kipara kipya
JF-Expert Member
- May 2, 2016
- 20,142
- 24,432
Tunasikia tetesi na kelele za maandamano kwenye mitandao ya kijamii,bila kuelewa kamanda Sirro ameshaanza kuweweseka na kuanza kutoa matamko na makaripio kwa atakaeandamana kinyume cha sheria atakiona.
Ushauri kamanda Sirro wape kibali waache hao watu wenye kutaka kuandamana waende watakako cha msingi wape ulinzi na uwaeleze kabisa viongozi na waratibu wa hayo maandamano suala lolote litakalotekea kinyume na kusudio la maandamano basi wao ndio watawajibika,najua watanzania kama wataachia waende walikokusudia bila bughudha yeyote sidhani kama kutakua na uvunjifu wa amani.
Na tunawataka nanyi waandamanaji maana maandamano hubeba vibaka wa kupora basi kweli muwe na nia moja ya kufikisha ujumbe wenu sehemu husika na sio kuanza kuwachokoza polisi.
Angalizo kamanda Sirro ukiingiza intelejensia tu umeshaharibu najua askari wa kutosha unao na wanaweza kuwatuliza watu na amani ikarejea kama ilipotea
Wape kibali wajione wapo huru katika huru,utaandikwa kwenye vitabu vya kumbukumbu na historia!
Ushauri kamanda Sirro wape kibali waache hao watu wenye kutaka kuandamana waende watakako cha msingi wape ulinzi na uwaeleze kabisa viongozi na waratibu wa hayo maandamano suala lolote litakalotekea kinyume na kusudio la maandamano basi wao ndio watawajibika,najua watanzania kama wataachia waende walikokusudia bila bughudha yeyote sidhani kama kutakua na uvunjifu wa amani.
Na tunawataka nanyi waandamanaji maana maandamano hubeba vibaka wa kupora basi kweli muwe na nia moja ya kufikisha ujumbe wenu sehemu husika na sio kuanza kuwachokoza polisi.
Angalizo kamanda Sirro ukiingiza intelejensia tu umeshaharibu najua askari wa kutosha unao na wanaweza kuwatuliza watu na amani ikarejea kama ilipotea
Wape kibali wajione wapo huru katika huru,utaandikwa kwenye vitabu vya kumbukumbu na historia!