Ushamba: Siasa ndani ya ndege ya kibiashara (Dreamliner)

Ushamba: Siasa ndani ya ndege ya kibiashara (Dreamliner)

Picha tafadhali maneno matupu kwenye tukio kama hilo ni kosa sana...

Nauliza hao viongozi nauli wamelipa lakini? Hatutaki mambo ya staff humo...


Cc: mahondaw
 
Ndege ya Serikali aina ya Boeing 787-8 Dreamliner imeanza safari ya kwanza leo Julai 29, 2018 tangu ilipowasili nchini Julai 8.

Ndege hiyo inayoelekea Mwanza kupitia Kilimanjaro (Kia) iliondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam saa 12:35 asubuhi badala ya saa kumi na mbili asubuhi.

Kabla ya ndege kuondoka abiria walihesabiwa na baadaye wahudumu walitoa matangazo ya usalama.

Tofauti na ndege nyingine za Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) aina ya Bombardier, matangazo ya usalama katika ndege ya Dreamliner yanatolewa kwa njia ya video kupitia skrini iliyo mbele ya kila kiti.

Ukaguzi wa abiria

Awali, eneo la ukaguzi wa abiria wa safari za ndani lilijaa hivyo mtu alitakiwa kusubiri kwa takriban dakika 20 ili kukaguliwa jambo lililosababisha muda wa abiria kuingia kwenye ndege kuchelewa.

Idadi ya abiria kwenye chumba cha kusubiri kupanda ndege kilikuwa na watu wengi.

Awali, ilipangwa muda wa abiria kuingia kwenye ndege uwe saa 11:20 asubuhi lakini kutokana na wingi wa watu, walianza kuingia saa 11:35 asubuhi wakitangulia viongozi kadhaa waliokuwapo na waandishi wa habari.

Ndani ya ndege kulikuwa na wahudumu takriban 10 waliotoa huduma kwa abiria kwa ukarimu.

Miongoni mwa abiria waliokuwapo ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk Hassan Abbasi.

Abiria aliyeingia na bendera ndogo tatu za CCM, alimkabidhi moja Polepole aliyekuwa amevaa sare za chama hicho.
Polepole aliyekuwa akipiga picha na baadhi ya abiria alisema, “Magufuli hoyee.”

Baadhi ya abiria aliokuwa amekaa nao karibu waliitikia, “Hoyee.”

Rais John Magufuli aliahidi kuifufua ATCL kwa kuipatia ndege mpya, Dreamliner ikiwa ni utekelezaji wa ahadi hiyo.

Abiria mwingine alisema ndege hiyo inatokana na kodi za wananchi.

Polepole aliijibu kwa kusema, "Ni kweli kabisa hizi ni kodi za wananchi lakini matumizi mazuri yanapangwa na Serikali."

Ilivyokuwa Kia

Ndege hiyo ilitua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia) saa 1:17 asubuhi.
Baada ya kutua Kia ikiwa ni mara ya kwanza, ndege hiyo ilipokewa kwa kumwagiwa maji.

Baadhi ya wananchi waliokuwapo uwanjani na wafanyakazi wa Kia walitumia simu zao za mkononi kupiga picha tukio hilo.

Abiria walioshuka uwanjani hapo walikabidhiwa maua.

Katika uwanja wa ndege wa Kia ndege ilikaa kwa dakika 40 kabla ya kuruka kuelekea Mwanza
Kabla ya ndege kuondoka abiria walihesabiwa na baadaye wahudumu walitoa matangazo ya usalama.

Tofauti na ndege nyingine za Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) aina ya Bombardier, matangazo ya usalama katika ndege ya Dreamliner yanatolewa kwa njia ya video kupitia skrini iliyo mbele ya kila kiti.
Miongoni mwa abiria waliokuwapo ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk Hassan Abbasi.

Abiria aliyeingia na bendera ndogo tatu za CCM, alimkabidhi moja Polepole aliyekuwa amevaa sare za chama hicho.
Polepole aliyekuwa akipiga picha na baadhi ya abiria alisema, “Magufuli hoyee.”

