Ushauri kwa Serikali ili kuboresha Elimu nchini Tanzania

Amani Msumari

JF-Expert Member
Aug 21, 2016
1,830
976
Wadau heshima kwenu.

Taifa lolote likitaka kufanikiwa ni lazima liwekeze kwenye elimu. Uongozi wa awamu zote umefanya ulivyoweza Kuboresha elimu nchini Tanzania. Serikali ya awamu ya tano nayo haiko nyuma na imejitahidi sana katika Kuboresha elimu.

Serikali ya awamu ya tano ndiyo inayotekeleza sera ya elimu ya mwaka 2014. Sera hii inataka wanafunzi wa elimu ya awali na msingi wapate elimu bila malipo katika shule za umma. Moja ya mafanikio makubwa ya utekelezaji huo ni ongezeko la uandikishaji wanafunzi na ufaulu (tembelea tovuti za wizara ya elimu, sayansi na teknolojia na TAMISEMI kwa taarifa zaidi).

Katika jitihada hizo, serikali ya awamu ya tano inatoa shilingi bilioni 23 kila mwezi kwaajili ya elimu bila malipo. Katika kipindi cha miaka 4 mpaka mwaka wa fedha uliopita (2016 - 2019), serikali ilitumia shilingi bilioni 42 kukarabati shule zake kongwe 42 kati ya 88 zilizopo sehemu mbalimbali nchini Tanzania.

Kila shule kongwe ilipata bilioni 1 kwa ajili ya ukarabati wa madarasa, mabweni, maabara na nyumba za walimu. Bajeti ya mwaka Jana ilitengwa shilingi bilioni 450 kwaajili ya mikopo ya elimu ya juu.

Hizo ni jitihada kubwa na kipekee niipongeze serikali. Pamoja na jitihada hizo ninaamini zipo changamoto mbalimbali.

Je, changamoto hizo ni zipi? Upi ushauri wako kwa serikali ili kiwango cha ubora wa elimu nchini Tanzania kiwe kikubwa zaidi?

Amani Msumari.

Tanga
 
Ngoja wake wanaccm wakupe mawazo mazuri lakini utegemee matusi kutoka mtaa wa pili ambako arufu ya mavi imetamalaki, maana mbuzi dume sio watu!
 
Haki Elimu walizungumzia na kukosoa vizuri sana kuhusu Sera ya Elimu ya mwaka 2014. Professor Suleman Sumra alielezea mambo mengi mazuri ambayo nadhani kama yakitendewa kazi basi tunaweza kufika mahali pazuri. Alikosa mambo haya kuhusu sera ya elimu ya 2014 ambayo awamu ya tano imeanza kuitekeleza:

1. Sera haijaweka bayana kuhusu lugha moja ya kufundishia,
2. Sera haijaweka bayana kuhusu sifa za walimu,
3. Sera iko kimya kuhusu uboreshaji wa elimu ya sayansi na ufundi mashuleni,
 
Ngoja wake wanaccm wakupe mawazo mazuri lakini utegemee matusi kutoka mtaa wa pili ambako arufu ya mavi imetamalaki, maana mbuzi dume sio watu!
Hapa Kuna mengi ya kujadili Kama vile:

Lugha ya kufundushia.

Weledi na ubora wa walimu.

Mazingira ya kufundushia na kujifunzia.

Ushiriki wa jamii.

Mchango wa serikali.

Muundo na mfumo wa elimu.

Mtalaa wa elimu yetu (maudhui)content). Kuna bwana mmoja ajulikanaye pia Kama "mama Tanzania" aliwahi kuuhadaa umma wa watanzania kuwa Tanzania haina mtalaa (eeeh hujasoma vibaya na Wala sijakosea - ni mtalaa).

Mambo ni mengi
 
Mmeua elimu kwa mitaala yenu ya hovyo alafu leo mnajifanya mnataka mawazo?

Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania 2020 - 2025 Tundu Antipas Lissu anakuja na Sera bora za kuboresha elimu yetu. Nyie kwa sababu mmeshindwa kwa miaka 59 tangu uhuru basi kaeni pembeni tu mkajipange upya
 
Bila kuwajali walimu maslahi yao ni sifuri tu
Walimu ndio kiungo muhimu sana unapotaka kuhakikisha unainua kiwango cha elimu kwenye nchi yoyote ile. Usipowajali walimu, sahau kuhusu ndoto ya kuwa na elimu bora. Walimu ndio wapishi.

Kwa Tanzania, ualimu ndio kada iliyoajiri watumishi wengi wa umma kuliko kada yoyote ile. Hi maana yake ni kuwa sehemu kubwa ya malipo ya mshahara wa serikali yanaenda kwa walimu.

