Ushauri kwa Ester Matiko (MB)

Sikutaka ku comment uzi huu !!, lakini nilipoona nawe unapotosha umma nikashangaa !!.

Hivi kweli Pascal, wabunge woote wawe CCM ndiyo tutapata maendeleo yalishindikana kwa miaka 60 ?!. Walioiharibu Tz yetu ni nani kama siyo hawa hawa CCM ?! Kweli Pascal nawe unaamini kuua upinzani kwa gharama za dola ndiyo malengo ya taifa!!!

WaTz ni waswahili na wanafki !! Yaani wote wakawe wapiga meza na kusema ndiyoooooo!! Mungu anawaona, acheni turudi kwenye u communist. Lakini tutaendelea kurudi nyuma ki maendeleo, kama ilivyokuwa huko awali .
 
Jaribuni kuvunja kibubu kilichonona madafu 500milion plus maybe itawezeakana kuhamia huko unakodai kuna umakini
 
Kama mawazo ya kuona mbali ni 2020, bado watakua hawaoni mbali! Mwaka huo siyo mwisho wa Tanzania, Tanzania itaendelea kuwepo wakiwa wameoza makaburini! Ona mbali, Paskali!
Kwenye siasa za Tanzania, tuna makundi matatu ya watu, the dreamers, the wishful thinkers, and the realists.
Dreamers wao wanaota tuu. Wishful thinkers wao wana wish, na realists wao wanausema ukweli uliopo, hivyo ukweli wa siasa za Tanzania kuelekea uchaguzi wa 2020 ni huu
Trend Reading: Wanaohamia CCM wasibezwe! Wanaona mbali, 2020 Majimbo yote kurejeshwa. Je tunarejea nchi ya Chama kimoja? - JamiiForums
P.
 
Yaani afuate nyao za kununuliwa kama mbunge wako wa serengeti ? Ujue le mutuz na kikundi chao cha ununuzi wabunge na madiwani wanapata 10% kwa kila kichwa unaelekea huwa wanakupa gawio ndiyo maana unashauri idadi ya wabunge wa kununuliwa iongezeke
 
Mkuu Odhiambo, mtu akiweka link, uwege unasoma kwanza hiyo link ndipo una comenti.
Trend Reading: Wanaohamia CCM wasibezwe! Wanaona mbali, 2020 Majimbo yote kurejeshwa. Je tunarejea nchi ya Chama kimoja? - JamiiForums
P
 

Tongozo lako bado halijamvutia
 
Mpaka sasa hakuna mbunge wa jimbo mwanamke amehama. Akihama Matiko atakuwa siyo mwanamke. Hiyo kazi waachie wanaume ndiyo wanajua wanachofanywa mpaka waamue bila kufikiri.

Pamoja na Bwana Mkubwa kumsifia kwa "kuwa mweupe na mzuri", sidhani kama Matiko anaweza fanya ujinga huu. Kimsingi Bwana Mkubwa anam-mind sana na ndiyo sababu ya kulegeza sauti siku ile.
 
Mbona humsemi Esther Bulaya au yeye ni mgumu sana?
 
Le mutuz na kikundi chao cha udalali wa siasa wabazidi kula vichwa mpaka kufika 2020 watakuwa wametengeneza pesa nyingi ni aina Fulani ya ufisadi na ufujaji wa pesa za umma, pesa za walipa kodi, hiyo pesa inayotumika kwenye kurudia chaguzi ni pesa ndefu ni pesa ambazo zingeweza kununua vivuko Nchi nzima na pengine kujenga daraja toka mwanza mpaka ukerewe na ukara.
 
Mbona humsemi Esther Bulaya au yeye ni mgumu sana?
Pesa inayotumika kuwanunua wabunge na kurudia chaguzi ingeelekezwa kwenye maendeleo leo hii Tanzania ingekuwa Nchi tajiri kuliko South Africa
 
Kura aliomba mwenyewe kwani ruzuku nyingi ilitumika kaskazini
Ruzuku ya chadema kwa sasa inatumika kulinda hujuma za CCM ikiwemo ubambikiwaji kesi na hujuma nyingi wanazofanyiwa na CCM na kikundi cha uhujumu demokrasia cha CCM, pesa nyingi inayotumika kujihami dhidi ya hujuma za CCM ingeweza kufanya vingi lakini CCM wapo busy kurejesha mfumo wa chama kimoja ndiyo maana chadema wanajihami kwa nguvu zote.
 
Keshakusikia na bila shaka mhadhiri huyu naye, kama ana roho ya 'kuunga mkono' juhudi za jiwe, atafuata nyayo. Yajayo yanafurahisha!
 
tusifurahie hata kidogo kufa kwa upinzani mana somo la Uraia tulilosoma msingi na sekondari tumefundishwa faida za upinzani katika nchi yenye demokrasia
 
Kwa sasa madalali wa siasa huko CCM wanaangalia 10% zao kwenye ununuzi wa wabunge na madiwani hawana dira wala kujua athari za kujaza wenye mioyo ya upinzani huko CCM.
 
Labda uondowe maneno “UKWELI WA”, uweke maneno “HALI YA”, please! Ukifanya hivyo utatendea kazi maneno na uzito wake!
 

Huyo anajitambua hawezi kugeuzwa bidhaa, nunueni hayo hayo makinikia, dhahabu safi itabaki Chadema.
 
Yaani kweli 2020 ndo mbali kwa Tanzania !!! Mimi nathani mbali ni "Utanzania Wetu", binadamu tuna mwisho lakini Utanzania hauna mwisho, ndio maana mataifa mengine yanaweka Sera na Mifumo ya kuwangoza hata miaka 200 ijayo ilhali sisi tunaweka malengo ya miaka miwili mbele !! Ni kweli kabisa kwamba mtu ana haki ya kuhamia Chama chochote anachoona kinamfaa, lakini akumbuke kuwa katika kuhama kwake kuna watu anawachia makovu, maana walijitoa akapata huo Ubunge, ingekuwa vizuri asubiri kipindi chake kiishe ili agombee upya kupitia Chama kingine. Kitendo cha mtu kuhama chama, anaweza kuwa anaweka doa kwa watoto au kizazi chake, kinaweza kisiamiwe tena miaka ijayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…