Ushahidi tuhuma za January Makamba

Ushahidi tuhuma za January Makamba

Mtoa hoja hajui hata kulinganisha vitu. Ishu za Zitto zinajukijana ni uwongo mtupu. Hii ya huyu jamaa ipo wazi sana. Acha kutetea ujinga. Hii ishu ya ufisadi ni tofauti na propaganda za kitoto za chadema kwa Zitto. Huu ni uchafu kwa kiongozi kama waziri. Hapaswi hata kutuumiwa.
 
Nasikitika, maana naona mtu uliyereta utetezi kama ni kijana mwenzangu, ambaye hata kama umetumwa na makamba ufanye hivyo,basi wewe tahaluma yako uitendei haki hata kama unatahaluma ya sayansi kimu, hisikufanye kuwa kasuku wa wanansiasa ambao wanatuma kama Makamaba, nataka niseme wazi katika sakata hili inatakiwa iundwe tume mahalumu nipo tayari kujitolea, lazma kuna jambo hapa.

Unataka ujitolee kwenye tume ya kuwapatanisha Mwamvita na mpenzi wake wa zamani wa Kiitaliano?watakucheka!!
 
Mwitaliano ana akili sana au niseme ame-apply mbinu za kimafia. Hii imekuwa kama ransom - teka mtu unayemdai, tena mwanasiasa maarufu, kwa kudai zawadi uliyotoa kwa vile ulikuwa ukipata p...ch ya dada mtu lakini ukatemwa. Serikali inatetemeka na kukulipa 'haki yako' maana hii ilikuwa ni aibu kwa serikali. Unaambiwa kanusha. Hana cha kupoteza, amepata chake na mwanasiasa aliyetekwa sasa yuko huru.

Hahahahah.....
 
Ata
Huyu mzungu naye mshenzi tu, asitufanye Watanzania ni wapumbavu.

Kwani hayo mawasiliano huyo Mange kayatoa wapi?!!

Watajuana wenyewe!

Atakwambia hizo records zimetengenezwa tu, sio za kweli na Inaishia hapo!
 
Huyo kapewa agizo tu!

Nakumbuka niliwaambia hapa msije kushangaa hata hiyo press confrerence inafutwa.
Kwani aliyewaambia kuwa kuna press ni Muitaliano? Manyumbu mtakufa kwa presha kwa kuwa kila kitu siku hizi mnazusha kuanzia tuhuma hadi press mmejitungia tu na hayo yote ni kukosa jambo la kuongea siku hizi dhidi ya serikali kwani Rais Jpm kawaziba kabisa midomo yenu.
 
Huyo kapewa agizo tu!

Nakumbuka niliwaambia hapa msije kushangaa hata hiyo press confrerence inafutwa.
MIMI NILIKUWA NASUBIRI SANA KUONA HAYO MAAJABU YA RAIA WA KIGENI, TENA "MZUNGU" , AKIITISHA PRESS CONFERENCE HAPA HAPA NCHINI KUMSEMA WAZIRI, TENA, WA CCM.! NILIAMINI ATAELEWA HATA KWA DALILI TU NA HATOTHUBUTU KUONGEA!
 
Ni muhimu sana kuweka akiba ya maneno?, See, Judge, Act then Reflect
 
nahisi kama mtu anajaribu kulazimisha evidence zaidi kwenye hili sakata, ngoja Movie iendelee
 
Una facts za ziada mkuu uweke?
Makamba amekubali alipokea hela kutoka kwa huyu jamaa kama msaada wa jimbo na zikaingia kwenye account binafsi ya makamba. Na Prof. Tibaijuka alisema alipokea hela za msaada wa kusaidia shule yake na zikawekwa kwenye account binafsi. Kunafouti gani kati ya January na Prof Tibaijuka?
Wote hawa walipokea rushwa kwa mgongo wa msaada.
Kwa hiyo January awe mnzalendo haondoke kwenye uwaziri na harudishe hela za mtaliano kwani ni hela ndogo kwake.
 
