Ushauri kwa Jirani: Mbowe must be disposed!

Ushauri kwa Jirani: Mbowe must be disposed!

Unajuwa kitu kinaitwa life cycle?...tamaa imefupisha maisha ya chadema,CCM wamewachezea shere chadema...kwa sasa wanamkakati,wasemaji na waamuzi wakuu ni chademaccm..hii itahitaji uwe na uzoefu na macho makali,Mrema alikuwaa mkali ungekuwepo usingeamini kama ndiye huyu wa leo!....utachukuwa miaka zaidi ya miaka 10 kujua kama hutojishughulisha...kwasasa kila mechi muhimu ccm watashinda bila presha!
Mrema mlimmaliza alipojisalimisha Lumumba. Na vivyo hivyo John Cheyo. Kwa CDM mnpoteza muda, lakini si kuna chochote kiti lumumba
 
Waliouza mapinduzi ni akina mbowe they must get out of here..
 
Huwa wananiboa zaidi panapokuwa Na shughuli isohusiana Na chama wao wanatinga Nguo za kijani hakika wanaboa

alafu ili ufanikiwe huko kwao lazima uwe mnafiki na mtu kuhamisha maneno huku kupeleka kule....yaani ni njaa kali alafu
 
Nitaanza kwa kifupi kueleza makosa ya kijinga waliyofanya CHADEMA kabla ya kuelezea yale ya msingi;

1. TAMAA – Viongozi wakuu wa CHADEMA walipata UROHO wa ghafla wa kutaka kuingia ikulu kwa namna yeyote, wakasahau misingi, wakaivunja UAMINIFU (LOYALTY) kwa wananchi walioujenga kwa miaka mingi na kwa nguvu kubwa iliyojumuisha DAMU ya watanzania. Tamaa ikawafumba macho, ikatawala akili zao, ladha ya madaraka ikatawala mioyo yao.


2. JEURI – Viongozi wa CHADEMA walipatwa na jeuri, jeuri ambayo asili yake ni FEDHA aliyokuja nayo EDWARD LOWASSA, wakadharau ushauri, wakapingana na wataalamu wao waliokuwa wakiwaamini miaka yote. Wakawashushua na kuwaona sio lolote si chochote pale walipowaeleza hatari ya kumpokea EDWARD ndani ya CHADEMA.


3. KIBRI – M/kiti wa CHADEMA na genge lake wakapatwa na kibri, wakaacha Mbachao kwa msala upitao. Wakawashambulia wenzao Slaa, lipumba na kila aliyepingana nao katika wazo lao la kumuweka EDO kuwa nahodha wa chombo chao. Wakaamini katika Edo na Matajiri wenzake wanaomuunga mkono. Ujuaji ukawa mwingi na kujiona wao ni zaidi ya kila mtu.


Mwisho wa Kunukuu.

Sasa turejee hoja chache za Juliana... kupitia watu wafuatao.

1. Jecha s. Jecha(Kibri na Jeuri)
2. Dr. Shein (Tamaa)
3. Magufuli (JEURI)

Juliana wewe na Mbowe mna kitu mlinyimana/mlitofautiana. Maana ugomvi wako mkuu si wewe na CHADEMA, bali ni wewe na Mbowe.
 
swadaktaaaaaaaaaaaa
Lkn siku zao zinahesabika binam kwa kuwa tushamjua yule jini wao wanomtumiaga, waendeleee tu kuyafanya maji ya bahari kuwa na chumvi zaidi, huku wakulima wakiendelea kupata shida ya mbolea
 
