Fred Mwakitundu
JF-Expert Member
- Dec 31, 2018
- 227
- 383
Umeibuka mjadala mkubwa sana kwa wakazi wa mji wa moshi wengi wakihoji mamlaka za serikali kuwa kimyaa kutokana na Baa moja kubwa kujengwa ikipakana na ukuta wa Banki ya NBC Tawi la Kibo Mjini Moshi.
Wapo wanaotilia shaka uwepo wa Baa hiyo wakidai inaweza ikaharisha usalama wa wateja wanaotumia machine za nje za kuchukulia fedha(ATM) ambazo zipo kupakana na Baa hiyo wakireeja tukio baya lililoikumba banki hiyo mwaka 2004 ambako zaidi ya Bilioni 5.3 ziliporwa katika tukio ambalo linadaiwa lilisukwa vyema na watu mbali mbali wakiwamo wenye mamlaka ya kusimamia usalama wa raia na mali zao.
Baa hiyo imejengwa kwenye uwanja mkuwa unaomilikiwa na Chama Kikuu cha ushirika Mkoa wa Kilimanjaro(KNCU),uwanja ambao ni kama ulitelekezwa kwa miaka nenda rudi na kugeuzwa kichaka cha makahaba waliokuwa wakilandalanda kwenye club ya usiku ya Pub Alberto kutokana na KNCU kutokuwa na mikakati mizuri ya kuendeleza mali zake na kuondokana na hali ya utegemezi na kukopakopa kwenye mabenki licha ya kuwa na mali nyingi zinazokiwezesha kutokuwa kwenye kundi la ombo omba ama kopa kopa kama sasa.
Watu wanaojiita wananchi wanadai uwepo wa baa hiyo ni hatari kubwa kwa usalama wa fedha za wateja,wakidai baa hiyo inaweza ikatumiwa na wahrifu kupanga njama za kuwapora wateja wanaochukua fedha kwenye Banki hiyo hasa nyakati za usiku na kuzitaka mamla za serikali kuchukua hatua haraka kabla ya hatari wakiamini baa hiyo ipo eneo ambalo si rafiki kwa usalama wa wateja wa Banki hiyo.
"mwanzo tulidhani ni hiyo supermaket tu ndo anajenga na vibanda vya maduka lakini kumbe anajenga baa kubwa tena inajengwa kupakana na ukuta wa banki,hii siyo sawa kiusalama",anasema mtu mmoja .
Uongozi wa banki ya NBC Tawi la Moshi umekataa kutoa msimamo wake juu ya Baa hiyo kujengwa ikipakana na ukuta wa banki yao lakini ofisa mmoja wa banki hiyo aliyeomba kutotajwa jina lake amesema tayari banki kama benki imeshachukua hatu juu ya uwepo wa Ba hiyo karibu na Banki yao na kusisitiza kuwa wanalichukulia kwa uzito wa kipekee jambo hilo.
"Sisi kama banki tunaangalia mambo mawili moja ni je uwepo wa baa hiyo una faida gani kwetu kama banki na pia uwepo wa baa hiyo una madhara gani kwetu kama banki,sasa tukishamaliza kufanya uchanganuzi wetu tutajua tufanye nini?"
Anasema ofisa huyo kwamba uwepo wa baa hiyo karibu na benki yao unaweza kuwa na faida kwa maana ya wateja wao kuchukua pesa hapo hasa nyakati za usiku wakiwa katika baa hiyo na hiyo ni kwa upande mmoja na upande mwingine uwepo wa baa hiyo karibu na benki yao unaweza kuwa kichocheo cha wateja wao kulengwa na waharifu wanaoweza kutumia kichaka cha 'wateja' wa baa hiyo na kutekeleza uharifu.