Ni ukweli usiopingika kuwa bado mishahara ya walimu iko chini na hili ni muhimu kuangaliwa vizuri kadiri uwezo wa kipato cha serikali unapoongezeka. Hatahivyo, sijajua ni kwanini, pengine ni kutokana na wingi wa walimu ila ukiongelea mshahara na maslahi ya walimu unatakiwa uongee kuhusu mishahara na maslahi ya watumishi wa umma. Kundi la walimu ni bahati mbaya kuwa linatumiwa vibaya kisiasa.

Vigezo vya kupanga mishahara ya watumishi wa umma pamoja na mambo mengine unaangalia muda wa kusomea fani husika. Hii Ni moja ya sababu ya madaktari kuwa na mshahara mkubwa kulinganisha na watumishi wengine kwenye ngazi ya serikali za mitaa.

Mwanasheria, mhasibu, mtu wa maendeleo ya jamii na mwalimu wenye elimu ya kiwango cha shahada ya kwanza wakiajiriwa leo katika ngazi ya halmashauri, basi angalau mwalimu ndie anayepata mshahara mkubwa kuwashinda hao wengine.

Mwalimu anafursa ya kukopa benki, anapata likizo yenye malipo (hata Kama sio kwa wakati) na ana bima ya afya Kama walivyo watumishi wengine. Tuache kudharau walimu.
 
Mmeua elimu kwa mitaala yenu ya hovyo alafu leo mnajifanya mnataka mawazo?!!!

Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania 2020 - 2025 Tundu Antipas Lissu anakuja na Sera bora za kuboresha elimu yetu. Nyie kwa sababu mmeshindwa kwa miaka 59 tangu uhuru basi kaeni pembeni tu mkajipange upya
Mawazo yako ni yapi ili yazingatiwe na chama kilichopo madarakani kwa sasa au kingine kitakachoshinda ikiwa mgombea wako hakupita?

Ningefurahi kusikia kuhusu sera hiyo ya elimu ya Tundu na chama chake
 
Kabla ya sisi wengine kutoa mawazo yetu wewe unadhani tatizo hasa la elimu yetu ni nini?.
 
Mmeua elimu kwa mitaala yenu ya hovyo alafu leo mnajifanya mnataka mawazo?

Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania 2020 - 2025 Tundu Antipas Lissu anakuja na Sera bora za kuboresha elimu yetu. Nyie kwa sababu mmeshindwa kwa miaka 59 tangu uhuru basi kaeni pembeni tu mkajipange upya
Lord Denning aione hi kwenye jalada "ni MTALAA na sio Mtaala"
 
Elimu haijitosherezi ukilinganisha na pre independence education na miaka ya mwanzo baada ya uhuru baadhi ya mambo kadhaa:-

Watoto wengi hadi 200 wanafundishwa katika chumba kimmoja cha darasa badala ya 30 hadi 45 katika shule za msingi.

Walimu wengine ni mizigo hawafai kufundisha hata wakiongezews mshahara mara elfu.

Syllabus ni za mihemuko wakati mwingine zinakosa uhalisia.

Kuna shule nyingi siku hizi zinafundisha past papers wanatakiwa kwanza wahakikishe kama wana cover all topics za Syllabus kwa undani

Idara ya Elimu au Wizara ya Elimu imenajisiwa mara kwa mara na wanasiasa.

Mwalimu ndio mlezi wa mtoto,ana majukumu mengi kuliko mfanyakazi yeyote ukiondoa taasisi chache ambazo mtumishi hufanya masaa hadi 16 au zaidi kwa siku.Serikali iboreshe maslahi,mishahara,vivutio kwa walimu.
 
Elimu haijitosherezi ukilinganisha na pre independence education na miaka ya mwanzo baada ya uhuru baadhi ya mambo kadhaa:-

Watoto wengi hadi 200 wanafundishwa katika chumba kimmoja cha darasa badala ya 30 hadi 45 katika shule za msingi.

Walimu wengine ni mizigo hawafai kufundisha hata wakiongezews mshahara mara elfu.

Syllabus ni za mihemuko wakati mwingine zinakosa uhalisia.

Kuna shule nyingi siku hizi zinafundisha past papers wanatakiwa kwanza wahakikishe kama wana cover all topics za Syllabus kwa undani

Idara ya Elimu au Wizara ya Elimu imenajisiwa mara kwa mara na wanasiasa.

Mwalimu ndio mlezi wa mtoto,ana majukumu mengi kuliko mfanyakazi yeyote ukiondoa taasisi chache ambazo mtumishi hufanya masaa hadi 16 au zaidi kwa siku.Serikali iboreshe maslahi,mishahara,vivutio kwa walimu.
Umesema vizuri sana ila ninaomba ufafanuzi was hoja zako mbili:
1. Elimu haijitoshelezi ukilinganisha na pre independence education na miaka ya mwanzo baada ya Uhuru
2. Walimu wengi ni mizigo hawafai kufundusha hata wakiongezewa mishahara mara elfu
 
Back
Top Bottom