Ushauri kwa mhariri wa BBC Swahili na Salim Kikeke

MeinKempf

JF-Expert Member
Jun 11, 2013
11,094
7,218
Miongoni mwa vyombo vya habari vyenye weledi usio na shaka katika habari zake ni BBC Swahili. Nami nimekuwa msikilizaji na msomaji wa chombo hiki kwa muda mrefu sasa hasa nyakati za asubuhi na jioni. Mimi si mwandishi mzuri hivyo usishangae namna ya mtiririko wangu ila kumbuka kuwa mimi ni "PRESCRIPTIVIST".

Siku za hivi karibuni kuna upungufu wa weledi ambao mimi kama mimi ninauona katika habari zao mbali mbali kama ifuatavyo.

1.Kuna makosa ya kiuandishi "TYPO" na baadhi ya sentensi zao kukosa upatanisho wa kisarufi "con-cordial relationship" katika makala na habari zao nyingi, kwa usahihi zaidi naomba ufatilie habari zao wanazorusha Facebook, na kwenye tovuti yao.

N.B: kwa chombo makini kama BBC wanajishushia heshima na credibility ya kuwa chombo cha
kuaminika katika habari zake kwani kinaonekana kuwa na wahariri wasio makini na habari wanazorusha
hewani. Mimi nawaomba walifanyie kazi jambo hilo ili kulinda heshima ya tasnina ya habari hasa ya
kimataifa (waige na kujifunza tokakwa wenzao BBC English) na kadhalika.

2.Kuhusu Kaka Salim Kikeke. Huyu ni mtangazaji mahiri na anayependwa na wadau wengi wa tasni ya habari ya ndani na ya kimataifa nikiwemo na mimi. Ila kuna baadhi ya mbo ninayaona kama hayaendani nae kama mtangazaji wa chombo kikubwa kama BBC. Huyu bwana Kikeke amekuwa akirusha "post" habari flani flani ambazo ninaona kama za "kitoto toto au udaku " katika ukurasa wake wa Facebook na Twitter, yaani habari nilizokuwa nikitegemea nizikute kwenye Global Publishers, Mpekuzi, Audiface, Mambo Mseto, Mambo ya Walimwengu, DJ Sek, na kadhalika ninaziona katika ukurasa wake kitu kinachofanya nione kuwa hatendei haki jina lake na hadhi yake.

N.B: Nimetoa ushauri tu, kama wakiona unafaa waufanyie kazi , kama wakishindwa wapotezee ila nimetoa dukuduku langu kwa nia ya kujenga na sio kushambulia au kuponda mtu flani au chombo flani.
Hivyo mchangiaji naomba awe ni mtu aliyesoma na kuuelewa uzi wangu na awe anayefatilia mambo niliyoainisha vinginevyo ukija kichwa kichwa utatoka kapa na kubaki.

ONYO: Changia hoja kwa adabu na heshima.
 
Watanzania kwa kuchambua tuu hatujambo, ndio maana kwenye kombe la dunia Tv zooote walikuwa na vipindi vya kukoso wachezaji wanajifaanya wachambuzi wakati timu yetu hoi bin taaban.

Walihairisha hata vipindi muhimu vya elimu nkwa jamii wakawa wapo bise na kombe la dunia, ndio matatizo yake haya kwa kuwa tumezoea kuchambua mazuri yanayofanywa na wenzetu wakati hatufanyi jitihada kutengeneza vya kwetu matokeo yake ndio hayo.

Kombe la dunia limeisha, sasa tunatafuta kingine cha kuchambua. Tumeibukia BBC Swahili.
 
Ukweli mtupu. Mara anapost akiwa Punbu street n.k. wakat anajua anachofanya.

nadhani unaona mwenyewe...na ndo mana kina shaka ssali wataendelea kuwa juu, tujenge pamoja tasnia yetu hii pendwa.
 

Attachments

  • AAAAAAAAAAAAAAAAAAAA.jpg
    AAAAAAAAAAAAAAAAAAAA.jpg
    41.4 KB · Views: 275
Sio kweli.

Mkuu , labda wewe utakuwa sio mpenzi wa kusoma BBC swahili na twit zake FB na twiter....wewe chukua muda wako anza kuchunguza, utajifunza kitu ninacho sema, lengo tumsaidie aweze jifunza uana habari wa kimataifa unavyokuwa.
 
Miongoni mwa vyombo vya habari vyenye weredi usio na shaka katika habari zake ni BBC SWAHILI. Nami nimekuwa msikilizaji na msomaji wa chombo hiki kwa muda mrefu sasa hasa nyakati za asubuhi na jioni. Kumbuka mimi si mwandishi mzuri hivyo usishangae namna ya mtiririko wangu ila kumbuka kuwa mimi ni "PRESCRIPTIVIST".

Lakini katika siku za hivi karibuni kuna upungufu wa weredi ambao mimi kama mimi ninauona katika habari zao mbali mbali kama ifuatavyo.

1.Kuna makosa ya kiuandishi "TYPO" na baadhi ya sentensi zao kukosa upatanisho wa kisarufi "con-cordial relationship" katika makala na habari zao nyingi, kwa usahihi zaidi naomba ufatilie habari zao wanazorusha "FB", na "WEBSITE" yao.

N.B: kwa chombo makini kama BBC wanajishushia heshima na credibility ya kuwa chombo cha
kuaminika katika habari zake kwani kinaonekana kuwa na wahariri wasio makini na habari wanazorusha
hewani. Mimi nawaomba walifanyie kazi jambo hilo ili kulinda heshima ya tasnina ya habari hasa ya
kimataifa (waige na kujifunza tokakwa wenzao BBC ENGLISH) na kadhalika.

2.Kuhusu Kaka SALIMU KIKEKE. Huyu ni mtangajizi mahili na anayependwa na wadau wengi wa tasni ya habari ya ndani na ya kimataifa nikiwemo na mimi. Ila kuna baadhi ya mbo ninayaona kama hayaendani nae kama mtangazaji wa chombo kikubwa kama BBC. Huyu bwana Kikeke amekuwa akirusha "post" habari flani flani ambazo ninaona kama za "kitoto toto au udaku " katika ukurasa wake wa FB, na TWITER , yaani habari nilizokuwa nikitegemea nizikute kwenye Global publishers,mpekuzi,audiface, mambo mseto, mambo ya walimwengu, dj sek, na kadhalika , leo hii ninaziona katika ukurasa wake kitu kinachofanya nione kuwa hatendei haki jina lake na hadhi yake.

N.B:
Nimetoa ushauri tu, kama wakiona unafaa waufanyie kazi , kama wakishindwa wapotezee ila Nimetoa dukuduku langu kwa nia ya kujenga na sio kushambulia au kuponda mtu flani au chombo flani.
Hivyo mchangiaji naomba awe ni mtu aliyesoma na kuuelewa uzi wangu na awe anayefatilia mambo niliyoainisha vinginevyo ukija kichwa kichwa utatoka kapa na kubaki. ONYO: Changia hoja kwa adabu na heshima.

nakubaliana na wewe kabisa hasa kwenye hilo la kwanza, nashuhudia makosa makubwa kabisa ya kiuandish ktk page ya bbc inanikera sana,
kingine ni vichwa vya habari vimekaa kiudaku sana halafu habari inaandikwa kifupi mno
wawaige wenzao DW
 
Back
Top Bottom