Lord Denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 23,494
- 57,869
Silvester Mwakitalu.
Sidhani kama kesi zilizofunguliwa dhidi ya Tundu Lissu zilipata baraka zako za kitaalam kabla ya kuwasilishwa Mahakamani. Nasema haya kwa sababu nakujua vizuri. Wewe ni mtu muungwana na mlokole sana.
Leo napenda kukushauri, kwa namna Shahidi wako wa kwanza alivyoanza kuelezea ushahidi wake dhidi ya mashtaka yanayomkabili Tundu Lissu. Ni busara kuficha aibu ya Serikali mbele ya wananchi na Wageni wa Kimataifa wanaohudhuria kwenye ile kesi kila siku kwa kuwasilisha nia ya kutoendelea na lile shauri.
Sababu kuu ni moja tu- Shahidi wako alieanzisha upelelezi wa Mashtaka yanayomkabili Lissu ya Uchochezi amesema hadharani na karekodiwa Mahakamani kuwa "alidhani Lissu alitenda kosa"
Najua unaelewa maana ya kudhani au kufikiri kwenye muktadha wa kisheria. Kwa kifupi kudhani au kufikiri kitaalam ni kupiga ramli. Mpelelezi hapigi ramli, mpelelezi anapeleleza kosa lenye mashiko kwa mujibu wa Sheria.
Kwa namna shahidi wenu wa leo alivyojielezea Mahakamani, na kwa kuwa kesi hii inafuatiliwa na mamilioni ya watu nje na ndani ya Taifa, kuepusha aibu nawashauri tu muende ku nolle. Msiponolle shauri hili, kuna aibu kuu itapata Serikali kwenye Cross examination. Kwa namna ninavyowajua Jeremiah Mtobesya, Peter Kibatala na Mpale Mpoki bila kusahau Tundu Lissu mwenyewe, mnaweza kuomba Camera zizimwe au ardhi ipasuke siku shahidi wenu atakapokuwa Cross examined.
Kuna kitu kikubwa sana mnaweza msikione kwa sasa, ila kwa namna mashahidi wenu watakavyoadhirika kwenye haya mashauri kuna picha itatengenezwa rasmi juu ya Taifa letu kimataifa kuwa ni Taifa linaloshitaki watu wake makosa ya uongo na ya kutengeneza. Na mtahitaji miaka mingine 50 kuwa convince donors, lenders na wawekezaji kuwa nyie sio Taifa la namna hiyo.
Sidhani kama kesi zilizofunguliwa dhidi ya Tundu Lissu zilipata baraka zako za kitaalam kabla ya kuwasilishwa Mahakamani. Nasema haya kwa sababu nakujua vizuri. Wewe ni mtu muungwana na mlokole sana.
Leo napenda kukushauri, kwa namna Shahidi wako wa kwanza alivyoanza kuelezea ushahidi wake dhidi ya mashtaka yanayomkabili Tundu Lissu. Ni busara kuficha aibu ya Serikali mbele ya wananchi na Wageni wa Kimataifa wanaohudhuria kwenye ile kesi kila siku kwa kuwasilisha nia ya kutoendelea na lile shauri.
Sababu kuu ni moja tu- Shahidi wako alieanzisha upelelezi wa Mashtaka yanayomkabili Lissu ya Uchochezi amesema hadharani na karekodiwa Mahakamani kuwa "alidhani Lissu alitenda kosa"
Najua unaelewa maana ya kudhani au kufikiri kwenye muktadha wa kisheria. Kwa kifupi kudhani au kufikiri kitaalam ni kupiga ramli. Mpelelezi hapigi ramli, mpelelezi anapeleleza kosa lenye mashiko kwa mujibu wa Sheria.
Kwa namna shahidi wenu wa leo alivyojielezea Mahakamani, na kwa kuwa kesi hii inafuatiliwa na mamilioni ya watu nje na ndani ya Taifa, kuepusha aibu nawashauri tu muende ku nolle. Msiponolle shauri hili, kuna aibu kuu itapata Serikali kwenye Cross examination. Kwa namna ninavyowajua Jeremiah Mtobesya, Peter Kibatala na Mpale Mpoki bila kusahau Tundu Lissu mwenyewe, mnaweza kuomba Camera zizimwe au ardhi ipasuke siku shahidi wenu atakapokuwa Cross examined.
Kuna kitu kikubwa sana mnaweza msikione kwa sasa, ila kwa namna mashahidi wenu watakavyoadhirika kwenye haya mashauri kuna picha itatengenezwa rasmi juu ya Taifa letu kimataifa kuwa ni Taifa linaloshitaki watu wake makosa ya uongo na ya kutengeneza. Na mtahitaji miaka mingine 50 kuwa convince donors, lenders na wawekezaji kuwa nyie sio Taifa la namna hiyo.