiswahili, (OYAAA), mitaa hii imejaa vijana Masikini wa kitanzania, na wale madon wa SEMBE/NGADA wako kibao pia.
Sasa lengo sio hizo biashara zao, lengo ni vibali vya kuishi.
Namnukuu mmoja wa viongozi wa hiyo DUDULA "Sisi hatujali, kama watakuja kistaarabu tutakuja nao hivyo, na wakija na bunduki tutawakabili kwa bunduki."
Kauli hii inaonesha chuki kubwa juu ya wageni wakijificha kwenye kichaka cha VIBALI vya kuishi.
Kama raia wa SAUZ ana haki kisheria kukagua documents zako?? Kwann wajichukulie sheria mkononi?? Na kwanini wana deal na weusi wenzao tu??
USHAURI
Ndugu zangu WATZ mlioko huko na mnaotarajia kwenda huko, zama zimebadilika, tafuta passport yako, ingia kwa halali, muda wa kustay ukiisha rudi nchi jirani kisha inga tena utagongewa mpakani au lipia VISA uishi kwa amani angalau kidogo.
Sehemu yoyote ukienda kwa halali hata kama hauna ndugu ni rahisi kupata ndugu, tunaona hata hapa mtu kumpokea mhamiaji haramu ni mziki.
Hivyo basi nendeni mkapate passport halali na kama imeisha sogea hapo kwa Balozi wetu hapo PT.
Pia waTZ mnawawekea wenzenu maisha magumu pindi wanapopita mipakani kisa tabia zenu mbovu hasa za kuuza ngada na uhuni wa kifala.
Kama huna shule, fani, mtaji, ndugu au hata kazi maalumu usiende AFRIKA KUSINI.
Nawasilisha.