Baadhi ya abiria aliokuwa amekaa nao karibu waliitikia, “Hoyee.”
Ulichoeleza ni mambo ya kawiada katika usafiri wa anga. Masuala ya usalama na watu kupiga picha ndani ya ndege hakuna Siasa kama unavyotaka kushawishi wasomaji kuamini. Kichwa cha habari, 'Ushamba:Siasa ndani ya ndege ya kibiashara (Dreamliner)' kimeandikwa kishabiki japokuwa maelezo yako ni fair. Siasa na ushamba umeviona wapi?
 
makamanda mtapata tabu sana awamu hii, hapo mlitamani hiyo ndege ikose abiria ila kwa maelezo wako inaonekana abiria walikuwa wengi kwelikweli!
Ndege isingeweza kukosa abiria asilani. Humo kuna viongozi kama polepole ambao wanatumia kodi zetu na pia hiyo ndege 95% wa abiria wanasafiri kwa complimentary tickets.
Kwa ufupi hapo hakuna biashara ni hasara kwa kiwango cha 100% sisi walipa kodi yutakifidia. Maana kwa hiyo mail I ya 98000 ukitoa matuminzi mishahara, ya crew, flight allowance, chakula cha ndani ya ndege, mafuta, landing charges ground handling kwa ujumla wake na crew transport mjue wengine wanatumia magari yao hapo kweli kuna faida?
 
Kwani Chadema mlinyimwa kwenda na Magwanda yenu?
 
Ndege olikua na abiria wangapi kwanza?
 
Nilishangaa kuona imeandikwa "hapa kazi tu"!!

Wasipofuta hili neno sintokaa nipande hili lindege...bora nikapande kenyaaiways, rwanair na ethiopia airline...
Hata mimi nikipata safari ya nje ni bora nisafiri na ndege za mashirika mengine lakini sio hii ndege ya kisiasa.Tuwaachie ndege yao maana walichoshindwa ni kuisajili tu kama mali ya CCM.
 
Asante kwa mrejesho mkuu, Nilikuwa na shauku ya kupata taarifa za tukio hilo muhimu. Agharabu nimepata picha kamili ya kilichotokea kabla ya taarifa za habari. Ubarikiwe🙂.
 
Kwani Chadema mlinyimwa kwenda na Magwanda yenu?
Tatizo siyo magwada wala CHADEMA tatizo ni matuminzi mabaya ya kodi za wananchi kuanzia wana CCM CHADEMA na wasiyo na vyama. Na usifikiri kuwa kwenye hiyo ndege hawapo wanachama wa CHADEMA wapo wengi tu maana hawajaziuliwa kupanda hata mimi ningekuwepo nigepanda nani asiye taka vitu cha urahisi?
 
Hata mimi nikipata safari ya nje ni bora nisafiri na ndege za mashirika mengine lakini sio hii ndege ya kisiasa.Tuwaachie ndege yao maana walichoshindwa ni kuisajili tu kama mali ya CCM.
Kwa ufupi mimi ikuwa nauli ni nafuu nitapanda kwa sababu mwisho wa siku hii hasara tutailipa kwa miaka mingi kwa kodi zetu ila ikuwa ghali sipandi. Inajua nikiifikiria hiyo hasara tutailipa kwa miaka mingapi Mungu ndiye anajua
 
Tatizo siyo magwada wala CHADEMA tatizo ni matuminzi mabaya ya kodi za wananchi kuanzia wana CCM CHADEMA na wasiyo na vyama. Na usifikiri kuwa kwenye hiyo ndege hawapo wanachama wa CHADEMA wapo wengi tu maana hawajaziuliwa kupanda hata mimi ningekuwepo nigepanda nani asiye taka vitu cha urahisi?
matumizi mabaya kwani wamenywea CHIMAY??
 
matumizi mabaya kwani wamenywea CHIMAY??
Sawa sawa na kununua Mercedes Benz brand na kuifanya biashara ya Uber na utegemee kurudisha gharama na kupata faida. Biashara ni fani
 
uzuri wa mtu anayepata taabu sana huwa anajitokeza hadharani na visingizio lukuki.....naishia hapa
 
Back
Top Bottom