Ushauri kwa waliochaguliwa UDOM

Ushauri kwa waliochaguliwa UDOM

mnisaidie kwa hili,payment tunaanza kulipa trh 15 hadi 30 september,je ni hyo trh 30 sptmber tunatakiwa kuripoti?

NimekuPM, Hata hivyo ni kwamba chuo hakina uhusiano na kulipa. Tarehe 30 wao wanataka uwe umelipa lakini kufungua sio tar hiyo. Fuatilia matangazo yao kwenye website yao.
 
je vipi kuhusu sehem za kufanyia ibada.
je ni hapo hapo chuo au mpaka mtoke nje ya chuo


Waislamu wao wanafanya ndani ya chuo. Wakristo, kwa baadhi ya madhehebu wanapiga ndani ya chuo, ila si unajua wakristo walivyojigawa? Yapo madhehebu ambao huwa wanakwenda mjini. Lakini sabato wao kotekote, kwa maana mjini na chuoni.
 
kuna gym karbu na chuo au ndio mpaka town

Classic gym ni hadi mjini, ila sidhani kama wapo watu wanaokwenda huko. but local gym zipo kwa wabeba makopo ila sio rasmi sana na sijui hili kwa colleges, na pia yawezekana hata ndani ya college watu hawajui kama kuna gyms, Kwa Educatoion kwa mfano, Wapo wanaofanya mazoezi Kwenye roof ya kila Hostel na huko ndo wameweka vyuma vya kubeba.
 
Classic gym ni hadi mjini, ila sidhani kama wapo watu wanaokwenda huko. but local gym zipo kwa wabeba makopo ila sio rasmi sana na sijui hili kwa colleges, na pia yawezekana hata ndani ya college watu hawajui kama kuna gyms, Kwa Educatoion kwa mfano, Wapo wanaofanya mazoezi Kwenye roof ya kila Hostel na huko ndo wameweka vyuma vya kubeba.

Ok makole na je vp kuhusu viwanja vya mpira, kipo kimoja kwa chuo kizima au kila college na uwanja wake coz sisi ni wachezaji mashuhuri na ili masomo yawe yanapanda lazima tuwe tunapata zoez la football
 
Ok makole na je vp kuhusu viwanja vya mpira, kipo kimoja kwa chuo kizima au kila college na uwanja wake coz sisi ni wachezaji mashuhuri na ili masomo yawe yanapanda lazima tuwe tunapata zoez la football

Kila college iko full na viwanja vyake
 
thanx sana kwa kutujuza hayo,,nami naomba kujua unaweza kukaa njee ya hostel,,maana wengine tuna familia,,


kuna jamaa yangu alikuwa akisoma pale na alikuwa na mke alipanga chumba mke na mtoto wanakaa uswaz na yeye akawa anabak chuo siku moja moja analala nyumban!!
 
Nakumbuka nilipata scholarship fulani ya hela kibao huko majuu. kwa mtazamo wangu nikajua ukiacha tuition fee nyingine zote nitapewa mimi. Kwanza nilipotua New York nikachukua cab/taxi jamaa akanipeleka mitaa kibao mwisho nikafika chuo kusoma mita nikadaiwa nauli kibao baada ya wiki moja nikaanza kutembea mitaani lahaula kumbe nilichukulia taxi ni takribani kilometa moja tu kufika ninakoenda nikagundua jamaa kanikaribisha ugaibuni.

Kufika chuoni nikapewa ID kwenda bwenini nikaombwa kadi yangu kwaajili ya malipo ikachanjwa nikarudishiwa, kwenye chakula ni kadi, library card, treni kadi mwisho nikaomba hela ya kujikimu nikisingizia kwenda mjini, cinema, na vitu vidogovidogo. nikajibiwa everything is in your ID nikastuka ndio nikaambiwa itanisaidia kuwa na matumizi sahihi na kuwa nikinunua vitu ina limit kiasi siyo kununua tu kila unachokitaka. Pia nikaambia nilichopewa ni accommodation, meals, transport na stationary na si vinginevyo. Nimefurahi sana mtoa mada alivyotoa muongozo ili kusaidia ndugu zetu wanaoenda vyuoni. Natafuta facts zo UDSM niliposoma nami nitatoa msaada kama alivyofanya ndugu MAKOLE. Naongezea tu kuwa kwa wanafunzi wote waliochaguliwa kuingia vyuoni na kuhakikishiwa mkopo wa asilimia yoyote kuwa. Asilimia ya Mkopo ipo kwenye ada, na baadhi ya vitu vinginie vichache ila ya kula na kulala unapea yote. Hela unayopewa mkononi ni Meals and Accommodation Allowance tusiichanganye na hela ya nauli, dawa ya mswaki, sabuni, nguo, simu/mawasiliano, ada ya ndugu, kununua kiwanja, kujenga au kusaidia wazazi. Kupanga matumizi ni kitu cha msingi sana unapokua chuoni maana bila hivyo maisha ya chuo utayashindwa.
 
