Usanii na usaliti wa Zitto Kabwe vinakaribia kufika kikomo. Nini hatima yake?

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,632
697,796
Upepo unavuma vibaya upande wa ACT wazalendo kupitia kiongozi wake mkuu asiyechaguliwa kwa kura ndugu ZZK.

Amebakiwa na muda mchache muhimu wa kuzicheza karata zake vema la sivyo chama kinaenda kumeguka mapande mawili huku pande kubwa likibaki visiwani na yeye kuachwa na kipande cha bara kisicho na maslahi wala nguvu..!

Je mapito ya CHADEMA yaliyopita na kukiacha chama kiikiwa kimoja na chenye kuimarika zaidi yatawezekana kwa ZZK na ACT yake¿? Kumbuka ZZK ni zao la CHADEMA na alisaidia pakubwa kuiyumbisha pale alipoutaka uenyekiti mwaka 2010/2011?

Mwisho wa mchezo yeye na kundi lake walikimbia CHADEMA na kwenda kuanzisha ACT WAZALENDO ile ya kwanza..Ambayo hata hivyo walihitalifiana na ikazaliwa ACT WZALENDO nyingine chini ya ZZK mwenyewe na washirika wake wengi kutimkia CCM.

Rangi halisi za ZZK zilianza kuonekana kwenye uchaguzi mkuu 2015, akionesha viashiria vingi vya ubinafsi, choyo ,tamaa na usaliti... Baadae ilikuja kuthibitika pasina shaka kwamba huyu ni pandikizi na yuko kww maslahi binafsi zaidi kuliko kazi za kisiasa zenye malengo makubwa kwa manufaa ya wengi.

Kupitia ZZK ACT kikawa chama cha mtu mmoja ama kikundi cha walafi wachache wasioaminiana na wasio wamoja.. Nusura ya ACT ni pale Maalim Seif Hamad Rashidi alipojitoa CUF na kuiiunga na ACT ndio chama kikapata uhai mpya lakini sasa mizizi yake kimamlaka ikahamia visiwani ambako kwa sababu ya Maalim seif chama kikapata viti vya uwakilishi na hatimaye kuunda serikali ya Kitaifa huko Zenji ambapo viongizi wa ACT waliula.

ACT baada ya uchaguzi mkuu wa 2020 kikawa na sura nyingine tofauti kabisa na hapo kilivyokuwa kabla..ACT ya sasa ni CUF asili ndani ya rangi za zambarau na kwa hakika bila kupepesa wala kupapasa macho nguvu yake iko kisiwani kwenye ruzuku na support ya serikali nzima.

ZZK hana asili na Visiwani na hana ubavu wa kuzi control siasa za CUF..Tangu kuondoka kwa Maalim seif na ile keleb aliyopigwa na mgombea urais jasusi mbobezi, amejaribu kwa kila namna kukidhibiti chama ili kiwe chini ya miliki na mamlaka yake lakini ameshindwa kabisa.

Sasa wanazi wa CUF ndani ya sare ya zambarau wameanza kumchoka na wameshamuanzishia chokochoko za kila aina.. Ana muda mchache wa kuzichanga karata zake vizuri..akiyumba kidogo tu watamtupa nje ya janazi na nje mawimbi ni mengi.

Je wakifanikiwa hili..ni nini future yake kisiasa!? Muda utasema THE SOONEST!
View attachment 2113949
 
Tatizo la Zitto anapenda siasa za kijanja akiamini watanzania ni wajinga hawatajua au hata wakijua hawatachelewa kusahau uhuni wake wa ushirikiano na CCM.

Anafanya hivyo kwasababu ya tamaa ya madaraka na umaarufu, anataka kulazimisha chama chake kiwe kikubwa zaidi ya Chadema kwa njia yoyote hata ikibidi kuuza uhuru wake na chama chake kwa CCM.

Sasa kinachoenda kutokea upande wa ACT Zanzibar, ambayo ndio ngome yake kuu ni kwamba, baadhi ya wanachama walioanza kujitoa kwasababu ya kutoridhishwa na namna uchaguzi wa kumpata mwenyekiti wa chama chao ulivyofanyika wataondoa na wenzao, hili litakuwa pigo lake la kwanza.

Pigo la pili ni ACT itaenda kupoteza umaarufu wake kwasababu itashindwa kuikemea serikali ya CCM wakiwa kama wenzao, hili litawafanya wazanzibar hasa wapemba wakose wa kuwasemea kwani viongozi wa chama wanachokiamini wameshawekwa mfukoni na serikali ya CCM.

Hapa naona kuna uwezekano kikatokea chama kingine cha upinzani Zanzibar kuwasemea hasa wapemba na hiki ndio kitaenda kupata umaarufu zaidi na kukipoteza kabisa ACT kwasababu ya tamaa ya madaraka aliyonayo Zitto.
 
Unataka kusema historia ya Wazanzibari wa CUF na James Mapalala inaweza kujirudia kwa ACT Wazalendo na Zitto Kabwe?
Mkuu, ukikutana misukule wa Mbowe wanamjadili Zitto wewe endelea na Maisha yako.

Hakuna mjadala wa maana wowote utaukuta Hapo.

