Ushauri: Huyu binti kumbe hajui kupika

Ushauri: Huyu binti kumbe hajui kupika

Troll JF

Platinum Member
Joined
Feb 6, 2015
Posts
9,328
Reaction score
13,774
Wakuu,

Hivi juzi kati nimempata mchumba though hatujatambulishana kwa wazazi tumekuwa tukiibana kila mtu giza litakapomfikia analala kwa mwenzie.

Ngoja nije kwenye mada nimekuwa nikila kwa mama ntilie mda mrefu nikaamua ninunue bidhaa za vyakula ndani ili angalau akija siku ya Ijumaa aweze kupika na kweli alivyoona kila kitu kipo huyu binti alianza kupika tangu wiki iliyopita alipika wali umeshikana naona aliweka maji mengi sana nyama alizipika kwa mda mrefu imagine hata vipande vya nyama vyenyewe vilikua vinagawanyika kama nyama iliyosagwa.

Kwa kweli niliona ni bahati mbaya japo ilikua Long dinner kwangu lakini weekend hii ndo nimegundua kuwa kumbe hajui kupika totally alirudia kupika wali vile vile kwenye kula navunga nilivunga tu kuonyesha sijagundua chochote.

Leo kabla hajaondoka amepika ugali yaani unanata kwenye mkono haujaiva kabisa. Nishaurini JamiiForums nataka nimpige chini huu ni mzigo kupika wali hata mimi sishindwi but huyu binti ambaye kamaliza chuo hivi karibuni inaonekana malezi yamemuharibu.
 
Hapo itabidi ufuatilie kipindi cha mapishi ch.10 ujaribu kutafuta mawasiliano ya mwongozaji.

Yale mapishi ya kweny 6X6 nayo hayawezi pia?
Mkuu thanks Kama hii kitu ipo she can learn japo hajajua kuwa nimegundua kuwa yeye ni mzigo
 
Mkuu thanks Kama hii kitu ipo she can learn japo hajajua kuwa nimegundua kuwa yeye ni mzigo
Utafute na bakora ya muanzi maana vya kupika anaenda navyo na akitoka kwny pindi anarudi nyumbani na alichokipika.

Akileta utumbo ni bakora tu.
 
Hahaha..mimi nimependa hapa kila mtu giza litakapomfikia analala kwa mwenzie
 
Mpe darasa la mapishi,,,unless humuhitaji ndomana unafikiria kumpiga chini
 
Ww unataka mpishi au mpenzi kama unataka mpish tafta house girl
 
Mkuu thanks Kama hii kitu ipo she can learn japo hajajua kuwa nimegundua kuwa yeye ni mzigo
Mmmh kwanza una mpango wa kumuoa au wataka kumchezea tu? kama vipi usimpotezee muda wake kutokujua kupika sio sabab ya kumuacha mwanamke kama kweli unampenda, Au unataka wale wanaojua kupika lakini ni wasaliti??? anaweza akajifunza ndani ya miezi michache tu na akawa mpishi mzuri tu.
 
I'd rather she never blow my brains, but she gotta blow my stomach with her recipes, man. Don't know what I woulda done in your shoes, but a mama that can't cook is a turn off.

We had maids, and cousin sisters around when growing up, but our mum still taught all her boys how fix ourselves in the kitchen. What's her excuse?
 
I'd rather she never blow my brains, but she gotta blow my stomach with her recipes, man. Don't know what I woulda done in your shoes, but a mama that can't cook is a turn off.

We had maids, and cousin sisters around when growing up, but our mum still taught all her boys how fix ourselves in the kitchen. What's her excuse?
Nice poem
 
Back
Top Bottom