Kwa maana hiyo maneno ya makamba alipohojiwa na kusema huyo mzungu ni tapeli naye ampekaziwaaa.nyi mlishajichanganya na tumeshayajua.so bado msimamo wetu ni kuona hilo jipu linatumbuka
 
Huku kitaa tushajua jamaa ni dalali so twamuangalia rais wetu magu atalitumbua ili tuzidi muamini amaaaa.afu nyi vijana wa buku7 kama leo mliitwa mpewe semina ya kuattack basi mshachelewa sanaaa jamaa yenu sasa yupo uchiiiii
 
Haujamsikia mwenyewe JM akikiri kuupokea mzigoo..?
waswahili wabaya sana, wao hawana jema, sasa leo mzungu kawaumbua, wale waliokuwa mishipa imewatoka wapo wapi sasa?.
muogopeni mungu. January Fanya kazi, achana na wajanja wajanja hawa.
 
mkuu Mchange tunakushukuru , lakini tunakuomba uweke wazi masilahi yako kwenye sakata hili .
 
nilijua tu hii mambo ni pulizo

mwanzoni nilisikiliza zile clip lakini sikuona sehemu ambayo makamba amehusika directly, ila watu wakai pump weee, pulizo likajaa na sasa lime burst
ila utetezi wa mzungu hauingii akilini, maana kwenye zile clip alikua anaonekana anamshinikiza dada mtu ili akutane na makamba kwa ajili ya serious business
 
Binafsi huwa nashindwa kuwaelewa viongozi wetu wa Kiafrika wakituhumiwa kwa jambo fulani wanakimbilia haraka sana kukanusha mwisho wa siku jambo alilokanusha linakuwa wazi na aibu kubwa kwa nini kama kuna tuhuma kama hizi wewe January Makamba usichukue hatua ya hekima kabisa yakujiuzulu nafasi yako ya uwaziri? kuna Waziri mmoja mdogo nchini Uingereza miaka ya nyuma aliwahi kutuhumiwa kuwa alionekana amesimama na mwanamke ambaye ni changudoa kesho yake ilipojulikana tu bila kusubiri uthibitisho wa jambo hilo alijiuzulu mara moja, sasa wewe Bwana Mdogo January uongozi ni dhamana na tena ni heshima ukijiheshimu kushikilia ofisi ya Umma unapaswa kuwa safi maana ni kioo cha jamii nzima ya kitanzania leo umetuhumiwa kumtapeli sijui mtaliano midola kadhaa ili umewezeshe kupata tenda ya kujenga bandari ya Bagamoyo jambo kama si la kweli litajulikana wakati huo ww ukiwa pembeni ya uongozi vyombo vya dola vifanye uchunguzi wake vijiridhishe bila wewe kuwepo ofisin, ukibakia umeshikilia ofisi maanake ni kwamba unataka kuvinyima vyombo vya dola kukuchunguza kwa sababu askari hawezi kumchunguza kiongozi wake wamefundishwa utii, nakushauri jambo likiwa jema utarudishwa kwenye nafasi yako tena itakuwa kubwa zaidi. Tatizo ninaloliona hapa ni AIBU ya Lugha mnazopenda kuzitumia mnapokuwa kwenye nafasi hizo mnajawa na viburi vya uzima, na madaraka kwa kutegemea nguzo ya chama jambo ambalo linaifanya nchi kukosa vijana wenye weledi wa uongozi, sisi tunawategemea vijana muwe na staha ktk uzungumzaji wenu lakini mmekosa maneno ya hekima mnazungumza na vyombo vya habari kwa kujisifu, kukashifu wazee, kujifanya kuwa ninyi ni zaidi ya wazee walioanza uongozi kwa mda mrefu lakini wao mwawaona kuwa sio kitu ninyi na wazazi wenu mmejimilikisha taifa nakusahau kuwa hii ni nchi yetu sote.
 
Hivi kuna tofauti ya Zitto na Makamba? Hata aliyeleta uzi ni Mchange! Unakanusha nini wakati Makamba amekiri kupokea fedha na kumuunganisha na Waziri wa uchukuzi?
asante sana mkuu .
 
Back
Top Bottom