Nakumbuka nilipata scholarship fulani ya hela kibao huko majuu. kwa mtazamo wangu nikajua ukiacha tuition fee nyingine zote nitapewa mimi. Kwanza nilipotua New York nikachukua cab/taxi jamaa akanipeleka mitaa kibao mwisho nikafika chuo kusoma mita nikadaiwa nauli kibao baada ya wiki moja nikaanza kutembea mitaani lahaula kumbe nilichukulia taxi ni takribani kilometa moja tu kufika ninakoenda nikagundua jamaa kanikaribisha ugaibuni.

Kufika chuoni nikapewa ID kwenda bwenini nikaombwa kadi yangu kwaajili ya malipo ikachanjwa nikarudishiwa, kwenye chakula ni kadi, library card, treni kadi mwisho nikaomba hela ya kujikimu nikisingizia kwenda mjini, cinema, na vitu vidogovidogo. nikajibiwa everything is in your ID nikastuka ndio nikaambiwa itanisaidia kuwa na matumizi sahihi na kuwa nikinunua vitu ina limit kiasi siyo kununua tu kila unachokitaka. Pia nikaambia nilichopewa ni accommodation, meals, transport na stationary na si vinginevyo. Nimefurahi sana mtoa mada alivyotoa muongozo ili kusaidia ndugu zetu wanaoenda vyuoni. Natafuta facts zo UDSM niliposoma nami nitatoa msaada kama alivyofanya ndugu MAKOLE. Naongezea tu kuwa kwa wanafunzi wote waliochaguliwa kuingia vyuoni na kuhakikishiwa mkopo wa asilimia yoyote kuwa. Asilimia ya Mkopo ipo kwenye ada, na baadhi ya vitu vinginie vichache ila ya kula na kulala unapea yote. Hela unayopewa mkononi ni Meals and Accommodation Allowance tusiichanganye na hela ya nauli, dawa ya mswaki, sabuni, nguo, simu/mawasiliano, ada ya ndugu, kununua kiwanja, kujenga au kusaidia wazazi. Kupanga matumizi ni kitu cha msingi sana unapokua chuoni maana bila hivyo maisha ya chuo utayashindwa.

Asante sana kwa kusaidia hii jamii
 
Na je watu huwa wanakwenda kugonga soka au ndo masomo yako tyti coz nisije chukua vifaa vya soka hali ya kuwa vitakaa kwenye begi

Ytegemea na uwezo wa mtu na namna ambavyo anaweza kufanya time management, waweza soma ukafeli na waweza cheza na kusoma ukapasua vilevile
 
Na je watu huwa wanakwenda kugonga soka au ndo masomo yako tyti coz nisije chukua vifaa vya soka hali ya kuwa vitakaa kwenye begi

wakati mwingine shule na kuufurahisha mwili na akili vinapanda sio msuli tuuu kila mara, utakufa buremtu wangu
 
thanx sana kwa kutujuza hayo,,nami naomba kujua unaweza kukaa njee ya hostel,,maana wengine tuna familia,,

Kwa UDOM kukaa nje ya chuo unaweza ila ni mchakato kidogo kwani hawaruhusu ki-vile. wanawake hasa wenye watoto wachanga wanayo ruhusa hiyo bt kwa ma dume ni mpaka uende kwa mtendaji wa mtaa unapokwenda au unapoishi, athibitishe kwa maandishi kwamba anakufahamu, huo mchakato kwa ma deans of colleges ndo si kitoto. But unafanikiwa na wengi wanafanya hivyo. Ingawa nakushauri ukae on campus mpaka utakapozoea mazingira kwani ukienda na familia yako wakati hata ratiba yenyewe ya vipindi inahitaji uende kwanza tuition utaumia, Utajikuta unaona maisha magumu mapeeeema kabisa.
 
Unapozungumzia suala la mavazi mabovu ni chuo kinakurudisha au? Naomba uniweke sawa mkuu
 
MAKOLE eti ni kweli wireles internet inapatikana had maeneo ya hoshel[ndan ya hostel] and vp kuhus people walifany fresh wanabakishwa kufundish hapo?
 
Mkuu MAKOLE vipi kuhusu suala la dress code kwa ujumla kuanzia hostel hadi lecture rooms, je pens,raba na open shoes a.k.a masai.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom