Usaliti wa Dkt. Slaa ni upi?

Usaliti wa Dkt. Slaa ni upi?

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
97,152
Reaction score
137,156
Nimekuwa nikisoma soma humu tokea 2015 kutoka kwa baadhi ya watu kuwa eti aliyekuwa katibu mkuu wa CHADEMA na mgombea urais wa chama hicho mwaka 2010, Dkt. Wilbroad Slaa ni msaliti.

Eti ni msaliti kwa sababu aliamua kuachana na siasa baada ya CHADEMA kuamua kubadili gia angani. Pia, baada ya kuachana na siasa akakataa pia kumuunga mkono mgombea wa UKAWA, Edward Lowassa.

Sioni kabisa usaliti wa Dkt. Slaa hapo. Ninachokiona ni mtu mwenye msimamo na uadilifu na anayeongozwa na kanuni.

Hivi kweli kabisa mtu na akili yako timamu, kati ya Slaa na CHADEMA, unaweza kumwona Slaa ndiye msaliti?

Kama kuna msaliti basi msaliti huyo ni CHADEMA na si Dkt. Slaa.

CHADEMA walisaliti karibu kila kitu walichokipigania wakiongozwa na Dkt. Slaa. Ni CHADEMA ndiyo waliobadilika. CHADEMA ndiyo wasaliti.

Nyie wote mnaodiriki kumuita Dkt. Slaa kuwa ni msaliti ni vifuu tundu msiojielewa kabisa.
 
Mbowe na Lowassa Nani msaliti?

Mbowe kawasaliti watanzania wapinzani waliokuwa wameujenga upinzani Kwa Hali na mali,

CCM mafail yote ya Lowassa wanayo na Lowassa ni mnyonge, kuna mengi hayasemi kuwahadaa watu,

Ila mbowe msaliti
 
Hadi sasa kwa kweli sijaona doc yuko vizuri ssana hata katika uzungumzaji wake kifupi anajielewa. Ila mahaba yakizidi huwezi kuona hili. Akirudi mi napendekeza apewe uwenyekiti atafaa sana.
 
..hakuna usaliti wowote.

..kwanza vita ya ufisadi haikupiganwa na Dr.Slaa peke yake.

..wako wanachama wengi waliojitoa pamoja na Dr ktk kupinga ufisadi.

..Ila CDM waliamini EL atawaletea ushindi.

..hawakuamini kama Dr.Slaa angeweza kushinda uchaguzi.

..matokeo yake wakambwaga Dr na kumchukua EL and the rest is history.

..chama chochote kinapoamua kumsimamisha mgombea fulani there is a risk involved.

..mgombea huyo anaweza kushinda au kushindwa. Sasa akishindwa chama kinapaswa kujipanga upya.
 
Hata hawa wabunge na madiwani wanaonunuliwa chanzo ni ujio wa Lowasa.

Hata baada ya kumpokea Lowasa Chadema walijifanya wanaweza kushindana na ccm ambacho ni chama dola.

Walimnunua Katibu wa ccm Iringa, alihama bila hata kukabidhi ofisi matokea yake akapewa ubunge viti maalum Chadema.

Tuliwaambia toka awali Chadema ifuate misingi na taratibu za chama kwenye uendeshaji wa shughuli zake sio kupimana na ccm ambacho ni chama dola.

Matokea yake ndio haya ccm wameingia miguu yote miwili kwenye ununuzi wa viongozi wa Chadema.

Ahaaa... hawa Chadema acha dhambi ya usaliti kwa watanzania iwatafune tu.
 
Yetu masikio na macho, 2020 election ndo tutajua nani msaliti, Kati ya Dr Slaa Na Mbowe
 
CHADEMA walisaliti karibu kila kitu walichokipigania wakiongozwa na Dkt. Slaa. Ni CHADEMA ndiyo waliobadilika. CHADEMA ndiyo wasaliti.

Nyie wote mnaodiriki kumuita Dkt. Slaa kuwa ni msaliti ni vifuu tundu msiojielewa kabisa.

Itawachukua muda mrefu sana hawa ndugu zetu kutambua hili na kukubali upekee wa mchango wa Dkt. Slaa katika kujenga upinzani. Sasa hivi wamekuwa kama kondoo wasio na mchungaji!
 
Uteuzi umeisha kinondoni walishamteua mgombea ccm punguza povu
Hizi ndizo hoja mlizobakiwa nazo!

Kufirisika kihoja ni kubaya sana!

Umejuaje kama anatoa povu lakini pia hata kama anatoa povu, umejuaje anatoa povu kwa ajiri ya kupata uteuzi?

Ina maana wewe hutoa povu kabla hawajafanya uteuzi?

Baadhi ya watu wakisema ninyi ni makarai mnaanza kupiga kelele?

Bora uwe mjinga lakini ujue kuwa ni mjinga kwa sababu atatafuta msaada kuliko kuwa mjinga asiyejua kama ni mjinga kwa sababu utaonyesha ukubwa wa ujinga wako bila kujitambua.
 
Slaa alimkataa lowasa akaonekana msaliti, leo hii wapo wengi waliokosa imani nae lkn hawakiri km slaa was right. Just bendera fata upepo. Chadema imebakia matusi tu na sio hoja.

Slaa hajabadilika.

Alimkataa Lowassa wakati Lowassa yupo CCM na akamkataa alipoenda CHADEMA.

Huyo ni mtu mwenye msimamo. Mtu mwenye kanuni.

Sioni kabisa usaliti wake.
 
Itawachukua muda mrefu sana hawa ndugu zetu kutambua hili na kukubali upekee wa mchango wa Dkt. Slaa katika kujenga upinzani. Sasa hivi wamekuwa kama kondoo wasio na mchungaji!
linganisha kura milioni mbili za mwaka 2010 na milioni sita za 2015
kama hata hujui hesabu za kujumlisha na kutoa mimi siwezi kukusaidia
 
Slaa hajabadilika.

Alimkataa Lowassa wakati Lowassa yupo CCM na akamkataa alipoenda CHADEMA.

Huyo ni mtu mwenye msimamo. Mtu mwenye kanuni.

Sioni kabisa usaliti wake.
Nisaidie kuelewa mkono wa kushoto wa Mbowe anaitwa nani huyo?
Alikuwa anafanya nini hapo?

Kama hakumkaribisha Lowassa alikuwa anafanya nini hapo?Si si asingekuwepo kabisa?

Mnaelewa kuwa kilichomtoa cdm ni baada ya kukataliwa kugombea urais!!!
Mmekuwa na nyinyi kama mmelishwa limbwata la kihaya shuntama
d06777c9-4a07-4ef9-9ce1-bdc6202508b9-jpeg.672363
 
linganisha kura milioni mbili za mwaka 2010 na milioni sita za 2015
kama hata hujui hesabu za kujumlisha na kutoa mimi siwezi kukusaidia
Kumbuka tu 2010 Chadema ilisimama peke yake, halafu 2015 viliungana vyama vingapi.?

Ukitaka kujua mchango wa Dr Slaa Nenda kwenye uchaguzi wa serikali za mtaa 2014......hapo ndio utajua hata kura na mafanikio ya 2015 mizizi ni 2014.

Huyo Lowasa amekuja kwenye shamba ambalo tayari limeshalimwa.
 
Back
Top Bottom