Kwa faida tu ya wasomaji wa JF,mwaka 2004 uvamizi mkubwa ulifanywa kwenye banki hiyo ambako ziliporwa zaidi ya Bilioni 5.3,tukio lililohusisha raia wa kenya,polisi,wafanyabiashara na mtu mmoja aliyekuwa akijiita mchungaji wa makanisa ya Kipentekosta A.K.A Askofu Jumanne Kilongola mkazi wa Matejoo Arusha ambaye ni mmoja wa waliotupwa jela miaka 32 kwa makosa ya kula njama na kupora pesa hizo kwa kutumia silaha.
Katika tukio hilo raia wanne wa Kenya walihukumiwa miaka 32 jela ambao ni Wilfred Onyango Nganyi,Gabriel Kungu Kariuki,Jimmy Maina Njoroge na Simon Ndungu Kiambuthi wakati wakenya Michael Mbanya Wathigo,Boniface Mwangi Mburu na David Ngugi Mburu wakiachiliwa huru na mahakama iliyokuwa chini ya hakimu Simon Kobelo.
Konstebo wanne wa polisi kikosi cha FFU Moshi ambao walihusishwa kwenye uporaji huo ambao ni PC.Stide Kahamba,PC.Jovin Pius,PC.Seif Makono na PC.mohamed Mlunguya waliachiliwa huru .
Mfanyabaishara mkubwa wa madini ya tanzanite Jackson Ole Nemetemi,naye alitupwa jela miaka 32 kwa kupatikana na hatia hiyo ya kula njama na kupora kiasi hicho cha fedha .
Benjamin Julius Dia na nduguye Kelvin Julius Dia na Jacob Raphael Kallaghe walitupwa jela miaka 30 jela na kuchapwa viboko 12 klia mmoja wakati Happy Memei Laizer,Evelin John Mlaki(mke wa Nemetemi) walihukumiwa miaka mitatu jela baada ya kupatikana na mali inayodhaniwa kuwa ni ya wizi.
baada ya jamaa kupora fedha na kuondoka,walifika Arusha na kukodi Coaster na kutambaa nato hadi serengeti na k ulala kwenye hotel ya kitall ya Sopa Lodge ckama watalii na kesho yake wakavuka upande wa Kenya kupitia Hifahdi ya Taifa ya Amboseri Nchini Kenya.
Wapo wanaotilia shaka uwepo wa Baa hiyo wakidai inaweza ikaharisha usalama wa wateja wanaotumia machine za nje za kuchukulia fedha(ATM) ambazo zipo kupakana na Baa hiyo wakireeja tukio baya lililoikumba banki hiyo mwaka 2004 ambako zaidi ya Bilioni 5.3 ziliporwa katika tukio ambalo linadaiwa lilisukwa vyema na watu mbali mbali wakiwamo wenye mamlaka ya kusimamia usalama wa raia na mali zao.
Baa hiyo imejengwa kwenye uwanja mkuwa unaomilikiwa na Chama Kikuu cha ushirika Mkoa wa Kilimanjaro(KNCU),uwanja ambao ni kama ulitelekezwa kwa miaka nenda rudi na kugeuzwa kichaka cha makahaba waliokuwa wakilandalanda kwenye club ya usiku ya Pub Alberto kutokana na KNCU kutokuwa na mikakati mizuri ya kuendeleza mali zake na kuondokana na hali ya utegemezi na kukopakopa kwenye mabenki licha ya kuwa na mali nyingi zinazokiwezesha kutokuwa kwenye kundi la ombo omba ama kopa kopa kama sasa.
Watu wanaojiita wananchi wanadai uwepo wa baa hiyo ni hatari kubwa kwa usalama wa fedha za wateja,wakidai baa hiyo inaweza ikatumiwa na wahrifu kupanga njama za kuwapora wateja wanaochukua fedha kwenye Banki hiyo hasa nyakati za usiku na kuzitaka mamla za serikali kuchukua hatua haraka kabla ya hatari wakiamini baa hiyo ipo eneo ambalo si rafiki kwa usalama wa wateja wa Banki hiyo.
