Nitakushangaa wewe unaetoka kijijini, wazazi na ndugu wote wanakutegemea wewe, nyumbani hata umeme bado haujafika, unafika chuo. Kwa kuwa tu unakutan ana wanarum wenzako wanamiliki readio kubwa, sub woofers, pamba za hatareee, na anasa nyingine, nawe ukajiona ni muda muafaka wa kujivinjari, pamoja na kwamba sio vibaya lakini mwisho wa semista vitu hivyo ni lazima uviuze kwa bei ya hasara kwa maana huna pa kuvipeleka.
Kuna tabia pia ya kusalimisha ATM kadi kwa wanadada, hili linafanywa na baadhi ya wanaume ambao ni malimbukeni. Wanawake wako kwa ajili ya huduma tu. hawana la maana la kusaidia. Mara nyingi posho ya bodi ikitoka ndio wanakomaa sana na wewe wakijua utagharamia maisha yake. yeye akaunti yake ianasoma wewe yako inashuka. Pia kumbuka nao wanakategorize kama kawaida. Utakuwepo wewe wa vocha, yupo wa starehe na yupo wa misosi. Yupo wa msalato ( Mnada wa nyama kila jumamosi) yupo wa vipodozi. Hivo mtajikuta mko wengi mnahudumia mwanamke mmoja.
Wapo wale ambao, ukinunua music, laptop au tv, wanalazimisha uwape wakae nazo wao. kwa mapenzi yako kwake ukampa akae navyo. take care brother, itakula kwa wewe.
Kwa wale wadada, Wapo wanaume wanakuhadaa watakuoa. Wakaka hao mara nyingi wanawarubuni watumishi (ma-inservice) Lengo lao ni kula mishahara yao tu na mwisho wa siku atakutema, ombea asikuache na mimba.