Ushauri kuhusiana na masuala ya mizimu!

Ushauri kuhusiana na masuala ya mizimu!

ferucho lamborgini

Senior Member
Joined
Nov 25, 2023
Posts
185
Reaction score
599
Napitia changamoto kuhusiana na maswala ya mizimu, nataka ninunue mbuzi, mbege na vitu vyingine vitakavyotumika kwenye mila.

Nipo mkoa mwingine sipo moshi, ila changamoto nyingine kule kijijini wazee waliacha mila baada ya kushawishiwa na ndugu zetu wasomi uchwara waliobahatika kupata pesa na kukimbilia kwa mwamposa, ila mila hazikuvunjwa zingatieni hili wakuu kwahiyo bado tupo kwenye mikataba na mizimu.

Ombi langu ni kwamba nitawezaje kuwapooza hawa wazee wangu(mizimu) kwa kuchinja mbuzi angali sipo moshi na kule kuna changamoto nilizozitaja hapo juu wale wazee hawatakubali kirahisi.

kuna mtu kanishauri niende moshi nikachukue udongo alafu nirudi mkoani nichinje mbuzi na kuomba mizimu je hii itafaa?

Naombeni ushauri wachagga wenzangu.

Wale wafia dini naombeni mpite kimya kimya kama umeona kinyesi kibichi.
 
Huyu hausiki hapa mkuu.
Tafuta maziwa mtindi safi ambao toka utengenezwe haujatiwa mkono, tayarisha, tafuta kipata wikia ho wari,
Kitanda unacholala, tendegu linalotazama mlango, hapo omba msamaa kwa kuwasahau na ahidi utawasahau tena, Anza na wari/mbege, baada ya Dk 30,omba tena maliza na mtindi.
N. B,
Hapo utapata nafuu tu, kwa muda, lakini kamilisha mila na nivizuri kwenda nyumbani mara moja kwa mwaka, aidha kama unahamisha mji sawa ispokuwa ndio unahamisha udongo, jiwe, na Isale!
 
• Mizimu ni ovyo sana, nimeteswa zaidi ya miaka 15, kila aina ya mikosi ilikuwa juu yangu,,, mpaka pale nilipo kubali mashart yao... 😥😥.

• kutuliza Mizimu inafanyika na wazee wa kimila katika eneo husika(nyumbani).
 
• Mizimu ni ovyo sana, nimeteswa zaidi ya miaka 15, kila aina ya mikosi ilikuwa juu yangu,,, mpaka pale nilipo kubali mashart yao... .

• kutuliza Mizimu inafanyika na wazee wa kimila katika eneo husika(nyumbani).
Pole sana mkuu, changamoto yangu ni hao wazee wameshadanganywa kwa kupewa pesa na zawadi na wakajengewa nyumba ya kifahari na wao wamesahau asili yao kabisa.

Au ninaweza kutumia wazee wa kichaga wa ukoo mwingine wa jirani au italeta madhara?
 
Huyu hausiki hapa mkuu.
Tafuta maziwa mtindi safi ambao toka utengenezwe haujatiwa mkono, tayarisha, tafuta kipata wikia ho wari,
Kitanda unacholala, tendegu linalotazama mlango, hapo omba msamaa kwa kuwasahau na ahidi utawasahau tena, Anza na wari/mbege, baada ya Dk 30,omba tena maliza na mtindi.
N. B,
Hapo utapata nafuu tu, kwa muda, lakini kamilisha mila na nivizuri kwenda nyumbani mara moja kwa mwaka, aidha kama unahamisha mji sawa ispokuwa ndio unahamisha udongo, jiwe, na Isale!
Nashukuru mkuu, wewe ni mchaga? Hili la kuchukua udongo unalizungumziaje? Mm nataka nichinje mbuzi kabisa na sio mara moja itakuwa mwendelezo kila baada ya muda fulani.
 
Napitia changamoto kuhusiana na maswala ya mizimu, nataka ninunue mbuzi, mbege na vitu vyingine vitakavyotumika kwenye mila.

Nipo mkoa mwingine sipo moshi, ila changamoto nyingine kule kijijini wazee waliacha mila baada ya kushawishiwa na ndugu zetu wasomi uchwara waliobahatika kupata pesa na kukimbilia kwa mwamposa, ila mila hazikuvunjwa zingatieni hili wakuu kwahiyo bado tupo kwenye mikataba na mizimu.