"mwanzo tulidhani ni hiyo supermaket tu ndo anajenga na vibanda vya maduka lakini kumbe anajenga baa kubwa tena inajengwa kupakana na ukuta wa banki,hii siyo sawa kiusalama",anasema mtu mmoja .
Uongozi wa banki ya NBC Tawi la Moshi umekataa kutoa msimamo wake juu ya Baa hiyo kujengwa ikipakana na ukuta wa banki yao lakini ofisa mmoja wa banki hiyo aliyeomba kutotajwa jina lake amesema tayari banki kama benki imeshachukua hatu juu ya uwepo wa Ba hiyo karibu na Banki yao na kusisitiza kuwa wanalichukulia kwa uzito wa kipekee jambo hilo.
"Sisi kama banki tunaangalia mambo mawili moja ni je uwepo wa baa hiyo una faida gani kwetu kama banki na pia uwepo wa baa hiyo una madhara gani kwetu kama banki,sasa tukishamaliza kufanya uchanganuzi wetu tutajua tufanye nini?"
Anasema ofisa huyo kwamba uwepo wa baa hiyo karibu na benki yao unaweza kuwa na faida kwa maana ya wateja wao kuchukua pesa hapo hasa nyakati za usiku wakiwa katika baa hiyo na hiyo ni kwa upande mmoja na upande mwingine uwepo wa baa hiyo karibu na benki yao unaweza kuwa kichocheo cha wateja wao kulengwa na waharifu wanaoweza kutumia kichaka cha 'wateja' wa baa hiyo na kutekeleza uharifu.
Kwa faida tu ya wasomaji wa JF,mwaka 2004 uvamizi mkubwa ulifanywa kwenye banki hiyo ambako ziliporwa zaidi ya Bilioni 5.3,tukio lililohusisha raia wa kenya,polisi,wafanyabiashara na mtu mmoja aliyekuwa akijiita mchungaji wa makanisa ya Kipentekosta A.K.A Askofu Jumanne Kilongola mkazi wa Matejoo Arusha ambaye ni mmoja wa waliotupwa jela miaka 32 kwa makosa ya kula njama na kupora pesa hizo kwa kutumia silaha.
Katika tukio hilo raia wanne wa Kenya walihukumiwa miaka 32 jela ambao ni Wilfred Onyango Nganyi,Gabriel Kungu Kariuki,Jimmy Maina Njoroge na Simon Ndungu Kiambuthi wakati wakenya Michael Mbanya Wathigo,Boniface Mwangi Mburu na David Ngugi Mburu wakiachiliwa huru na mahakama iliyokuwa chini ya hakimu Simon Kobelo.
Konstebo wanne wa polisi kikosi cha FFU Moshi ambao walihusishwa kwenye uporaji huo ambao ni PC.Stide Kahamba,PC.Jovin Pius,PC.Seif Makono na PC.mohamed Mlunguya waliachiliwa huru .
Mfanyabaishara mkubwa wa madini ya tanzanite Jackson Ole Nemetemi,naye alitupwa jela miaka 32 kwa kupatikana na hatia hiyo ya kula njama na kupora kiasi hicho cha fedha .
Benjamin Julius Dia na nduguye Kelvin Julius Dia na Jacob Raphael Kallaghe walitupwa jela miaka 30 jela na kuchapwa viboko 12 klia mmoja wakati Happy Memei Laizer,Evelin John Mlaki(mke wa Nemetemi) walihukumiwa miaka mitatu jela baada ya kupatikana na mali inayodhaniwa kuwa ni ya wizi.
baada ya jamaa kupora fedha na kuondoka,walifika Arusha na kukodi Coaster na kutambaa nato hadi serengeti na k ulala kwenye hotel ya kitall ya Sopa Lodge ckama watalii na kesho yake wakavuka upande wa Kenya kupitia Hifahdi ya Taifa ya Amboseri Nchini Kenya.