Siku zote wanasiasa wote ambao huwa wanakosana na Mbowe huwa wanapotea kwenye siasa, sasa huyu Zitto anaonekana Ni kichwa ngumu ndio maana vimjadala uchwara kama hivi kutoka kwa Hawa wafuasi wake Mbowe vimeshindwa kuisha.

Kumbuka, siku zote ukikosana na Mbowe wewe ndio MKOSAJI.
 
Unafikiri dola itamuacha mama avuke mstari wa miaka miwili wa kutawala kwamba wameridhika na utawala Wake?
Inategemea na inategemea bado wanamhitaji Zitto kiasi gani! Kama tayari wameshapata mbadala kilio kinakuja....
 
Mkuu, ukikutana misukule wa Mbowe wanamjadili Zitto wewe endelea na Maisha yako.

Hakuna mjadala wa maana wowote utaukuta Hapo.

Siku zote wanasiasa wote ambao huwa wanakosana na Mbowe huwa wanapotea kwenye siasa, sasa huyu Zitto anaonekana Ni kichwa ngumu ndio maana vimjadala uchwara kama hivi kutoka kwa Hawa wafuasi wake Mbowe vimeshindwa kuisha.

Kumbuka, siku zote ukikosana na Mbowe wewe ndio MKOSAJI.
Kwanini unalazimisha huu mjadala uwe wa wafuasi wa Mbowe?

Watu wengine hawawezi kujadili haya mambo?
 
Kwanini unalazimisha huu mjadala uwe wa wafuasi wa Mbowe?

Watu wengine hawawezi kujadili haya mambo?
Aliyeanzisha mjadala Ni mfuasi wa Mbowe.

Kwanini unalazimisha kufumbia macho Jambo lililo wazi?
 
Aliyeanzisha mjadala Ni mfuasi wa Mbowe.

Kwanini unalazimisha kufumbia macho Jambo lililo wazi?

Tuseme kweli, mjadala ni wa misukule wa Mbowe, for the sake of argument.

Wewe umekuta misukule wa Mbowe wanamjadili Zitto, umeshindwa kuendelea na maisha yako.

Umejiingiza katika mjadala.

Halafu unanishauri mimi nikikuta misukule ya Mbowe wanamjadili Zitto, niendelee na maisha yangu.

Unaelewa kwamba hapa hata wewe mwenyewe umeshindwa kufuata ushauri unaonipa?
 
Wewe umekuta misukule wa Mbowe wanamjadili Zitto, umeshindwa kuendelea na maisha yako.

Umejiingiza katika mjadala.

Halafu unanishauri mimi nikikuta misukule ya Mbowe wanamjadili Zitto, niendelee na maisha yangu.

Unaelewa kwamba hapa hata wewe mwenyewe umeshindwa kufuata ushauri unaonipa?
Hi ni public platform. Huwezi kuweka mada kwenye public platform halafu ukataka public iendelee na Maisha yake.

Huo Ni UJUHA.

Huwezi ku-dictate aina ya mjadala unavyotaka uwe.
 
Hi ni public platform. Huwezi kuweka mada kwenye public platform halafu ukataka public iendelee na Maisha yake.

Huo Ni UJUHA.
Sasa kama unajua hii ni public platform, kwa nini unanipangia mjadala upi nichangie na upi niuache niendelee na maisha yangu tu?

Nilikuomba ushauri wa mijadala ya kuchangia?

Au kiherehere chako tu kupapatikia watu?
 
Sasa kama unajua hii ni public platform, kwa nini unanipangia mjadala upi nichangie na upi niuache niendelee na maisha yangu tu?

Nilikuomba ushauri wa mijadala ya kuchangia?

Au kiherehere chako tu kupapatikia watu?
Sasa kama unajua hii ni public platform, kwa nini unanipangia mjadala upi nichangie na upi niuache niendelee na maisha yangu tu?

Nilikuomba ushauri wa mijadala ya kuchangia?

Au kiherehere chako tu kupapatikia watu?
Unaweza kunionesha Ni wapi nimepkupangia mjadala upi ucha gie?

Nikupapatikie wewe, kwani una tundu lolote la ajabu ninalolihitaji?
 
Unaweza kunionesha Ni wapi nimepkupangia mjadala upi ucha gie?

Nikupapatikie wewe, kwani una tundu lolote la ajabu ninalolihitaji?
Umeandika hivi. Bila mimi kukuomba unisaidie kujua mjadala upi nichangie.

Sihitaji msaada wako kujua mjadala wa kuchangia, siku nyingine usiniletee kiherehere chako.

Maneno yako haya.

"Mkuu, ukikutana misukule wa Mbowe wanamjadili Zitto wewe endelea na Maisha yako.

Hakuna mjadala wa maana wowote utaukuta Hapo.

Siku zote wanasiasa wote ambao huwa wanakosana na Mbowe huwa wanapotea kwenye siasa, sasa huyu Zitto anaonekana Ni kichwa ngumu ndio maana vimjadala uchwara kama hivi kutoka kwa Hawa wafuasi wake Mbowe vimeshindwa kuisha.

Kumbuka, siku zote ukikosana na Mbowe wewe ndio MKOSAJI."
 
Back
Top Bottom