Ushauri: Baba anampendelea mke mdogo kuliko wa ndoa

Ushauri: Baba anampendelea mke mdogo kuliko wa ndoa

TINDIX

Member
Joined
Jun 4, 2015
Posts
26
Reaction score
7
Baba yangu ana wake wengi tu wa kutosha japo ni mkristu, lakini kati ya hao wengi watatu tu ndo wanofahamika, ila amekuwa akipendelea sana nyumba ndogo kuliko familia yangu (mke wa ndoa) yani akija nyumbani ni kutufokea 24-7, hana zuri hata moja kwetu sisi, huyu mke wa pili kajengewa bonge la jumba maeneo ya Kange Tanga hilo jumba linaitwa white house.

Kanunuliwa mashamba in short yuko vizuri, sisi kuna nyumba tunakaa aliijenga yeye mwenyewe mzee mpaka sasa hatujui hiyo ni nyumba ya nani japo tunaishi, tukiimuliza anakuwa mkali sana mpaka tunatetemeka, some time anatutamkia kuwa vitu hivi nivya mke mdogo, hata sielewi tumfayaje maana kila kitu ni cha nyumba ndogo.

Some time anakudhihaki mtu unatamani umjibu vibaya, ila ndo hivo unapga moyo konde, nishaurini niseme nae kwa njia gani huyu mzee atuelewe sisi watoto wake/ na huyu bi mdogo nimfanye nini? Maana kama ni dawa huyu bi mdogo amezidisha, hatuna raha na baba hata kidogo.
 
Daini urithi.......

Waanze kutafuta vyao..., urithi washaambiwa unaenda kwa bi mdogo!
TINDIX, kama umeshafikia umri wa kujitegemea anza ku-hustle uwe na vyako achana na mawazo ya kusubiria toka kwa baba! Kingine, endelea tu kumuheshimu mshua wako hata kama ni mkali na anatoa kauli za kukera.
 
Last edited by a moderator:
Achana na mambo ya baba yako fanya kazi kwa bidii uwe na maisha mazuri umsaidie mama yako, umeandika vizuri umaonekana unajitambua so pambana. Huwezi kudai urithi akiwa hai zaidi baaye itakuja kukuumiza tu kichwa.
 
Waanze kutafuta vyao..., urithi washaambiwa unaenda kwa bi mdogo!
TINDIX, kama umeshafikia umri wa kujitegemea anza ku-hustle uwe na vyako achana na mawazo ya kusubiria toka kwa baba! Kingine, endelea tu kumuheshimu mshua wako hata kama ni mkali na anatoa kauli za kukera.
Yes njia pekee ni ku hustle,, kama yuko hai huna haki ya kudai urithi.
 
Last edited by a moderator:
Kama una uwezo au kakuwezesha kupata shule komaa upate vyako, achana na mzee, labda tu umsaidie mama apate haki yake maana katafta nae kwa hiyo ana haki yake hapo.

Mshauri mama kama haridhiki aombe talaka awe huru na nyie muwe huru mbakie kua na mahusiano ya damu ya yeye kama baba yenu.

Nyie kama watoto komaeni mpate vyenu, acheni kumtegemea mzee wenu kwenye mali yake, ni zake na ana haki ya kutumia atakavyo na amtakae.

Cha msingi msaidieni mama apate haki yake muachane na huyo mzee. Hayo ndio madhara ya mke zaidi ya mmoja.
Mimi hiwa sikubaliani na hoja ya mke mmoja kwenye mahusiano, yaani huwezi kuniambia niwe na mwanamke mmoja, ila kwenye ndoa nadhani hoja ya mke mmoja ina uzito kidogo.
 
Maskini! Dogo kua uyaone. Kila mwanaume anathamini anapopata K ikamridhisha (wengi watabisha). Jiulize ni kwa nini alioa mke mwingine! Ni kwa vile mama wa kwanza hawakuendana sawa katika suala la ndoa. Pili kawaida mwanaume akimchukia mwanamke anawachukia pia watoto. Ingawa mwanamke akichukiana na mumewe hawachukii watoto. Hii inatokana na nature ambapo mwanamke hujipenda kwanza; wanafuatia watoto. Kwetu wanaume tunapenda wake zetu kwanza na sisi tunajipenda ikiwa ni namba mbili. Tatu ni watoto tuliowazaa. Hivyo kama bi mdogo akiwachukia jua baba yanu atawachukia.

Jinsi ya kufanya: Ni kujitahidi mkawa na uhusiano mzuri na huyo bi mdogo. Pili hayo ni mapenzi mapya, yakichuja atamrudia mama yenu inagawa naye wakati huo cha moto kinamsubiri. Tatu achana na dhana ya kurithi, urithi wa mtoto ni ELIMU. Nne, mzazi ni mzazi (titi la mama tamu hata likiwa la mbwa). Ukionyesha mapenzi kwa baba yako naye nafsi itamsuta. J'mosi njema
 
Kabla ya hapo inabidi wamrestishe in pisi

Kumrestisha mshua hapana........wao wamzingue.........kama nae kazingua.........wampiganie mama yao.......
 
Unatakiwa kuanza kuishi kama yatima
jihesabu huna baba
mchukulie kuwa ni mtu tu aliwa okota wewe mama yenu na dada zenu
kidogo anachowapa mshukuru huku akili zenu ziki concetrate na kutafuta vyenu
hampaswi kumfanyia ujeuri wala kumuuliza chochote..
mtazameni kama 'mtu mwenye matatizo ya akili'....
 
Una umri gani?

Ushauri wangu kama una umri wa kujiajiri ni vyema wewe, mama yako na nduguzo muanze kujishughulisha kutafuta pesa kivingine kuendesha maisha...
 
Nikosa kubwa kuingilia mahusiano ya baba yako na mama yako hata kama sio mama wa kukuzaa lakini kama mzee unatengenezea usingizi pale, huyo ni mama yako.
Pia kama kijana unapaswa ujitambue, huu sio wakati wa kutoa mimacho kwenye mali za urithi. Soma kwa bidii, fanya kazi kwa bidii, tafuta kwa bidii ili nawe umiliki vyako kwa jasho lako.
Mzee kua mkali haiwezekani awe mkali pasipo sababu, jitazame na ikibidi mjichunguze kwamba wapi mnamkwaza mshua au pengine mnamuonyesha wazi kuegamia upande mmoja wa mama kwakua tu yeye na mamaenu wametofautiana.
Alafu kwanza nakuona kama unadalili ya uvivu sana kijana wewe, yaani kwa umri huo mdogo umesha anza kujipangia kupata urithi! Kwaivyo unaombea mzee atoweke mapema ili upate chako?
Badilika kijana
 
Una umri gani...?achana na hayo piga kitabu au piga kazi uanze maisha yako waachie yao
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom