Ushauri kuhusiana na masuala ya mizimu!

Ushauri kuhusiana na masuala ya mizimu!

Running from your origin is craziness, they struggle seeking for the other power that doesn't belong to them

Hakuna msomi mpumbavu ndugu yangu hizo degree na masters ni makaratasi tu.

Degree au master ya uchumi inakusaidia nini kwenye maswala ya imani, stop being fool.


Aaahh ..
 
Nakazia hoja. Hawa jamaa weupe/wageni walipokuja, cha kwanza walihakikisha wamevunja-vunja, wamedhalilisha na kuifanya duni kabisa imani walioikuta tunayo na tunaiheshimu, kisha wakapandikiza mambo yao kwa manufaa yao hususan kurahisisha uchukuaji wa mali asili na kutufanya watulivu ili tutawalike kirahisi.
Sio kweli,shida mizimu yetu ilikuwa dhaifu kuliko Yao,kama mizimu yetu ilishindwa kutulinda dhidi ya uvamizi wa wakoloni huoni ilikuwa ni dhaifu na sio ya kuitegemea sana
 
Oneni hii kenge, Mungu alikuzaa wewe? Au ulizaliwa kupitia mama na baba ambao wakifa tunawaita mizimu ndugu zetu wa karibu, au wewe umebeba makamasi hapo kichwani ukisikia neno mizimu unapagawa unaona kama majini, mapepo
Hakuna konakona mnaomba mashetani hizo ni ibada za kishetani hao mnaowaomba hawadhuru wala kunufaisha chochote
 
Mortal ni hali sio kitu ambacho unaweza kukishika wala kukiona
Unajua maana ya hali,? Kabla sijakupinga au kukubalia basi niambie unaposema hali unamaanisha nini?
Yaani unajuaje hii ni hali na hii si hali au nikipimo gani kinachotumika kuijua hali?
 
Unajua maana ya hali,? Kabla sijakupinga au kukubalia basi niambie unaposema hali unamaanisha nini?
Yaani unajuaje hii ni hali na hii si hali au nikipimo gani kinachotumika kuijua hali?
Nikisema hali namanisha “state” of being mortal or immortal, its not an object or organ that you may see or touch.
 
Shukran mkuu,
• Kama ni ukoo wa kabila moja ni Sawa, maana Mizimu inaombwa hasa hasa makaburini( ya ukoo, kuyasafisha, kuchinja wanyama kwa ajili ya damu, baada ya hapo mtaludi nyumbani ) sehemu walipo kuwa wanaishi bibi na babu(kama walisha tangulia mbele za haki,).

• Mimi hii kazi kila misho wa mwaka lazima nifanye,

• Mizimu ni ulizi mkubbwa sana katika maisha wakikupenda na ni ngumu kuwatoa kupitia imani za kawaida.

• Faida niliyo iona kwenye Mizimu ni kwamba:-
(1) ukilala usiku wanakuletea njozi ya Maisha ya kesho yake itakuwaje katika harakati zako za utafutaji.
(2) wachawi watakuchukia sana maana hawezi kukuroga hata waungane, maana mchawi hawezi kuroga bila kuomba Mizimu husika ya ukoo wenu.
(3) mambo hunyooka kila utakacho gusa kwenye biashara kupata hasara ni mara chache sana.
Yah ni kweli
 
mimi sielewi mizimu inapataje nguvu. ndugu yetu walihangaika kwa waombezi wote hakuna kitu mpaka huyo Mwamposa.
alipopelekwa Meru wazee walicheka sana. chap wakafanya mambo akakaa sawa.
sasa huwa nashindwa kuelewa ina maana hiyo nguvu ya maombezi inashindwa na mizimu? wajuzi nipeni majibu.
cc Mshana Jr
 
Back
Top Bottom