Ushauri kuhusu bandari kavu ya Kwala

Ushauri kuhusu bandari kavu ya Kwala

koryo1952

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2023
Posts
1,289
Reaction score
2,190
Jana Mhe. Rais alifungua Bandari kavu ya Kwala. Hongera sana. Kwenye maelezo ya Mhe. Mbarawa kwa Mhe. Rais alitaja mambo yafuatayo:-
(1) Bandari kavu ya Kwala itahudumia makasha yanayokadiriwa 300,000 kwa mwaka.
(2) Bandari kavu ya Kwala itahudumia 30% ya makasha yote ktoka Bandari ya Dar es Salaam. Sasa swali langu.

Kwanini Serikali isitafute eneo kubwa litakaloweza kuhudumia makasha yote kwa asilimia mia moja?. Pili kama Serikali ina uwezo . Je ni kwa nini ICD nyingi zimefunguliwa badala ya Serikali kufanya kazi hiyo?.
Ninaishauri Serikali itafute eneo kubwa na ijenge bandari kavu ili iweze kuhudumia makasha yote yanayokadiriwa kuwa 3 millioni kwa mwaka kuliko kuwaachia watu binafsi kufungua ICDS nyingi.
 
Back
Top Bottom