Lkn siku zao zinahesabika binam kwa kuwa tushamjua yule jini wao wanomtumiaga, waendeleee tu kuyafanya maji ya bahari kuwa na chumvi zaidi, huku wakulima wakiendelea kupata shida ya mbolea

hahahahahahahha...binamu hawa jamaa pona yao ni kuwafanya wagogo waendelee kula viwavi...may be wataendelea kuwapigia kura
 
hahahahahahahha...binamu hawa jamaa pona yao ni kuwafanya wagogo waendelee kula viwavi...may be wataendelea kuwapigia kura
Na watakula sana tu, nimesikia yule fisi ameenda kufanyiwa kazi visiwani, tutashuhudia mengi
 
Nakushanga sana Shoza kifo cha chadema ni ahweni kwako na familia yako amboyo mtaendelea kuitafuna nchi......sioni maana ya wewe kuishauri chadema ,nenda kamshauri mrema na Tlp yake ambye chamavchake kinafanya vizur na nitishio kwa ccm
 
Mzee. Yupo busy kuandaa mtandao wake utakao mweka kugombea tens 2020 kama huamini mark my word
 
July nilikuwa nakuona malayer kumbe una akili sana
CDM hakika ni SACCOS sio chama cha siasa
Over..
 
Hoja zako Mheshimiwa Juliana Shonza ingawa zina msingi wake lakini zina walakini pia zina upogo katika kuziwasilisha kwake. Kwanza andiko lako limejaa mikingamo ya kutosha kiasi kwamba huwezi kujulikana kama unashutumu au unaionea huruma CHADEMA!!

Kwanza unasema kwenye uchaguzi wa Mwaka jana Lowassa alishindwa kwa "aibu". Hivi watu zaidi ya (kwa mujibu wa Lubuva) milioni sita waliomchagua Lowassa ambao ni sawa na asilimia karibia 40 ni aibu hiyo? Ina maana kati ya watu 10 watu 4 walimchagua Lowassa na wewe unasema ushindi wa aina hiyo ni aibu?

Lowassa hakutumia hila. ghilba, wala nguvu ya dola kupata kura alizozipata halafu unasema kwamba ameshindwa kwa aibu? Halafu kwa nini maandiko yenu yanaonesha kwamba ndani ya nafsi zenu mlitaka Lowassa ashinde? Au ndiyo yale mambo ya kikulacho ki nguoni mwako unatimia? Bila shaka mbele ya safari wanaowakodisha watakuja kugundua nyie ni watu wa aina gani.

Hoja nyingine ambayo ilitakiwa isitoke kwenye kundi lenu ni hii ya kusema kwamba CHADEMA imeacha kuwatetea wanyonge. CHADEMA imeacha kuwatetea wanyonge dhidi ya nani? Bila shaka kama CHADEMA ilikuwa na imeacha kuwatetea wanyonge, basi ni dhidi ya CCM na serikali inayoongozwa na CCM. Kwa maana nyingine wewe na wenzako mnakiri wazi kuwa kuna wanyonge wanaogandamizwa na CCM na wanatakiwa kutetewa.
Ndio, Lowassa ameshindwa kwa aibu, aibu yake mwenyewe, aibu kwa waliomfuata uhamishoni, aibu kwa viongozi waaandamizi Chadema, aibu kwa wapiga kura waliohemewa na mhemuko wa ulaghai kuwa sasa pasipo shaka ni hakika zamu ya Chadema. kushindwa kwake kumefadhaisha na kuvunja mioyo ya wengi, wamepoteza nguvu na mali nyingi kwa hadaa iliyoingizwa na Lowassa ndani ya chama na kushereheshwa na tamaa ya fedha na uchu wa madaraka wa Mwenyekiti wa chama. Haijalishi kwa asilimia ngapi, nguvu, hiana, fitina, pesa aliyoteketeza ili kuingia madarakani nafasi ambayo hakuipata ni aibu, amewaondoa ktk msitari kuanzia maaskofu, wanasiasa maarufu hata wamakosa fulsa ya kuaminiwa tena.
 
Madhara ya kubadili gia angani ni kuanguka kwa ndege iwapo rubani aliyebadilisha gia sio mweledi.
 
Back
Top Bottom