Ombi langu ni kwamba nitawezaje kuwapooza hawa wazee wangu(mizimu) kwa kuchinja mbuzi angali sipo moshi na kule kuna changamoto nilizozitaja hapo juu wale wazee hawatakubali kirahisi.

kuna mtu kanishauri niende moshi nikachukue udongo alafu nirudi mkoani nichinje mbuzi na kuomba mizimu je hii itafaa?

Naombeni ushauri wachagga wenzangu.

Wale wafia dini naombeni mpite kimya kimya kama umeona kinyesi kibichi.
Mizimu inatesa sana ninakushauri urudi kijini ukafanye matambiko pasipo na hivyo utaharibikiwa na kila kitu.
 
Napitia changamoto kuhusiana na maswala ya mizimu, nataka ninunue mbuzi, mbege na vitu vyingine vitakavyotumika kwenye mila.

Nipo mkoa mwingine sipo moshi, ila changamoto nyingine kule kijijini wazee waliacha mila baada ya kushawishiwa na ndugu zetu wasomi uchwara waliobahatika kupata pesa na kukimbilia kwa mwamposa, ila mila hazikuvunjwa zingatieni hili wakuu kwahiyo bado tupo kwenye mikataba na mizimu.

Ombi langu ni kwamba nitawezaje kuwapooza hawa wazee wangu(mizimu) kwa kuchinja mbuzi angali sipo moshi na kule kuna changamoto nilizozitaja hapo juu wale wazee hawatakubali kirahisi.

kuna mtu kanishauri niende moshi nikachukue udongo alafu nirudi mkoani nichinje mbuzi na kuomba mizimu je hii itafaa?

Naombeni ushauri wachagga wenzangu.

Wale wafia dini naombeni mpite kimya kimya kama umeona kinyesi kibichi.
Amua kujishika na boss hao mizimu, Yesu Kristo Aliye Hai. Ongea nae yeye, jiweke mikononi mwake Yesu, basi, kesi zote zitakuwa zimekwisha. Tena kuanzia hapo unakuwa boss wa hao mizimu!
 
Huyu hausiki hapa mkuu.
Tafuta maziwa mtindi safi ambao toka utengenezwe haujatiwa mkono, tayarisha, tafuta kipata wikia ho wari,
Kitanda unacholala, tendegu linalotazama mlango, hapo omba msamaa kwa kuwasahau na ahidi utawasahau tena, Anza na wari/mbege, baada ya Dk 30,omba tena maliza na mtindi.
N. B,
Hapo utapata nafuu tu, kwa muda, lakini kamilisha mila na nivizuri kwenda nyumbani mara moja kwa mwaka, aidha kama unahamisha mji sawa ispokuwa ndio unahamisha udongo, jiwe, na Isale!
Isale ni kitu gani mkuu?
 
Kwaiyo ww unataka kusema huna wazee au watu wazima wa ukoo ukawapigia simu wakakupa utaratibu mzuri wa nn chakufanya
Mbona kla kitu mnaweka wazi wazi wakat ayo ni mambo nyeti naya kifamilia
Ebu punguza kuomba ushauri ovyo ovyo tafta ndgu zako au wazee wa kabila lako wakupe maelezo nn chakufanya

Uwo ni ushamba na ujinga unafanya
 
Kwaiyo ww unataka kusema huna wazee au watu wazima wa ukoo ukawapigia simu wakakupa utaratibu mzuri wa nn chakufanya
Mbona kla kitu mnaweka wazi wazi wakat ayo ni mambo nyeti naya kifamilia
Ebu punguza kuomba ushauri ovyo ovyo tafta ndgu zako au wazee wa kabila lako wakupe maelezo nn chakufanya

Uwo ni ushamba na ujinga unafanya
Jitafakari kabla ya kuropoka bwana mdogo, rudi darasani ujue kwanza maana ya ushamba.

Wazee muhimu wa ukoo wameshalambishwa asali na ndugu zetu wakubwa wenye pesa na wao ni wafuasi wa mwamposa.

Wewe unafikiri utapata msaada kwa watu kama hawa?
 
Back
Top Bottom