kwa kweli kama kuna jambo la kusikitisha ni wanafunzi wa mwaka wa kwanza. Nendeni na akiba ya kutosha kwani suala la book ni mchakato mrefu. Mwaka wa kwanza wanateseka sana kwa sababu ya urasimu. Pia kuna utaratibu wa kusaini fedha za bodi kabla ya kuzipata, hata hivyo hili hufanyika sana kwa wanaoendelea. Hii wakati mwingine inasababishwa na kuchaguliwa mara mbili kwa mwanachuo mmoja hivyo mpaka confirmation ya kuwa umedahiliwa chuo kipi ifanyike. Mambo ni mengio kwa mkopo wa mwaka wa kwanza, Chukua tahadhari na uende na akiba ya kutosha. Zoezi la malipo ni vema ulifanyie ukiwa nyumbani kwenu. Dodoma hali za benki hasa CRDB inakuwa mbaya sana. Ushauri tu ni kuwa juu ya kila paying slip andika jina lako ukianza na surname, mwaka wako na namba ya usajili na degree program yako. pia usisahau kupiga photocopy ya kila document yako. Hii utaiona umuhimu wake endapo utapoteza hizo na pia unaweza kuibiwa paying slip isiyo na jina.
Malipo ya chuo hayategemeani na boom lako kwani hujaingia mkataba na chuo kuhusu fedha, makataba wako umeingia na Bodi. Kama unategemea fedha ya bodi ulipe expenses nyingine utapata shida. We lipia accomodation yao, pamoja na vitu vingine. fees utaitoa kulingana na bodi wanavyokujali.kuhusu 31 sept nimekupm