Usalama wa barakoa protective coveralls upoje?

Usalama wa barakoa protective coveralls upoje?

PAZIA 3

JF-Expert Member
Joined
Jan 30, 2018
Posts
1,104
Reaction score
1,924
Ni swali dogo ila gumu ki mantiki, Kama Corona viruses wanaweza kukaa kwenye kitu chochote na kwenye hewa zaidi ya masaa matatu, je usalama wa waaguzi na wahanga upoje?

Ndiyo kusema zile coats/ protective gears wanazotumia Madaktari haziwezi shikwa na Hawa viruses? Kama jibu Ni ndiyo, Ni chemicali gani zimetumika kuzitengenezea ambazo zitumike pia Kama Kinga kwa ugonjwa huu?

Kama jibu Ni hapana, kumbe Kuna uwezekano hizo barakoa, overall coats na ambulance zinaweza kuwa chanzo Cha kueneza virusi Hawa? Nani anitoe wasiwasi huu!!?
 
huwa wanazisafisha kwa dawa kila baada ya muda fulani
Ndiyo kumaanisha hiyo dawa inaua hao virusi? Kwanini tunaambiwa Hamna dawa ya kupambana na Corona viruses? Zaidi tunaambiwa wanatibu dalili nyemelezi?
 
Ndiyo kumaanisha hiyo dawa inaua hao virusi? Kwanini tunaambiwa Hamna dawa ya kupambana na Corona viruses? Zaidi tunaambiwa wanatibu dalili nyemelezi?
sabuni na sanitizer zinatumika kusafisha maeneo ya nje ya mwili kupambana na majimaji yanayohisiwa kuwa na virusi vya korona.

huwezi kunywa sabuni kama dawa ya korona.
 
sabuni na sanitizer zinatumika kusafisha maeneo ya nje ya mwili kupambana na majimaji yanayohisiwa kuwa na virusi vya korona.

huwezi kunywa sabuni kama dawa ya korona.
Unazani sijui mkuu? Shida Ni kwamba, taarifa zidi ya virusi Hawa inachanganya Sana, Kama virusi vina uwezo wa kukaa sehemu yoyote, inamaana ukinawa kwa sanitizer si wanadondoka chini? Wakiwa hapo chini wanakufa au hawana uwezo wa kusavive kwenye majimaji? Nini maana ya kusema hakuna dawa ya kumuua Corona virus? Kama ukinawa na kupuliza hizo dawa je huyo virus anakufa, ndo swali langu lilopo
 
Yaani kwa akili yangu tu ya darasa la ²à nimeelewa kwamba haiyumkini dawa ya kumuua kirusi Covid'19 ipo ikiwa ni pamoja na sabuni au sanitizers na dawa nyingine nyingi tu za kimaabala,,

Kwamba kinachotafutwa ni dawa ya kumuua kirusi mwenyewe akishaingia mwilini mwa mtu bila kusababisha athari yoyote,,

Kwamba pengine dawa zinazoweza kuua virusi wakishaingia mwilini akipewa mgonjwa hazitaua virusi peke yake bali na cells nyingine zenye kukinga mwili hivyo kupelekea kifo kwa mgonjwa,, tayari mpaka hapo haitakua dawa tena bali sumu,,
 
Unazani sijui mkuu? Shida Ni kwamba, taarifa zidi ya virusi Hawa inachanganya Sana, Kama virusi vina uwezo wa kukaa sehemu yoyote, inamaana ukinawa kwa sanitizer si wanadondoka chini? Wakiwa hapo chini wanakufa au hawana uwezo wa kusavive kwenye majimaji? Nini maana ya kusema hakuna dawa ya kumuua Corona virus? Kama ukinawa na kupuliza hizo dawa je huyo virus anakufa, ndo swali langu lilopo
aisee

Sent From Galaxy S9
 
Back
Top Bottom